Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 8

Wanakimbia Mutawala Mukali

Wanakimbia Mutawala Mukali

MATAYO 2:13-23

  • FAMILIA YA YESU INAKIMBILIA MISRI

  • YOSEFU ANAHAMIA NAZARETI PAMOJA NA FAMILIA YAKE

Yosefu anamuamusha Maria ili kumupatia ujumbe wa haraka. Malaika wa Yehova ametoka tu kumutokea Yosefu katika ndoto na kumuambia hivi: “Simama, chukua ule mutoto mudogo na mama yake na ukimbilie Misri, na ukae kule mupaka wakati nitakuambia urudie; kwa maana Herode iko karibu kutafuta ule mutoto mudogo ili amuue.”—Matayo 2:13.

Bila kukawia, Yosefu, Maria na mutoto wao wanakimbia usiku. Wanafanya hivyo mbele ya wakati, kwa sababu Herode anatambua kama wanaume hao wenye elimu ya nyota wamemudanganya. Alikuwa amewaambia wamuletee habari. Lakini, walitoka katika inchi bila kufanya hivyo. Herode anakasirika sana. Kwa sababu anapenda kumuua Yesu, anatoa amri ya kuua watoto wote wanaume wa miaka mbili na kushuka wenye kuwa katika Betlehemu na maeneo yenye kuzunguka Betlehemu. Uamuzi huo ulitegemea habari yenye alisikia kupitia watu wenye elimu ya nyota wenye walitoka Mashariki.

Kuua watoto wote wanaume ni jambo lenye kuumiza sana! Hatuwezi kujua ni watoto ngapi waliuawa, lakini machozi na kilio cha mama wenye huzuni vinatimiza unabii wa Biblia wenye ulitolewa na Yeremia, nabii wa Mungu.—Yeremia 31:15.

Wakati huo, Yosefu na familia yake walikuwa wamekimbilia Misri, na wanaendelea kuishi huko. Kisha, usiku fulani malaika wa Yehova anamutokea tena Yosefu katika ndoto. Malaika huyo anamuambia hivi: “Simama, chukua ule mutoto na mama yake na uende katika inchi ya Israeli, kwa sababu wale wenye walikuwa wanatafuta uzima wa ule mutoto wamekufa.” (Matayo 2:20) Kwa hiyo, Yosefu anaamua sasa kama familia inaweza kurudia katika inchi yao. Hilo linatimiza unabii mwingine wa Biblia: Mwana wa Mungu anaitwa kutoka Misri.—Hosea 11:1.

Inaonekana Yosefu anapanga kuishi na familia yake katika Yudea, pengine karibu na muji wa Betlehemu kwenye walikuwa wanaishi mbele wakimbilie Misri. Lakini anasikia kuwa mutoto muovu wa Herode mwenye kuitwa Arkelao ndiye sasa mufalme wa Yudea. Katika ndoto ingine, Mungu anamuonya Yosefu juu ya hatari ya kuenda Yudea. Kwa hiyo Yosefu na familia yake wanasafiri kuenda mbali kaskazini na wanakaa katika muji wa Nazareti katika eneo la Galilaya, mbali na makao makubwa ya maisha ya kidini ya Wayahudi. Yesu anakomalia katika eneo hilo, na hilo linatimiza unabii mwingine wa Biblia wenye kusema: “Ataitwa Munazareti.”—Matayo 2:23.