Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 10

Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu

Yesu na Familia Yake Wanasafiri Kuenda Yerusalemu

LUKA 2:40-52

  • YESU MWENYE KUWA NA MIAKA KUMI NA MBILI ANAULIZA WALIMU MAULIZO

  • YESU ANAMUITA YEHOVA “BABA YANGU”

Ni wakati wa kipindi cha kuchipuka kwa majani. Kwa hiyo, wakati umefika ili familia ya Yosefu, pamoja na marafiki na watu wa jamaa wafanye safari yao ya kila mwaka ya kuenda Yerusalemu. Wanaenda huko kwa ajili ya sherehe ya Pasaka, kama vile Sheria inaomba. (Kumbukumbu la Torati 16:16) Kutoka Nazareti mupaka Yerusalemu ni safari ya kilometre karibu 120. Ni wakati wenye mambo mengi na wenye kufurahisha kwa watu wote. Yesu, mwenye iko sasa na miaka 12, anangojea kwa hamu sana sherehe hiyo na nafasi ya kuwa tena kwenye hekalu.

Yesu na familia yake, hawaone Pasaka kuwa tu tukio la siku moja. Kisha siku ya Pasaka, ni mwanzo wa Sherehe ya Mikate Yenye Haina Chachu yenye inachukua siku saba. (Marko 14:1) Tukio hilo linaonwa kuwa sehemu ya kipindi cha Pasaka. Safari ya kutoka nyumbani kuenda Nazareti, kubakia katika Yerusalemu, na kurudia kwao, inachukua karibu majuma mbili. Lakini mwaka huu, kwa sababu ya jambo fulani lenye linamuhusu Yesu, safari hiyo inachukua zaidi ya majuma mbili. Inakuwa hivyo kwa sababu ya tatizo fulani lenye linatokea wakati wako wanarudia kutoka Yerusalemu.

Wakati wako katika safari, Yosefu na Maria wanawaza kuwa Yesu iko katika kikundi cha marafiki na watu wa familia wenye kusafiri kuenda upande wa kaskazini. Lakini, wakati wanasimamisha safari kwa sababu ya usiku, hawamuone. Kwa hiyo, wanaenda kumutafuta kati ya marafiki, lakini haonekane. Mutoto wao haonekane nafasi hata moja! Kwa hiyo, Yosefu na Maria wanarudia Yerusalemu ili kumutafuta.

Wanamutafuta siku nzima, lakini hawamupate. Wanamutafuta tena siku ya pili, hawamupate. Mwishowe, katika siku ya tatu, wanapata mutoto wao katika hekalu lenye vyumba vingi. Wanaona Yesu amekaa katikati ya walimu fulani Wayahudi. Iko anawasikiliza, anawauliza maulizo, na kuwashangaza na ujuzi wake.

Maria anamuuliza hivi: “Mutoto wangu, sababu gani umetutendea hivi? Mimi na baba yako tumekutafuta tukiwa na wasiwasi sana.”—Luka 2:48.

Yesu anashangaa kusikia kama hawakujua nafasi kwenye angekuwa. Anauliza hivi: “Sababu gani mulikuwa munanitafuta? Je, hamukujua kama ninapaswa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”—Luka 2:49.

Sasa wako tena pamoja, Yesu anarudia nyumbani pamoja na Yosefu na Maria na anaendelea kujitiisha kwao. Anaendelea kuwa na hekima zaidi na kukomaa kimwili. Hata kama angali kijana, anakubaliwa na Mungu na wanadamu. Ndiyo, tangu utoto wake na kuendelea, Yesu anaonyesha mufano muzuri, haiko tu katika kupendezwa na mambo ya kiroho, lakini pia kuheshimia wazazi wake.