Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 9

Anakomalia Katika Nazareti

Anakomalia Katika Nazareti

MATAYO 13:55, 56 MARKO 6:3

  • FAMILIA YA YOSEFU NA MARIA INAONGEZEKA

  • YESU ANAJIFUNZA KUFANYA KAZI

Yesu anakomalia katika Nazareti, muji mudogo na wenye hauko wa maana. Unapatikana kaskazini mwa Yudea, katika vilima vya eneo lenye kuitwa Galilaya, mangaribi mwa bahari kubwa yenye kuitwa Bahari ya Galilaya.

Wakati iko pengine na miaka mbili, Yosefu na Maria wanamutosha Yesu Misri na kuenda naye Nazareti. Inaonekana kuwa wakati huo ni Yesu tu ndiye mutoto wao. Lakini kisha, ndugu-nusu za Yesu wanazaliwa pia: Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda. Yosefu na Maria wanazaa pia watoto wanamuke, dada-nusu wa Yesu. Ndiyo, Yesu iko na wadogo yake sita hivi, wanaume na wanamuke.

Bila shaka, Yesu iko na watu wengine wa jamaa. Tumekwisha kuzungumuzia Elizabeti na mutoto wake, Yohana. Yohana anaishi kwenye kilometre nyingi kusini, ni kusema, katika Yudea. Salome yeye anaishi karibu na Galilaya, na inawezekana ni dada yake na Maria, na kwa hiyo ni shangazi yake na Yesu. Bwana yake na Salome ni Zebedayo. Watoto wao wawili, Yakobo na Yohana, wanaonekana kuwa wao ndio binamu (cousins) wa Yesu. Hatujue ikiwa Yesu anapitisha wakati mwingi pamoja nao wakati wako wanakomaa, lakini wanafikia kuwa marafiki wake wa sana, na wawili kati ya mitume wa Yesu.

Yosefu anapaswa kutumika sana ili kutegemeza familia yake yenye inaongezeka. Anafanya kazi ya useremala. Yosefu anamulea Yesu kama mutoto wake mwenyewe, ndiyo sababu anaitwa “mwana wa ule seremala.” (Matayo 13:55) Yosefu anafundisha pia Yesu kazi ya useremala, na Yesu anaijua muzuri. Ndiyo sababu, watu wanafikia kusema juu ya Yesu: “Huyu ni ule seremala.”—Marko 6:3.

Familia ya Yosefu inatia ibada ya Yehova pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. Kwa kutii Sheria ya Mungu, Yosefu na Maria wanafundisha watoto wao mambo ya kiroho ‘wakati wanakaa katika nyumba yao na wakati wanatembea katika barabara na wakati wanalala na wakati wanaamuka.’ (Kumbukumbu la Torati 6:6-9) Katika Nazareti kuko sinagogi. Tunaweza kuwa hakika kama Yosefu na familia yake wanaenda katika sinagogi hiyo kwa ajili ya ibada. Biblia inasema kama “kulingana na desturi yake siku ya Sabato,” Yesu alienda katika sinagogi. (Luka 4:16) Pia, familia inafurahi kufanya safari za kuenda kwa ukawaida kwenye hekalu katika Yerusalemu.