Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 6

Mutoto Mwenye Aliahidiwa

Mutoto Mwenye Aliahidiwa

LUKA 2:21-39

  • YESU ANATAHIRIWA NA KISHA ANAPELEKWA KWENYE HEKALU

Yosefu na Maria wanabakia Betlehemu kuliko kurudia Nazareti. Wakati Yesu anakuwa na siku munane, anatahiriwa kulingana na Sheria ya Mungu kwa Waisraeli. (Mambo ya Walawi 12:2, 3) Kulingana na desturi, hiyo ilikuwa pia siku ya kumupatia mutoto jina. Wanaita mutoto wao Yesu, kama vile malaika Gabrieli aliwaambia.

Kumepita zaidi ya mwezi moja, na Yesu iko sasa na siku 40 tangu kuzaliwa kwake. Sasa, wazazi wake wanamupeleka wapi? Wanamupeleka kwenye hekalu katika Yerusalemu, kwenye kilometre kidogo na mahali kwenye wanaishi. Sheria inasema kama siku 40 kisha kuzala mutoto mwanaume, mama aliombwa kutoa toleo la utakaso kwenye hekalu.—Mambo ya Walawi 12:4-8.

Maria anafanya hivyo. Toleo lake, ni ndege wawili wadogo. Hilo linatusaidia kuelewa hali ya maisha yenye Yosefu na Maria walikuwa nayo. Kulingana na Sheria, iliomba kutoa mwana-kondoo dume na ndege. Lakini kama mama hana uwezo wa kupata kondoo dume, angetoa njiwa (pigeon) ao njiwa-tetere (tourterelle) mbili. Maria alijikuta katika hali hiyo na alitoa kulingana na hali yake.

Kwenye hekalu, mwanaume moja mwenye kuzeeka anakaribia Yosefu na Maria. Jina lake Simeoni. Mungu alimufunulia kwamba mbele akufe, atamuona Kristo, ao Masiya mwenye aliahidiwa na Yehova. Siku hii roho takatifu inamuongoza Simeoni aende kwenye hekalu; anakuta Yosefu na Maria pamoja na mutoto wao. Simeoni anachukua mutoto katika mikono yake.

Wakati iko na Yesu katika mikono, Simeoni anamushukuru Mungu, na kusema: “Sasa, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, mutumwa wako anaweza sasa kufa kwa amani kama vile ulisema, kwa sababu macho yangu yameona njia yako ya wokovu yenye umetayarisha ili ionekane na watu wote, mwangaza wa kuondoa kitambaa chenye kinafunika mataifa, na utukufu wa watu wako Israeli.”—Luka 2:29-32.

Yosefu na Maria wanashangaa kusikia maneno hayo. Simeoni anawabariki na anamuambia Maria kwamba mutoto wake “atawekwa kwa ajili ya kuanguka na kusimama tena kwa wengi katika Israeli” na uchungu, kama upanga murefu, utaingizwa ndani yake.—Luka 2:34.

Kuko mutu mwengine kwenye hekalu siku hiyo. Jina lake Ana, nabii mwanamuke wa miaka 84. Hakosake hata siku moja kuwa kwenye hekalu. Sasa, anakuja kukutana na Yosefu, Maria, na mutoto Yesu. Ana anaanza kumushukuru Mungu na kuzungumuza na wote wenye wanamusikiliza juu ya Yesu.

Wazia namna Yosefu na Maria wanafurahia mambo hayo yote yenye yanatokea kwenye hekalu! Bila shaka, mambo yote hayo yanawahakikishia kwamba mutoto wao ni Mwenye Aliahidiwa na Mungu.