Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 3

Mutu Fulani wa Kutayarisha Njia Anazaliwa

Mutu Fulani wa Kutayarisha Njia Anazaliwa

LUKA 1:57-79

  • YOHANA MUBATIZAJI ANAZALIWA NA KUPEWA JINA

  • ZEKARIA ANATABIRI DARAKA LENYE YOHANA ATAKUWA NALO

Elizabeti anakuwa karibu kuzaa mutoto wake. Maria amebakia pamoja naye kwa muda wa miezi tatu. Sasa ni wakati wa Maria kumuacha Elizabeti na kuanza safari ndefu kuelekea kaskazini ili kurudia Nazareti, mahali kwenye alikuwa anaishi. Kunabakia karibu miezi sita ili yeye pia azae.

Muda kidogo tu kisha Maria kuenda, Elizabeti anazaa. Ni jambo lenye kufurahisha kuona namna mutoto anazaliwa bila shida na Elizabeti na mutoto wake ni wenye afya ya muzuri! Wakati Elizabeti anaonyesha mutoto wake kwa majirani na watu wa jamaa yake, wote wanafurahi pamoja naye.

Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli ilisema kama siku munane kisha mutoto mwanaume kuzaliwa, mutoto huyo anapaswa kutahiriwa, na kisha kupewa jina. (Mambo ya Walawi 12:2, 3) Watu fulani wanawaza kama mutoto wa Zekaria anapaswa kuchukua jina la baba yake. Lakini, Elizabeti anawaambia hivi: “Hapana! ataitwa Yohana.” (Luka 1:60) Kumbuka kwamba malaika Gabrieli alisema kama mutoto huyo anapaswa kuitwa Yohana.

Majirani na watu wa jamaa wanakataa na kusema hivi: “Hakuna mutu wa jamaa yako mwenye anaitwa kwa jina hilo.” (Luka 1:61) Wanamuuliza Zekaria kwa kufanya ishara, ili aonyeshe jina lenye anapenda kumupatia mutoto wake. Zekaria anaomba kibao na kuandika hivi: “Jina lake Yohana.”—Luka 1:63.

Kisha hapo, Zekaria akaanza tena kusema kwa njia ya muujiza. Unakumbuka? Zekaria alipoteza uwezo wake wa kusema wakati hakuamini maneno ya malaika yenye kuonyesha kama Elizabeti angezaa mutoto. Sasa, wakati Zekaria anaanza tena kusema, majirani wanashangaa na kusema hivi: “Mutoto huyu mudogo atakuwa mutu wa namna gani?” (Luka 1:66) Wanaona mukono wa Mungu katika namna Yohana alipewa jina.

Kisha, Zekaria anajazwa roho takatifu na kusema hivi: “Yehova asifiwe, Mungu wa Israeli, kwa sababu ameelekeza uangalifu wake kwa watu wake na amewaletea ukombozi. Na ametuinulia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mutumishi wake.” (Luka 1:68, 69) Kwa kusema maneno “pembe ya wokovu,” anamaanisha Bwana Yesu, mwenye alikuwa karibu kuzaliwa. Zekaria anasema kama kupitia Huyo, Mungu ‘atatukomboa kutoka katika mikono ya maadui wetu, atatupatia pendeleo la kumutolea bila woga utumishi mutakatifu kwa ushikamanifu na kwa kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele yake siku zetu zote.’—Luka 1:74, 75.

Kuhusu mutoto wake, Zekaria anatabiri hivi: “Lakini wewe, mutoto mudogo, utaitwa nabii wa Mwenye Kuwa Juu Zaidi, kwa maana utaenda mbele ya Yehova ili kutayarisha njia zake, kutangazia watu wake kwamba atawaokoa kwa kuwasamehe zambi zao, kwa sababu ya huruma nyingi za Mungu wetu. Kupitia huruma hizo mwangaza wa asubui utatufikia kutoka juu, ili kuangazia wale wenye kukaa katika giza na katika kivuli chenye kuleta kifo na kuongoza miguu yetu katika njia ya amani.” (Luka 1:76-79) Ni unabii wenye kutia moyo kabisa!

Sasa, Maria mwenye kwa kweli hajaolewa, anafika Nazareti, mahali kwenye alikuwa anaishi. Mambo yatakuwa namna gani wakati itajulikana kama iko na mimba?