Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 4

Maria Iko na Mimba Lakini Hajaolewa

Maria Iko na Mimba Lakini Hajaolewa

MATAYO 1:18-25 LUKA 1:56

  • YOSEFU ANASIKIA KAMA MARIA IKO NA MIMBA

  • MARIA ANAKUWA BIBI YA YOSEFU

Maria iko sasa katika mwezi wake wa 4 tangu alipata mimba. Kumbuka kama alipitisha miezi ya kwanza ya mimba yake pamoja na Elizabeti mutu wa jamaa yake, katika vilima vya Yudea, sehemu za kusini. Lakini sasa, Maria amerudia Nazareti, kwenye alikuwa anaishi. Hivi karibuni, watu wote watajua kama iko na mimba. Wazia namna jambo hilo linamuhangaisha!

Jambo lenye kuhangaisha zaidi ni kwamba Maria anachumbiwa na seremala mumoja mwenye kuitwa Yosefu. Na anajua kama kulingana na Sheria yenye Mungu alipatia Waisraeli, mwanamuke mwenye kuchumbiwa lakini anafanya uasherati kimakusudi na mwanaume mwengine anapaswa kuuawa kwa kupigwa majiwe. (Kumbukumbu la Torati 22:23, 24) Lakini, hata kama Maria hakufanya uasherati, pengine anajiuliza namna atamuelezea Yosefu kuhusu mimba yake na anajiuliza mambo yatakuwa namna gani.

Yosefu hakumuona Maria muda wa miezi tatu; kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kama iko na hamu ya kumuona. Wakati wanakutana, inawezekana Maria anamuelezea hali yake, na anajikaza kumuelezea kwamba alipata mimba kwa nguvu za roho takatifu ya Mungu. Hata hivyo, kama vile unaweza kuona, ni vigumu sana kwa Yosefu kuelewa na kuamini jambo hilo.

Yosefu anajua kama Maria ni mwanamuke muzuri na kama iko na mwenendo muzuri. Na anamupenda sana. Lakini Yosefu anawaza tu kwamba kuko mwanaume mwenye alimupatia ile mimba. Yosefu hapendi Maria apigwe majiwe na kuuawa ao apate haya mbele ya watu wote; kwa hiyo anapenda kuvunja ndoa yao kwa siri. Katika siku hizo, watu wenye kuchumbiana walionwa kuwa watu wenye kufunga ndoa, na talaka (divorce) iliombwa ili kumaliza uchumba.

Kisha, wakati Yosefu angali anafikiria kwa uzito jambo hilo, anaenda kulala. Malaika wa Yehova anamutokea katika ndoto na kumuambia: “Usiogope kumuchukua Maria bibi yako na kumupeleka kwako, kwa maana mimba yenye iko nayo ameipata kupitia roho takatifu. Atazaa mwana, na utamupatia jina Yesu, kwa maana ataokoa watu wake katika zambi zao.”—Matayo 1:20, 21.

Wakati Yosefu anaamuka, anashukuru sana kuona namna sasa mambo yanakuwa wazi zaidi! Bila kukawia anatenda kulingana na muongozo wa malaika. Anamuchukua Maria na kumupeleka nyumbani kwake. Hilo ni tendo la wazi lenye kuonyesha kama wamefunga ndoa, na kwamba Yosefu na Maria wamekuwa sasa bibi na bwana. Hata hivyo, Yosefu halale na Maria wakati iko na mimba ya Yesu.

Miezi fulani kisha hapo, Yosefu na Maria, mwenye kuwa muzito kwa sababu ya mimba, wanapaswa kujitayarisha ili kuenda mbali na Nazareti, mahali kwenye walikuwa wanaishi. Wanaenda wapi wakati Maria iko karibu kuzaa?