Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 14

Yesu Anaanza Kufanya Wanafunzi

Yesu Anaanza Kufanya Wanafunzi

YOHANA 1:29-51

  • WANAFUNZI WA KWANZA WA YESU WANAJIUNGA NAYE

Kisha kufanya siku 40 katika jangwa na mbele ya kurudia Galilaya, Yesu anaenda tena kumuona Yohana, mwenye alimubatiza. Wakati Yesu anakaribia, Yohana anamuonyesha kwa watu na kusema hivi: “Ona, Mwana-Kondoo wa Mungu mwenye anatosha zambi ya ulimwengu! Huyu ndiye nilisema juu yake: ‘Kuko mwanaume mwenye anakuja nyuma yangu mwenye ametangulia mbele yangu, kwa maana alikuwa mbele yangu.’” (Yohana 1:29, 30) Hata kama ni Yohana ndiye mukubwa kidogo kuliko Yesu, anajua kama Yesu aliishi mbele yake wakati alikuwa mutu wa roho huko mbinguni.

Majuma kidogo mbele ya hapo, wakati Yesu alikuja kubatizwa, Yohana alionekana kuwa mwenye mashaka kwamba Yesu ndiye Masiya. Yohana anasema hivi: “Hata mimi sikumujua, lakini nilikuja kubatiza katika maji ili afunuliwe kwa Israeli.”—Yohana 1:31.

Yohana anaendelea kuelezea wasikilizaji wake mambo yenye yalifanyika wakati alimubatiza Yesu. Anasema hivi: “Niliona roho ikishuka kama njiwa kutoka mbinguni, na ikakaa juu yake. Hata mimi sikumujua, lakini Ule mwenye alinituma nibatize katika maji aliniambia: ‘Mutu yeyote mwenye utaona roho inashuka na kukaa juu yake, huyo ndiye mwenye anabatiza katika roho takatifu.”—Yohana 1:32-34

Yohana iko pamoja na wanafunzi wake wawili siku ya pili wakati Yesu anakaribia kwenye iko. Yohana anasema hivi: “Ona, Mwana-Kondoo wa Mungu!” (Yohana 1:36) Kwa hiyo, wanafunzi hao wawili wa Yohana Mubatizaji wanamufuata Yesu. Mumoja wa wanafunzi hao ni Andrea. Inawezekana mwanafunzi mwengine ni ule mwenye aliandika tukio hili, mwenye anaitwa pia Yohana. Inaonekana kama huyu Yohana ni binamu ya Yesu, mwana wa Salome. Inawezekana Salome ni dada yake na Maria, na bwana yake ni Zebedayo.

Wakati anageuka na kuona Andrea na Yohana wanamufuata, Yesu anawauliza: “Munatafuta nini?”

Wanamuuliza, “Rabi, unakaa wapi?”

Yesu anawajibu, “Mukuje na mutaona.”—Yohana 1:37-39.

Ni karibu saa ya kumi ya mangaribi, na Andrea na Yohana wanabakia pamoja na Yesu mupaka mwisho wa siku hiyo. Andrea anafurahi sana hivi kwamba wakati anamuona ndugu yake Simoni, mwenye kuitwa pia Petro, anamuambia: “Tumemupata Masiya.” (Yohana 1:41) Andrea anaenda na Petro kwa Yesu. Matukio yenye kufuata yanaonyesha kwamba Yohana pia anakutana na ndugu yake mwenye kuitwa Yakobo na kumupeleka kwa Yesu; lakini, Yohana hazungumuzie jambo hilo katika maandishi yake.

Siku yenye kufuata, Yesu anakutana na Filipo, wa muji wa Betsaida. Muji huo unapatikana karibu na inchi kavu ya kaskazini mwa Bahari ya Galilaya na ni muji wa Andrea na Petro. Yesu anamualika Filipo: “Kuwa mufuasi wangu.”—Yohana 1:43.

Kisha Filipo anakutana na Natanaeli, mwenye anaitwa pia Bartolomayo, na kumuambia hivi: “Tumemupata ule mwenye Musa, katika Sheria, na Manabii waliandika juu yake: Yesu, mwana wa Yosefu, kutoka Nazareti.” Natanaeli ni mwenye mashaka na anamuambia Filipo hivi: “Je, kuko kitu kizuri chenye kinaweza kutoka Nazareti?”

Filipo anamuambia, “Kuja na uone.” Yesu anamuona Natanaeli na kusema hivi: “Ona, Mwisraeli wa kweli mwenye hana udanganyifu ndani yake.”

Natanaeli anamuuliza, “Umenijua namna gani?”

Yesu anamujibu: “Mbele Filipo akuite, wakati ulikuwa chini ya muti wa tini, nilikuona.”

Kwa kushangaa Natanaeli anamujibu hivi: “Rabi, wewe ni Mwana wa Mungu, wewe ni Mufalme wa Israeli.”

Yesu anamuuliza hivi: “Je, unaamini kwa sababu nimekuambia nilikuona chini ya muti wa tini? Utaona mambo makubwa kuliko haya.” Kisha Yesu anatoa ahadi hii: “Kwa kweli kabisa ninawaambia nyinyi, mutaona mbingu imefunguliwa na malaika wa Mungu wakipanda na kushuka kwenye Mwana wa binadamu iko.”—Yohana 1:45-51.

Muda kidogo tu kisha hapo, Yesu, pamoja na wanafunzi wake wapya wenye ametoka tu kupata, wanatoka katika Bonde la Yordani na wanasafiri kuenda Galilaya.