Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 16

Yesu Anaonyesha Bidii kwa Ajili ya Ibada ya Kweli

Yesu Anaonyesha Bidii kwa Ajili ya Ibada ya Kweli

YOHANA 2:12-22

  • YESU ANASAFISHA HEKALU

Kisha karamu ya ndoa katika Kana, Yesu anaenda Kapernaumu. Mama yake na Yesu na ndugu-nusu zake: Yakobo, Yosefu, Simoni, na Yuda, wanasafiri pamoja naye.

Lakini sababu gani Yesu anaenda Kapernaumu? Muji huo unapatikana mahali penye kujulikana zaidi kuliko Nazareti ao Kana na unaonekana kuwa mukubwa zaidi. Pia, wengi kati ya wanafunzi wapya wa Yesu wanaishi Kapernaumu ao karibu na muji huo. Kwa hiyo, Yesu anaweza kuwatolea mazoezi fulani katika eneo lao.

Wakati iko katika Kapernaumu, Yesu pia anafanya kazi za ajabu. Kwa hiyo watu wengi wa muji huo na maeneo ya karibu wanasikia kuhusu mambo yenye Yesu anafanya katika Kapernaumu. Lakini Yesu na marafiki wake, ambao ni wanaume Wayahudi washikamanifu, wanapaswa kuenda bila kukawia katika Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu.

Wakati wako kwenye hekalu katika Yerusalemu, wanafunzi wa Yesu wanaona jambo fulani lenye Yesu anafanya ambalo linawashangaza sana, jambo lenye kuwa tofauti na lile waliona mbele ya hapo.

Sheria ya Mungu inaomba Waisraeli kufanya matoleo ya wanyama kwenye hekalu, na wageni wako na lazima ya kuwa na chakula katika siku zote zenye watafanya huko. Kwa hiyo, Sheria inaruhusu wale wenye kutoka mbali ili kuenda Yerusalemu, wakuwe na feza za kutumia ili kuuza “ngombe, kondoo, mbuzi,” na vitu vingine vya lazima katika siku zote zenye watafanya katika muji huo. (Kumbukumbu la Torati 14:24-26) Kwa hiyo, wafanyabiashara wenye kuwa katika Yerusalemu wanauzisha wanyama ao ndege ndani ya uwanja mukubwa wa hekalu. Na wamoja kati yao wanaiba watu kwa kuuzisha vitu kwa bei ya juu sana.

Yesu anakasirika; kwa hiyo, anamwanga feza za vichele za wale wenye kubadilisha feza, anapindua meza zao, na kuwafukuza inje. Kisha, Yesu anawaambia hivi: “Mutoshe vitu hivi hapa! Muache kufanya nyumba ya Baba yangu kuwa nyumba ya biashara!”—Yohana 2:16.

Wakati wanafunzi wa Yesu wanaona jambo hilo, wanakumbuka unabii kuhusu Mwana wa Mungu: “Bidii kwa ajili ya nyumba yako itanikula.” Lakini Wayahudi wanamuuliza hivi: “Unaweza kutuonyesha alama gani, kwa sababu unafanya mambo haya?” Yesu anawajibu: “Mubomoe hekalu hili, na kwa siku tatu nitalisimamisha.”—Yohana 2:17-19; Zaburi 69:9.

Wayahudi wanawaza kuwa Yesu anazungumuzia hekalu lenye walikuwa wanaona kwa macho yao lenye kuwa katika Yerusalemu, kwa hiyo wanauliza hivi: “Hekalu hili lilijengwa kwa miaka makumi ine na sita (46), na je, wewe utalisimamisha kwa siku tatu (3) ?” (Yohana 2:20) Lakini, Yesu iko anafananisha mwili wake na hekalu. Miaka tatu kisha, wanafunzi wake wanakumbuka maneno hayo wakati anafufuliwa.