Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 13

Mambo Tunaweza Kujifunza Kupitia Namna Yesu Alipambana na Majaribu

Mambo Tunaweza Kujifunza Kupitia Namna Yesu Alipambana na Majaribu

MATAYO 4:1-11 MARKO 1:12, 13 LUKA 4:1-13

  • SHETANI ANAMUJARIBU YESU

Kisha tu Yohana kumubatiza Yesu, roho ya Mungu inamuongoza Yesu katika jangwa la Yudea. Iko na mambo mengi ya kufikiria. Wakati Yesu alibatizwa, ‘mbingu zilifunguliwa.’ (Matayo 3:16) Kwa hiyo, anaweza kukumbuka mambo yenye alijifunza na kufanya huko mbinguni. Kwa kweli, kuko mambo mengi yenye anapaswa kufikiria sana!

Yesu anafanya siku 40 na usiku 40 katika jangwa. Wakati huo, hakule kitu. Kisha, wakati Yesu anasikia njaa sana, Shetani Ibilisi anamukaribia ili kumujaribu, kwa kumuambia hivi: “Kama wewe uko mwana wa Mungu, ambia majiwe haya yakuwe mikate.” (Matayo 4:3) Kwa sababu anajua kama ni mubaya kutumia uwezo wake wa kufanya miujiza ili kutimiza tamaa zake mwenyewe, Yesu anapinga jaribu hilo.

Ibilisi haache kumujaribu. Anajaribu kutumia njia ingine. Anamuambia Yesu ajitupe kutoka kwenye munara wa hekalu. Lakini Yesu hakubali kufanya tendo hilo la kushangaza sana. Kwa kutumia maneno ya Maandiko, Yesu anaonyesha kwamba ni mubaya kumujaribu Mungu katika njia hiyo.

Kisha, kwenye jaribu la tatu, Ibilisi anamuonyesha Yesu kwa njia fulani “falme zote za ulimwengu na utukufu wa falme hizo” na kumuambia hivi: “Nitakupatia vitu hivi vyote ukianguka chini na kunifanyia tendo la ibada.” Tena Yesu anakataa kabisa. Anasema hivi: “Toka mbele yangu, Shetani!” (Matayo 4:8-10) Hajiache ajaribiwe kufanya mambo ya mubaya, kwa sababu anajua kama ni Yehova tu ndiye anastahili kutolewa utumishi mutakatifu. Ndiyo, anachagua kubakia muaminifu kwa Mungu.

Majaribu hayo na namna Yesu alipambana nayo vinaweza kutufundisha mambo fulani. Majaribu hayo yalikuwa ya kweli, na hilo linaonyesha kama Ibilisi haiko tu uovu kama vile watu fulani wanasema. Ni mutu wa kweli, mwenye haonekane. Habari hii inaonyesha pia kwamba serikali za ulimwengu huu ni za Ibilisi; ziko chini ya utawala wake. Je, jaribu lake la kumupatia Kristo serikali hizo lingekuwa la kweli ikiwa hazikuwa chini ya utawala wake?

Tena, Ibilisi alisema kama atafikia kumupatia Yesu falme zote za ulimwengu, ikiwa tu angemufanyia tendo moja la ibada. Ibilisi anaweza kabisa kutujaribu kwa njia kama hiyo, pengine kwa kututia mbele ya nafasi za kutuchochea kutafuta utajiri katika ulimwengu, mamlaka, ao cheo. Tutatenda kwa hekima ikiwa tunafuata mufano wa Yesu kwa kubakia waaminifu kwa Mungu hata kama tunakutana na jaribu gani! Lakini usisahau kama Ibilisi alimuacha Yesu tu “mupaka wakati mwingine wenye kufaa.” (Luka 4:13) Sisi pia, Shetani anaweza kututendea hivyo; kwa hiyo tunapaswa kuendelea kuwa waangalifu.