Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Njia, Kweli, na Uzima

Njia, Kweli, na Uzima

Bila shaka unapendaka kusikia habari njema. Na kuko kabisa habari njema kwa ajili yako na wale wenye unapenda.

Habari njema hiyo inapatikana katika Biblia, kitabu chenye Muumbaji wa ulimwengu wote, Yehova Mungu, alifanya kiandikwe kumepita miaka mingi. Katika kichapo hiki, tutakazia uangalifu juu ya vitabu ine vya Biblia vyenye kuwa na habari njema kwa ajili ya sisi wote. Vitabu hivyo vinaitwa kwa majina ya wanaume wenye Mungu alitumia ili kuviandika, ni kusema, Matayo, Marko, Luka, na Yohana.

Watu wengi wanaita habari hizo ine kuwa Injili ine. Vitabu vyote ine vinazungumuzia injili, ao habari njema kuhusu Yesu; kwamba yeye ni njia yenye Mungu anatumia ili kuokoa wanadamu na kwamba, kwa kuwa yeye ni Mufalme wa Ufalme wa Mungu wenye kuwa mbinguni, Yesu ataleta baraka za milele kwa wote wenye kuonyesha imani katika yeye.​—Marko 10:17, 30; 13:13.

SABABU GANI KUKO VITABU INE VYA INJILI?

Pengine umekwisha kujiuliza sababu gani Mungu aliongoza kupitia roho yake takatifu wanaume ili waandike habari ine kuhusu maisha ya Yesu na mafundisho yake.

Kuko faida ya kuwa na habari hizo ine tofauti kuhusu mambo yenye Yesu alisema na kufanya. Kwa mufano, waza wanaume ine wanasimama karibu na mwalimu mwenye kujulikana sana. Mwanaume mwenye kusimama mbele ya mwalimu ni mukusanya-kodi. Ule mwenye kuwa upande wa kuume ni munganga. Mwanaume mwenye iko anasikiliza upande wa kushoto ni muvuvi wa samaki, na ni rafiki wa sana wa mwalimu. Na mwanaume wa ine, mwenye kuwa nyuma ya mwalimu, ni mutazamaji ambaye ni mudogo zaidi kuliko wengine. Wote ine ni wanaume waaminifu, na kila mumoja wao iko na mambo yenye anapendezwa nayo ao yenye anakazia. Ikiwa kila mutu anaandika habari kuhusu mambo yenye mwalimu anasema na kufundisha, inaonekana kila habari itazungumuzia mambo ao matukio tofauti. Ikiwa tunachunguza habari zote ine, kwa kuweka katika akili maoni ao makusudi ya kila muandikaji, tutapata picha kamili ya mambo yenye mwalimu alisema na kufanya. Hilo linaonyesha namna gani tunaweza kupata faida ya kuwa na habari ine tofauti kuhusu maisha ya Mwalimu Mukubwa, ni kusema, Yesu.

Tuendelee na mufano: mukusanya-kodi anapenda habari ikuwe yenye kupendezwa kwa Wayahudi, kwa hiyo anakusanya mafundisho ao matukio fulani katika njia yenye itasaidia kwanza watu hao. Munganga yeye anakazia kuponyeshwa kwa wagonjwa ao vilema, kwa hiyo anaacha mambo fulani yenye mukusanya-kodi aliandika ao anayaeleza kwa kufuata mupangilio mwengine. Rafiki wa sana wa mwalimu anakazia namna mwalimu huyo anajisikia na sifa zake. Ule mwandikaji mudogo yeye anatoa habari yake kwa kifupi zaidi. Hata hivyo, habari ya kila mwanaume ni ya kweli. Hilo linaonyesha muzuri kwamba kuwa na habari zote ine kuhusu maisha ya Yesu kunaongeza ujuzi wetu juu ya kazi zake, mafundisho, na sifa zake.

Watu wanaweza kusema ‘Injili ya Matayo’ ao ‘Injili ya Yohana.’ Hilo ni kweli kwa sababu kila Injili iko na “habari njema juu ya Yesu Kristo.” (Marko 1:1) Lakini, kwa ujumla, kuko injili moja tu, ao habari njema, kuhusu Yesu, yenye tunaweza kupata katika maandishi ine.

Wanafunzi wengi wa Neno la Mungu wamelinganisha na kupatanisha matukio na mambo mbalimbali yenye kupatikana katika Injili ya Matayo, Marko, Luka, na Yohana. Katika mwaka wa karibu 170 kisha kuzaliwa kwa Yesu, mwandikaji Musiria mwenye kuitwa Tatian alijikaza kufanya hivyo. Alikubali kuwa habari zenye kuwa katika vitabu hivyo ine ni za kweli na kuwa ziliongozwa na roho takatifu ya Mungu; na alikusanya habari hizo ine za maisha na utumishi wa Yesu katika habari moja yenye aliita Diatessaron.

Kitabu Yesu​—Ni Njia, Kweli, na Uzima kinafanya pia hivyo, lakini kinatoa habari za kweli zaidi na kamili. Hilo linawezekana kwa sababu sasa tunaelewa muzuri zaidi utimizo wa unabii mbalimbali wenye Yesu alitoa na mifano yake. Uelewaji huo unatusaidia kuelewa wazi mambo yenye alisema na kufanya, na pia mupangilio wa matukio mbalimbali. Ushuhuda wa vitu vya zamani vyenye vilivumbuliwa umeleta pia mwangaza juu ya mambo fulani na juu ya maoni ya waandikaji. Ni kweli kwamba hakuna mutu mwenye anaweza kueleza kwa uhakika wote namna mambo yalifuatana. Lakini kitabu Yesu​—Ni Njia, Kweli, na Uzima kinatoa habari kwa usawaziko na kwa njia yenye kupatana na akili.

NJIA, KWELI, NA UZIMA

Wakati uko unasoma na kufurahia kitabu hiki, ujikaze kuchunga katika akili ujumbe wa musingi kwa ajili yako na kwa ajili ya watu wenye unapenda. Kumbuka kama Yesu Kristo mwenyewe aliambia mutume Tomasi hivi: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima. Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.”​—Yohana 14:6.

Kitabu Yesu​—Ni Njia, Kweli, na Uzima kitakusaidia kuelewa namna gani Yesu ndiye kabisa “njia.” Ni yeye tu ndiye njia yenye inatuwezesha kumukaribia Yehova Mungu katika sala. Zaidi ya hilo, Yesu ni njia yenye inatusaidia tujipatanishe na Mungu. (Yohana 16:23; Waroma 5:8) Kwa hiyo, ni Yesu tu ndiye njia ya kutusaidia kuwa na urafiki wa muzuri pamoja na Mungu.

Yesu ni “kweli.” Alisema kweli na aliishi kulingana na kweli hiyo; ilikuwa kama vile Yesu ndiye alileta kweli. Alitimiza unabii mwingi, unabii wenye umekuwa “‘ndiyo’ kupitia yeye.” (2 Wakorinto 1:20; Yohana 1:14) Unabii kama huo unatusaidia kuona daraka lake kubwa katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu.​—Ufunuo 19:10.

Na Yesu Kristo ni “uzima.” Kupitia zabihu ya ukombozi, kwa kutoa uzima wake mukamilifu na damu yake, alifanya iwezekane kupata “uzima wa kweli,” ni kusema, “uzima wa milele.” (1 Timoteo 6:12, 19; Waefeso 1:7; 1 Yohana 1:7) Atajionyesha pia kuwa “uzima” kwa ajili ya mamilioni ya watu wenye wamekufa lakini wenye watafufuliwa na tumaini la kuishi milele katika Paradiso.​—Yohana 5:28, 29.

Sisi wote tunapaswa kuelewa daraka la Yesu katika kutimizwa kwa kusudi la Mungu na kuona daraka hilo kuwa la maana. Furahia basi kujifunza mengi zaidi kuhusu Yesu, mwenye ni “njia na kweli na uzima.”