Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ili Kufuata Mufano wa Yesu, Ukuwe . . .

Ili Kufuata Mufano wa Yesu, Ukuwe . . .

MWENYE HURUMA

Kwa kuwa Yesu alikuwa mutu mukamilifu, hakupata mateso na mahangaiko mengi kama wanadamu wengine. Hata hivyo, alikuwa na huruma nyingi kwa ajili ya watu. Alikuwa tayari kujitoa ili kusaidia, ni kusema, alifanya mambo mengi zaidi kuliko yale yenye watu walitazamia. Ndiyo, huruma yenye alikuwa nayo ilimuchochea kusaidia wengine. Fikiria mifano yenye kuzungumuziwa kwenye Sura 32, 37, 57, 99.

MUTU MWENYE WENGINE WANAWEZA KUKARIBIA

Watu wa miaka yote, ni kusema, vijana na wale wenye kukomaa, walimukaribia Yesu kwa sababu hakuonekana kuwa mutu mwenye kuwa na mambo mengi ya kufanya ao mutu wa maana sana. Wakati waliona kuwa Yesu ni mwenye kupendezwa nao, watu walijisikia muzuri wakati iko pamoja nao. Ili kujua jambo hilo, ona Sura ya 25, 27, 95.

MWENYE KUSALI

Kwa ukawaida, Yesu alisali Baba yake kwa bidii. Alifanya hivyo pekee yake na wakati alikuwa pamoja na waabudu wa kweli. Alisali katika hali mbalimbali, haiko tu wakati wa chakula. Alisali ili kumushukuru Baba yake, kumusifu, na kutafuta muongozo wake mbele ya kukamata maamuzi mazito. Chunguza mifano yenye kuwa kwenye Sura ya 24, 34, 91, 122, 123.

MWENYE KUTANGULIZA FAIDA ZA WENGINE

Wakati fulani alikuwa na lazima ya kupumuzika na kujifurahisha kidogo, hata hivyo alitia mahitaji ya wengine pa nafasi ya kwanza kuliko yake mwenyewe. Hakuwa anajipendelea. Katika jambo hilo pia, alituachia mufano wenye tunaweza kufuata kwa ukaribu. Ujifunze namna mufano huo unaonyeshwa kwenye Sura ya 19, 41, 52.

MWENYE KUSAMEHE

Yesu alifanya zaidi ya kufundisha watu kuwa ni jambo la lazima wakuwe wenye kusamehe; alionyesha kuwa yeye ni mwenye kusamehe katika namna alitendea wanafunzi wake na watu wengine. Fikiri sana juu ya mifano yenye kuzungumuziwa kwenye Sura ya 26, 40, 64, 85, 131.

MWENYE BIDII

Ilitabiriwa kwamba Wayahudi wengi watakataa kumukubali Masiya na kwamba maadui wake watamuua. Kwa hiyo, Yesu angefanya tu mambo madogo sana. Lakini, aliendeleza kwa bidii ibada ya kweli. Aliacha mufano wa bidii kwa wanafunzi wake wote wenye wanapambana na upinzani ao wanakutana na watu wenye hawapendezwe. Ona sura ya 16, 72, 103.

MUNYENYEKEVU

Katika njia nyingi, Yesu alikuwa mukubwa zaidi kuliko wanadamu wenye hawakamilike; kama vile katika ujuzi na hekima. Bila shaka, kuwa mukamilifu kulimupatia uwezo wa kimwili na akili kuliko watu wote wenye walikuwa karibu naye. Lakini, alitumikia wengine kwa unyenyekevu. Utajifunza somo mbalimbali juu ya hilo kwenye Sura ya 10, 62, 66, 94, 116.

MUVUMILIVU

Kila mara Yesu alivumilia mitume wake na watu wengine wakati walishindwa kufuata mufano wake ao wakati walishindwa kutumikisha mambo yenye alisema. Kwa uvumilivu, alirudilia mafundisho yenye walikuwa nayo lazima ili wamukaribie Yehova. Fikiri juu ya mifano kuhusu uvumilivu wa Yesu kwenye Sura ya 74, 98, 118, 135.