Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA 3

Yesu Anafanya Utumishi Mukubwa Katika Galilaya

‘Yesu Anaanza Kuhubiri: “Ufalme wa Mbinguni Umekaribia.”’​—Matayo 4:17

Yesu Anafanya Utumishi Mukubwa Katika Galilaya

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 20

Muujiza wa Pili Katika Kana

Yesu anaponyesha mutoto kwa mbali, kwenye kilometre 26.

SURA YA 21

Kwenye Sinagogi ya Nazareti

Yesu alisema jambo gani lenye lilifanya watu wa muji wake watafute kumuua?

SURA YA 22

Wanafunzi Ine Watakuwa Wavuvi wa Watu

Anawaomba waache kufanya aina fulani ya kazi ya kuvua na waanze kufanya aina ingine.

SURA YA 23

Yesu Anafanya Miujiza Katika Kapernaumu

Wakati Yesu iko anafukuza pepo wachafu, anakataza pepo hao wachafu kuambia watu kama yeye ni Mwana wa Mungu. Sababu gani?

SURA YA 24

Utumishi Wake Unapanuka Katika Galilaya

Watu wanakuja kwa Yesu ili awaponyeshe, lakini Yesu anafasiria kuwa utumishi wake uko na kusudi kubwa zaidi.

SURA YA 25

Anaponyesha Mutu Mwenye Ukoma kwa Huruma

Kwa kutumia maneno mepesi lakini yenye nguvu, Yesu anaonyesha kuwa anahangaikia kabisa watu wenye anaponyesha.

SURA YA 26

“Zambi Zako Zimesamehewa”

Yesu anaonyesha kuwa kuko uhusiano gani kati ya zambi na magonjwa?

SURA YA 27

Matayo Anaalikwa

Sababu gani Yesu anakula chakula na watu wenye kujulikana kuwa watenda-zambi?

SURA YA 28

Sababu Gani Wanafunzi wa Yesu Hawafunge?

Yesu anatumia mufano juu ya chupa ya ngozi ya kuwekea divai ili kutoa jibu.

SURA YA 29

Mutu Anaweza Kufanya Matendo ya Muzuri Siku ya Sabato?

Juu ya nini Wayahudi wanamutesa Yesu kwa sababu anaponyesha mwanaume mwenye alikuwa mugonjwa kwa miaka 38?

SURA YA 30

Uhusiano wa Yesu Pamoja na Baba Yake

Wayahudi wanafikiri kuwa Yesu anajifanya sawasawa na Mungu, lakini Yesu anaonyesha wazi kuwa Mungu ni mukubwa kuliko yeye.

SURA YA 31

Wanakata Masuke ya Nafaka Siku ya Sabato

Sababu gani Yesu anajiita “Bwana wa Sabato”?

SURA YA 32

Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?

Kwa kawaida Wasadukayo na Wafarisayo hawasikilizane; sasa wanajiunga kwa ajili ya jambo moja.

SURA YA 33

Anatimiza Unabii wa Isaya

Sababu gani Yesu anakataza wale wote wenye anaponyesha wasiambie wengine yeye ni nani ao kusema mambo yenye amefanya?

SURA YA 34

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Mbili

Kuko tofauti gani kati ya mutume na mwanafunzi?

SURA YA 35

Mahubiri ya Mulimani Yenye Kujulikana Sana

Pata mafasirio ya mambo makubwa ya mahubiri ya Yesu.

SURA YA 36

Mukubwa Fulani wa Jeshi Anaonyesha Imani Kubwa

Mukubwa huyo wa jeshi anafanya jambo gani lenye linamushangaza Yesu?

SURA YA 37

Yesu Anafufua Mutoto wa Mujane

Wale wenye waliona muujiza huo walielewa kabisa maana.

SURA YA 38

Yohana Anapenda Kupata Habari Juu ya Yesu

Sababu gani Yohana Mubatizaji anauliza ikiwa Yesu ndiye Masiya? Je, Yohana anakosa imani?

SURA YA 39

Ole kwa Kizazi Chenye Kukataa Kusikiliza

Yesu anasema kuwa katika Siku ya Hukumu, itakuwa mwepesi zaidi kwa Sodoma kuliko kwa Kapernaumu, muji wenye ulikuwa makao yake makubwa.

SURA YA 40

Anafundisha Watu Kusamehe

Kwa kuambia mwanamuke mwenye alikuwa mwasherati kama zambi zake zimesamehewa, je, Yesu alikuwa anasema kama haiko mubaya kuvunja sheria za Mungu?

SURA YA 41

Anafanya Miujiza kwa Nguvu za Nani?

Ndugu za Yesu wanawaza kuwa amepoteza akili.

SURA YA 42

Yesu Anakemea Wafarisayo

“Alama ya nabii Yona” ni nini?

SURA YA 43

Mifano Mbalimbali Kuhusu Ufalme

Yesu anatoa mifano munane ili kufasiria mambo mbalimbali juu ya Ufalme wa mbinguni.

SURA YA 44

Yesu Ananyamazisha Upepo Mukali Kwenye Bahari

Wakati Yesu alituliza upepo na mawimbi, alifundisha jambo la maana sana juu ya namna maisha yatakuwa wakati wa utawala wake katika Ufalme wa mbinguni.

SURA YA 45

Iko na Mamlaka Juu ya Pepo Wengi Wachafu

Je, mutu anaweza kuwa na pepo wengi wachafu?

SURA YA 46

Anaponyeshwa kwa Kugusa Nguo ya Yesu

Yesu anaonyesha kuwa iko na uwezo na huruma katika hali hii yenye kugusa moyo.

SURA YA 47

Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

Watu wanamucheka Yesu wakati anasema kuwa mutoto mwanamuke mwenye amekufa ni mwenye kulala tu usingizi. Ni jambo gani lenye Yesu anajua ambalo watu hao hawajue?

SURA YA 48

Anafanya Miujiza, Lakini Anakataliwa Hata Katika Nazareti

Watu wa Nazareti wanamukataa Yesu, haiko kwa sababu ya mafundisho ao miujiza yake, lakini wanamukataa juu sababu ingine.

SURA YA 49

Anahubiri Katika Galilaya na Anazoeza Mitume

Maneno ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia’ yanamaanisha kabisa nini?

SURA YA 50

Wanatayarishwa Kuhubiri Hata Katika Mateso

Sababu gani anawaambia wakimbie wakati wanateswa ikiwa hapaswe kuogopa kifo?

SURA YA 51

Mutu Anauawa Wakati wa Karamu ya Sikukuu ya Kuzaliwa

Namna Salome anacheza dansi inafurahisha Herode sana hivi kwamba anamuahidi kumupatia kitu chochote chenye ataomba. Ni kitu gani chenye anaomba chenye kinaleta huzuni sana?

SURA YA 52

Anatumia Mikate Tano na Samaki Wawili ili Kukulisha Maelfu ya Watu

Muujiza wa Yesu ni wa maana sana hivi kwamba vitabu vyote ine vya Injili vinauzungumuzia.

SURA YA 53

Mutawala Mwenye Kuwa na Mamlaka Juu ya Nguvu za Asili

Mitume wanajifunza mambo gani wakati Yesu anatembea juu ya maji na kutuliza upepo?

SURA YA 54

Yesu Ni “Mukate wa Uzima”

Sababu gani Yesu anakemea watu hata kama wamejikaza sana ili kuja kwenye iko?

SURA YA 55

Watu Wengi Wanakwazika kwa Sababu ya Maneno ya Yesu

Yesu anafundisha jambo fulani lenye linakwaza sana watu hivi kwamba wanafunzi wake wengi wanaacha kumufuata.

SURA YA 56

Mutu Anachafuliwa na Nini?

Ni kile chenye kinaingia katika kinywa chake, ao kile chenye kinatoka?

SURA YA 57

Yesu Anaponyesha Mutoto Mwanamuke na Mwanaume Mwenye Kuwa Kiziwi

Sababu gani mwanamuke hakwazike wakati Yesu analinganisha watu wa taifa lake na imbwa wadogo?

SURA YA 58

Anazidisha Mikate na Kuonya Juu ya Chachu

Mwishowe, wanafunzi wa Yesu wanaelewa aina ya chachu yenye iko anazungumuzia.

SURA YA 59

Mwana wa Binadamu Ni Nani?

Funguo za Ufalme ni gani? Ni nani anazitumia, na namna gani?

SURA YA 60

Kugeuzwa Sura: Kristo Anaonekana Katika Utukufu

Kugeuzwa sura kulifanyika namna gani? Na tukio hilo lilimaanisha nini?

SURA YA 61

Yesu Anaponyesha Kijana Mwanaume Mwenye Kuwa na Pepo Muchafu

Yesu anasema kama ule kijana mwanaume hakuponyeshwa kwa sababu ya kukosa imani, lakini ni nani ndiye alikosa imani? Ni kijana mwanaume, baba yake, ao wanafunzi wa Yesu?

SURA YA 62

Anafundisha Somo la Maana Kuhusu Unyenyekevu

Wanaume wenye kukomaa wanajifunza jambo fulani la maana kupitia mutoto mudogo.

SURA YA 63

Yesu Anatoa Mashauri Kuhusu Kukwaza Wengine na Kuhusu Zambi

Anaonyesha hatua tatu za kufuata ili kumaliza magumu kati ya ndugu.

SURA YA 64

Ni Jambo la Lazima Kusamehe

Kwa kutumia mufano wa mutumwa mwenye hana huruma, Yesu anaonyesha kama Mungu anaona kuwa ni jambo la maana sana kuwa tayari kusamehe wengine.

SURA YA 65

Anafundisha Katika Safari Yake ya Kuenda Yerusalemu

Katika mazungumuzo hayo tatu ya mufupi-mufupi, Yesu anaonyesha mambo yenye yanaweza kuzuia mutu kuwa mwanafunzi wake.