Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 37

Yesu Anafufua Mutoto wa Mujane

Yesu Anafufua Mutoto wa Mujane

LUKA 7:11-17

  • UFUFUO KATIKA NAINI

Kisha tu kuponyesha mutumishi wa mukubwa fulani wa jeshi, Yesu anatoka Kapernaumu na kuenda Naini, muji wenye kuwa kwenye kilometre 32 upande wa kusini-mangaribi. Haiko yeye mwenyewe. Wanafunzi wake na watu wengine wengi sana wanasafiri pamoja naye. Inawezekana ni wakati wa mangaribi ndio wanafika karibu na maeneo ya pembeni ya muji wa Naini. Mahali hapo, wanakutana na hesabu kubwa ya Wayahudi wenye wako wanaenda inje ya muji ili kuzika kijana mumoja mwanaume mwenye amekufa.

Mutu mwenye kuwa na huzuni nyingi zaidi kati ya watu hao ni mama ya kijana huyo mwanaume. Mama huyo ni mujane, na sasa mutoto wake mumoja tu amekufa. Wakati bwana yake alikufa, alibakia tu na mutoto wake mupendwa. Waza namna mama huyo alipaswa kumupenda sana mutoto wake, kwa sababu alitumaini kuwa ni mutoto huyo ndiye atamusaidia na kumutegemeza. Sasa yeye pia amekufa. Atabakia na nani, na ni nani atamutegemeza?

Wakati Yesu anaona mwanamuke huyo, anaumia sana kwa sababu ya huzuni nyingi ya mwanamuke huyo na anahuzunika juu ya hali yake. Kwa huruma na kwa kutumia maneno yenye kutia nguvu, Yesu anamuambia hivi: “Acha kulia.” Hata hivyo, Yesu anafanya zaidi ya hilo. Anakaribia na kugusa kitanda cha kubebea maiti. (Luka 7:13, 14) Matendo yake yanafanya watu wa muji wenye walikuwa wanalia wasimame mara moja. Wengi kati yao wanapaswa kuwa wanajiuliza, ‘Anataka kusema nini, na atafanya nini?’

Na tuseme nini juu wale wako wanasafiri na Yesu wenye wamemuona anafanya miujiza, akiponyesha magonjwa mengi? Inaonekana kuwa hawajaonaka Yesu anafufua mutu yeyote mwenye alikufa. Hata kama ufufuo mbalimbali ulifanyika zamani sana, Yesu anaweza kufufua mutu mwenye amekufa? (1 Wafalme 17:17-23; 2 Wafalme 4:32-37) Yesu anasema hivi: “Kijana, ninakuambia, amuka!” (Luka 7:14) Na anainuka kabisa. Mwanaume huyo anakaa na kuanza kusema! Yesu anamupatia mama yake mwenye anashangazwa, lakini anafurahi sana. Mama huyo haiko tena pekee yake.

Wakati watu wanaona kuwa kijana huyo mwanaume ni muzima kabisa, wanamusifu Yehova, Mupaji-Uzima, kwa kusema hivi: “Nabii mukubwa ameinuliwa katikati yetu.” Wengine wanaelewa maana ya muujiza huo wa Yesu na kusema hivi: “Mungu amekumbuka watu wake.” (Luka 7:16) Habari kuhusu jambo hilo lenye kushangaza inaenda haraka katika maeneo ya pembeni na inawezekana pia katika Nazareti muji kwenye Yesu alikomalia, kwenye kilometre kumi hivi. Habari inafika hata mupaka maeneo ya kusini, katika Yudea.

Yohana Mubatizaji angali katika gereza, na anapendezwa sana na mambo yenye Yesu iko anafanya. Wanafunzi wa Yohana wanamuelezea juu ya miujiza hiyo. Anatenda namna gani?