Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 65

Anafundisha Katika Safari Yake ya Kuenda Yerusalemu

Anafundisha Katika Safari Yake ya Kuenda Yerusalemu

MATAYO 8:19-22 LUKA 9:51-62 YOHANA 7:2-10

  • NDUGU ZA YESU WANAMUONA NAMNA GANI?

  • KAZI YA UFALME NI YA MAANA KWA KIASI GANI?

Kwa wakati fulani, Yesu amefanya utumishi wake zaidi sana katika Galilaya, kwenye amepata matokeo ya muzuri zaidi kuliko Yudea. Zaidi ya hilo, wakati alikuwa katika Yerusalemu na kuponyesha mwanaume mumoja siku ya Sabato, “Wayahudi walianza kutafuta hata zaidi kumuua.”—Yohana 5:18; 7:1.

Sasa, tuko katika Mwezi wa 9 ao Mwezi wa 10 wa mwaka wa 32 wakati wetu, na Sikukuu ya Vibanda inakaribia. Sikukuu hiyo inafanywa kwa siku saba, na siku ya munane kunakuwa mukusanyiko mutakatifu. Sikukuu hiyo inaonyesha mwisho wa mwaka wa kufanya kazi ya kulima na kupanda na huo ni wakati wa furaha sana na wa kutoa shukrani.

Ndugu-nusu za Yesu, ni kusema, Yakobo, Simoni, Yosefu, na Yuda, wanamuambia Yesu hivi: “Toka hapa uende Yudea.” Yerusalemu ni makao makubwa ya kidini ya inchi hiyo. Wakati wa sikukuu hizo tatu za mwaka, watu wengi sana wanakutana katika muji huo. Ndugu za Yesu wanamuambia hivi: “Hakuna mutu mwenye anafanya jambo lolote kwa uficho wakati anatafuta kujulikana mbele ya watu wote. Kama unafanya mambo haya, ujionyeshe mwenyewe kwa ulimwengu.”—Yohana 7:3, 4.

Kwa kweli, ndugu hawa ine “hawakukuwa wanamuamini” Yesu kuwa Masiya. Hata hivyo, wanapenda watu wenye wanakuja kwenye sikukuu hiyo wamuone Yesu anafanya miujiza fulani. Yesu, anajua hatari ya kufanya hivyo, kwa hiyo anawaambia hivi: “Ulimwengu hauna sababu ya kuwachukia ninyi, lakini unanichukia mimi, kwa sababu ninatoa ushahidi juu yake kwamba kazi zake ni za uovu. Ninyi muende kwenye sikukuu; mimi sitapanda sasa kuenda kwenye sikukuu hiyo, kwa sababu wakati wangu haujafika kabisa.”—Yohana 7:5-8.

Siku fulani kisha ndugu za Yesu kuenda pamoja na kikundi cha watu wenye kusafiri, Yesu na wanafunzi wake wanaenda kwa siri, bila watu wengi kuwaona. Wanachukua barabara yenye kuenda mara moja Yerusalemu kupitia Samaria, kuliko barabara yenye watu wanazoea kutumia yenye kuwa karibu na Muto Yordani. Yesu na wanafunzi wake wako na lazima ya nafasi ya kufikia katika Samaria, kwa hiyo, anatuma wajumbe ili wafanye matayarisho. Mahali fulani, watu wanakataa kuwakaribisha ao kuwaonyesha ukaribishaji-wageni wenye watu wanazoea kuonyeshwa, kwa sababu Yesu iko anaenda katika Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu ya Wayahudi. Yakobo na Yohana wanauliza hivi kwa kisirani: “Bwana, unataka tuite moto ushuke kutoka mbinguni na kuwaharibu?” (Luka 9:54) Yesu anawakemea kwa sababu ya kusema hivyo, na wanaendelea na safari yao.

Wakati wako katika barabara, mwandishi mumoja anaambia Yesu hivi: “Mwalimu, nitakufuata kila mahali utaenda.” Yesu anamujibu: “Mbweha wako na mashimo na ndege wa mbinguni wako na machicha, lakini Mwana wa binadamu hana mahali pa kulalisha kichwa chake.” (Matayo 8:19, 20) Yesu iko anaonyesha kuwa mwandishi huyo atapatwa na magumu ikiwa anakuwa mwanafunzi wake. Na inaonekana kuwa mwandishi huyo hawezi kukubali namna hiyo ya maisha kwa sababu ya kiburi. Kwa hiyo, kila mumoja wetu anaweza kujiuliza, ‘Niko tayari kabisa kumufuata Yesu?’

Yesu anaambia mwanaume mwingine: “Kuwa mufuasi wangu.” Mwanaume huyo anajibu hivi: “Bwana, uniruhusu kwanza niende nimuzike baba yangu.” Yesu anajua hali ya mwanaume huyo, kwa hiyo, anamuambia: “Acha wafu wazike wafu wao, lakini wewe uende na utangaze Ufalme wa Mungu kila mahali.” (Luka 9:59, 60) Bila shaka, baba ya mwanaume huyo hajakufa. Ikiwa alikuwa amekufa, pengine mutoto wake hangekuwa anazungumuza na Yesu wakati huo. Mutoto huyo haiko tayari kutanguliza Ufalme wa Mungu katika maisha yake.

Wakati wako katika barabara ya kuenda Yerusalemu, mwanaume mwingine anaambia Yesu hivi: “Nitakufuata Bwana, lakini uniruhusu kwanza niage watu wa nyumba yangu.” Yesu anamujibu hivi: “Hakuna mutu mwenye anaweka mukono wake kwenye jembe la kukokotwa na ngombe na kuangalia mambo yenye kuwa nyuma mwenye anafaa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu.”—Luka 9:61, 62.

Wale wenye wanapenda kuwa wanafunzi wa kweli wa Yesu wanapaswa kukaza macho yao juu ya kazi ya Ufalme. Ikiwa mulimaji mwenye kulima na jembe la kukokotwa hakaze macho yake mbele, mustari wenye iko anafanya hautanyooka. Ikiwa anatia jembe lake chini ili kuangalia mambo yenye kuwa nyuma yake, kazi haitaendelea. Vilevile, mutu yeyote mwenye anaangalia nyuma katika mupangilio huu wa mambo anaweza kabisa kujikwaa na kushindwa kuendelea katika barabara yenye kuongoza kwenye uzima wa milele.