Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 42

Yesu Anakemea Wafarisayo

Yesu Anakemea Wafarisayo

MATAYO 12:33-50 MARKO 3:31-35 LUKA 8:19-21

  • YESU ANAZUNGUMUZIA ‘ALAMA YA YONA’

  • IKO NA UHUSIANO WA KARIBU ZAIDI NA WANAFUNZI WAKE KULIKO WATU WA FAMILIA YAKE

Kwa kukataa kama Yesu anafukuza pepo wachafu kwa nguvu za Mungu, waandishi na Wafarisayo wako katika hatari ya kukufuru roho takatifu. Sasa, wako upande wa nani? Wa Mungu ao wa Shetani? Yesu anasema hivi: “Kama ninyi ni muti wa muzuri mutazaa matunda ya mazuri, lakini kama ninyi ni muti wenye kuoza mutazaa matunda yenye kuoza, kwa maana muti unajulikana kwa matunda yake.”—Matayo 12:33.

Ni jambo lenye halipatane na akili kusema kuwa ikiwa Yesu anafukuza pepo wachafu ni kwa sababu iko anamutumikia Shetani. Kama vile Yesu alionyesha waziwazi kwenye Mahubiri ya Mulimani, ikiwa matunda ni ya muzuri, muti pia uko muzuri, hauoze. Kwa hiyo, matunda ya Wafarisayo, ni kusema, mashitaka yao yenye haiko ya kweli ambayo wanaleta juu ya Yesu yanaonyesha nini? Yanaonyesha kwamba ni wenye kuoza. Yesu anawaambia hivi: “Ninyi wazao wa nyoka-vipiri, namna gani munaweza kusema mambo ya muzuri, wakati ninyi ni waovu? Kwa maana kinywa kinasema kutokana na mambo yenye kujaa katika moyo.”—Matayo 7:16, 17; 12:34.

Ndiyo, maneno yetu yanaonyesha hali ya moyo wetu, na yanaweza kufanya tuhukumiwe. Kwa hiyo Yesu anasema hivi: “Ninawaambia ninyi kwamba katika Siku ya Hukumu watu watatoa hesabu juu ya kila neno lenye halifae lenye wanasema; kwa maana kwa maneno yako utatangazwa kuwa mutu mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa, na kwa maneno yako utahukumiwa.”—Matayo 12:36, 37.

Hata kama waandishi na Wafarisayo wako wanaona miujiza yenye Yesu iko anafanya, wanamuomba zaidi. Wanamuambia hivi: “Mwalimu, tunataka kuona alama kutoka kwako.” Ikuwe wamejionea namna anafanya miujiza ao hapana, kuko ushuhuda wa watu wengi wenye wanajionea kwa macho yao wenyewe mambo yenye Yesu iko anafanya. Kwa hiyo, Yesu iko na sababu ya kuambia viongozi hao wa dini hivi: “Kizazi kiovu na chenye uzinifu kinaendelea kutafuta alama, lakini hakitapewa alama yoyote isipokuwa alama ya nabii Yona.”—Matayo 12:38, 39.

Yesu hawaachie nafasi ya kujiuliza-uliza ikiwa maneno yake yanamaanisha nini. Anawaambia hivi: “Kama vile Yona alikuwa ndani ya tumbo la ule samaki mukubwa siku tatu (3) muchana na usiku, ni vile Mwana wa binadamu atakuwa katika kaburi siku tatu (3) muchana na usiku.” Yona alimezwa na aina fulani ya samaki kubwa lakini alifikia kutapikwa. Ilikuwa kama vile anafufuliwa. Kwa hiyo, Yesu anatabiri kama atakufa na kisha siku tatu atafufuliwa. Wakati jambo hilo lilifikia kutokea, viongozi wa dini walikataa ‘alama ya Yona,’ ni kusema, walikataa kutubu na kubadilika. (Matayo 27:63-66; 28:12-15) Tofauti nao, “watu wa Ninawi” walitubu kisha Yona kuwahubiria. Kwa hiyo, watahukumu kizazi hiki. Yesu anasema pia kama kupitia mufano wake, malkia wa Sheba atawahukumu. Alitamani kusikia hekima ya Sulemani na aliifurahia sana. Sasa, Yesu anasema, “hapa kuko mutu mukubwa kuliko Sulemani.”—Matayo 12:40-42.

Yesu anafananisha hali ya kizazi hiki kiovu na mwanaume mwenye roho muchafu ametoka ndani yake. (Matayo 12:45) Kwa sababu mutu huyo hakujaza mambo ya muzuri nafasi kwenye kulikuwa kunakosa, ule roho muovu anarudia na roho wengine saba waovu kuliko yeye na wanaanza kumutawala. Kama ule mwanaume mwenye roho muchafu alitoka ndani yake, taifa la Israeli lilikuwa limesafishwa na kufanywa upya. Lakini taifa hilo lilikataa manabii wa Mungu, na kufikia hata kumupinga ule mwenye kuwa kabisa na roho ya Mungu, ni kusema, Yesu. Hilo linaonyesha kama hali ya taifa hilo imekuwa mubaya zaidi kuliko hata zamani.

Wakati Yesu iko anazungumuza, mama yake na ndugu zake wanafika na kusimama nyuma ya watu. Watu fulani wenye kukaa karibu naye wanamuambia hivi: “Mama yako na ndugu zako wamesimama inje, wanataka kukuona.” Kisha Yesu anaonyesha kuwa iko na uhusiano wa karibu pamoja na wanafunzi wake, wenye wako kama ndugu zake, dada, na mama. Kwa hiyo, anaonyesha mukono kwenye wanafunzi wake wako na kusema: “Mama yangu na ndugu zangu ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulitenda.” (Luka 8:20, 21) Kwa hiyo, Yesu anaonyesha kuwa hata kama uhusiano wake pamoja na watu wa jamaa yake ni wa maana, uhusiano wake pamoja na wanafunzi wake ni wa maana hata zaidi. Ni jambo lenye kutia moyo sana kuwa na urafiki wa karibu kama huo pamoja na ndugu zetu, zaidi sana wakati watu wengine wanatutilia mashaka na kutusema mubaya juu ya matendo yetu ya muzuri!