Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 40

Anafundisha Watu Kusamehe

Anafundisha Watu Kusamehe

LUKA 7:36-50

  • MWANAMUKE MWENYE ZAMBI ANAMWANGA MAFUTA KWENYE MIGUU YA YESU

  • ANATUMIA MUFANO WA MUTU MWENYE KUWA NA DENI ILI KUZUNGUMUZIA MUSAMAHA

Kulingana na hali ya moyo ya kila mutu, watu wanatenda kwa njia tofauti wakati wanasikia mambo yenye Yesu anasema na kufanya. Jambo hilo linaonekana wazi kwenye nyumba fulani katika Galilaya. Mufarisayo mumoja mwenye kuitwa Simoni anamualika Yesu kwenye chakula, pengine anapenda aone muzuri mutu huyo mwenye iko anafanya miujiza. Yesu anakubali mwaliko huo; pengine anaona hilo kuwa nafasi ya kuhubiria watu wenye kupatikana hapo, kama vile tu nyakati zingine alikubali mialiko ili kula na wakusanya-kodi na watenda-zambi.

Lakini, hawamukaribishe Yesu kwa shauku kama vile wanazoea kukaribisha wageni. Katika barabara yenye vumbi ya Palestina, mutu mwenye kutembea na viatu, miguu yake inakuwa yenye joto na yenye kuchafuka. Kwa hiyo, ni desturi kwa mukaribishaji-wageni kunawisha mugeni miguu kwa kutumia maji ya baridi. Lakini Yesu hatendewe hivyo. Tena hapewe busu yenye wageni wanazoea kupewa. Tendo lingine la kuonyesha wema na ukaribishaji-wageni ni kumwanga mafuta kwenye kichwa cha mugeni. Yesu hatendewe pia hivyo. Sasa, tutasema kuwa Yesu anakaribishwa muzuri?

Wakati wa kula unafika, na wageni wako kwenye meza. Wakati wako wanakula, mwanamuke mumoja anaingia katika nyumba bila kualikwa. Mwanamuke huyo ‘anajulikana katika muji kuwa mutenda-zambi.’ (Luka 7:37) Watu wote wenye hawakamilike ni watenda-zambi, lakini mwanamuke huyu anaonekana kuwa na mwenendo muchafu, pengine ni mwasherati. Inawezekana alikuwa amesikia mafundisho ya Yesu, kutia ndani mwaliko wa Yesu kwa ‘wote wenye kubeba mizigo mizito wakuje kwake ili wapate pumuziko.’ (Matayo 11:28, 29) Pengine maneno na matendo ya Yesu, vinachochea amutafute.

Anaenda nyuma ya Yesu na anapiga magoti. Machozi yake yanaangukia kwenye miguu ya Yesu na anaipanguza na nywele zake. Anabusu polepole miguu ya Yesu na anaimwangia mafuta yenye harufu ya muzuri ambayo alileta. Simoni hafurahie jambo hilo, na anajiambia hivi: “Kwa kweli mutu huyu angekuwa kabisa nabii, angejua mwanamuke huyu mwenye anamugusa ni nani na ni wa namna gani, kwamba ni mutenda-zambi.”—Luka 7:39.

Yesu anatambua mawazo ya Simoni, na anamuambia hivi: “Simoni, niko na jambo fulani la kukuambia.” Anamujibu hivi: “Sema, Mwalimu!” Yesu anaendelea kumuambia: “Watu wawili walikuwa na deni la mukopeshaji fulani; mumoja alikuwa na deni la dinari mia tano (500), lakini mwingine la makumi tano (50). Wakati walikosa kitu cha kumulipa, akawasamehe wote wawili kwa kupenda. Kwa hiyo, ni nani kati yao mwenye atamupenda zaidi?” Pengine kwa kuonyesha kama vile hapendezwe, Simoni anamujibu hivi: “Ninafikiri ni ule mwenye alisamehewa deni kubwa zaidi.”—Luka 7:40-43.

Yesu anakubaliana na jibu lake. Kisha anaangalia ule mwanamuke na kumuambia Simoni: “Unaona mwanamuke huyu? Niliingia katika nyumba yako; haukunipatia maji ya kunawa miguu. Lakini mwanamuke huyu alilowanisha miguu yangu kwa machozi yake na kuipanguza kwa nywele zake. Haukunibusu, lakini tangu saa niliingia, mwanamuke huyu, hajaacha kubusu miguu yangu kwa upole wote. Haukumwanga mafuta kwenye kichwa changu, lakini mwanamuke huyu amemwanga mafuta yenye marashi kwenye miguu yangu.” Yesu aliona kama mwanamuke huyo alikuwa anaonyesha kuwa anatubu kutoka moyoni kwa sababu ya mwenendo wake muchafu. Kwa hiyo, anamalizia kwa kusema hivi: “Ninakuambia, zambi zake, hata kama ni nyingi, zimesamehewa, kwa sababu alipenda sana. Lakini mwenye anasamehewa kidogo, anapenda kidogo.”—Luka 7:44-47.

Yesu hafunge macho juu ya mwenendo muchafu wa mwanamuke huyo. Lakini, anaonyesha kama anasikilia huruma na kuelewa watu wenye, kisha kufanya zambi nzito wanahuzunika juu ya zambi hizo na kumuendea Yesu ili wapate kitulizo. Na mwanamuke huyo anatulizwa kabisa wakati Yesu anasema: “Zambi zako zimesamehewa. . . . Imani yako imekuokoa; uende kwa amani.”—Luka 7:48, 50.