Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 47

Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!

Yairo anaona kuwa Yesu ameponyesha mwanamuke mwenye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu. Bila shaka, Yesu anaweza kusaidia mutoto wake pia, hata kama Yairo anafikiri kuwa ‘kufikia sasa mutoto wake mwanamuke atakuwa amekufa.’ (Matayo 9:18) Inawezekana kabisa Yesu asaidie mutoto huyo?

Wakati Yesu angali anazungumuza na mwanamuke mwenye ameponyesha, wanaume fulani wanakuja kutoka nyumbani kwa Yairo na kumuambia Yairo hivi: “Binti yako amekufa!” Wanaongeza hivi: “Sababu gani uendelee kumusumbua Mwalimu?”—Marko 5:35.

Hiyo ni habari yenye kuhuzunisha sana! Mwanaume huyo, mwenye watu wanaheshimia sana, anavunjika moyo sana. Binti yake mumoja tu amekufa. Lakini, Yesu anasikia habari hiyo, na anamuangalia Yairo na kumuambia kwa maneno yenye kutia moyo: “Usiogope, ukuwe tu na imani.”—Marko 5:36.

Kisha Yesu anaenda na Yairo nyumbani kwake. Wakati wanafika, wanakuta muvurugo mwingi. Watu wenye kuwa nyumbani kwa Yairo wako wanalia, na kujipiga-piga kwa huzuni. Yesu anaingia ndani ya nyumba na kusema maneno haya yenye kushangaza: “Mutoto hakukufa lakini amelala usingizi.” (Marko 5:39) Wakati watu wanasikia hivyo, wanamucheka Yesu. Wanajua kama mutoto huyo tayari amekufa. Lakini, kwa kutumia mamlaka yenye Mungu amemupatia, Yesu ataonyesha kuwa inawezekana watu wafufuliwe kama vile tu wanaweza kuamushwa wakati wamelala usingizi muzito.

Sasa Yesu anatosha watu wote inje, lakini anaacha tu Petro, Yakobo, Yohana, na wazazi wa mutoto mwenye amekufa. Yesu anaenda na watu hao tano mahali kwenye mutoto huyo mwanamuke alikuwa amelala. Anamukamata kwenye mukono na kumuambia: “‘Talita kumi,’ maneno yenye wakati yanatafsiriwa yanamaanisha: ‘Mutoto mwanamuke, ninakuambia, “Simama!”’” (Marko 5:41) Mara moja, mutoto huyo anasimama na kuanza kutembea. Wazia namna Yairo na bibi yake wanafurahi wakati wanaona jambo hilo! Ili kuwahakikishia kuwa mutoto anaishi kabisa, Yesu anawaambia wamupatie kitu fulani cha kula.

Katika miujiza mingine yenye Yesu alifanya mbele ya hapo, aliambia watu wenye aliponyesha wasitangaze mambo yenye amefanya; anaambia wazazi hawa hivyohivyo. Hata hivyo, wazazi hao wenye furaha sana na watu wengine wanatangaza habari hiyo “katika eneo hilo lote.” (Matayo 9:26) Ni wazi kwamba, ikiwa unaona mutu mwenye unapenda anafufuliwa, utakuwa kabisa na furaha ya kuambia wengine juu ya jambo hilo, haiko vile? Huu ndio ufufuo wa pili wenye Yesu anafanya wenye umeandikwa katika vitabu vya Injili.