Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 60

Kugeuzwa Sura: Kristo Anaonekana Katika Utukufu

Kugeuzwa Sura: Kristo Anaonekana Katika Utukufu

MATAYO 16:28–17:13 MARKO 9:1-13 LUKA 9:27-36

  • MAONO YA KUGEUZWA SURA

  • MITUME WANASIKIA SAUTI YA MUNGU

Wakati Yesu iko anafundisha watu katika eneo la Kaisaria Filipi, lenye kuwa kwenye kilometre 25 kutoka Mulima Hermoni, anatolea mitume wake tangazo moja lenye kushangaza. Anasema hivi: “Kwa kweli ninawaambia ninyi kwamba kuko wamoja wenye kusimama hapa wenye hawataonja kifo hata kidogo mupaka waone kwanza Mwana wa binadamu akikuja katika Ufalme wake.”—Matayo 16:28.

Wanafunzi wanapaswa kuwa wanajiuliza ikiwa Yesu anataka kusema nini. Karibu juma moja kisha hapo, Yesu anachukua mitume wake tatu, Petro, Yakobo, na Yohana, na anaenda nao mupaka kwenye mulima murefu. Inawezekana ni usiku, kwa sababu wanaume hao watatu wanalala usingizi. Wakati Yesu iko anasali, anageuzwa sura mbele yao. Mitume wanaona uso wake unangaa kama jua, na nguo zake zinangaa kama mwangaza na kuwa mweupe sana.

Kisha kunatokea watu wawili wenye wanatambuliwa kuwa “Musa na Eliya.” Wanaanza kuongea naye juu ya ‘kuondoka kwake kwenye kunapaswa kutokea katika Yerusalemu.’ (Luka 9:30, 31) Inaonekana kuondoka huko kunahusu kifo cha Yesu na kufufuliwa kwake, vyenye alizungumuzia hivi karibuni. (Matayo 16:21) Mazungumuzo hayo yanaonyesha kuwa, tofauti na namna Petro alimushauria, kifo chake chenye haya ni jambo lenye hapaswe kuepuka.

Wakati wanaamuka kabisa, mitume hao tatu wanaona na kusikiliza kwa kushangaa. Ni maono, lakini yanaonekana kuwa ya kweli hivi kwamba Petro anaanza kujitia katika maono hayo kwa kusema hivi: “Rabi, ni muzuri kwetu kuwa hapa. Basi, tusimamishe mahema matatu (3), moja lako, moja la Musa, na moja la Eliya.” (Marko 9:5) Je, Petro anapenda mahema yasimamishwe ili maono hayo yaendelee?

Wakati Petro iko anazungumuza, wingu lenye kungaa linawafunika na sauti inatoka katika wingu yenye kusema hivi: “Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, mwenye nimekubali. Mumusikilize.” Wakati wanasikia sauti ya Mungu, mitume hao wenye kuogopa wanapiga magoti na kuinama mupaka chini, lakini Yesu anawaambia: “Musimame. Musiogope.” (Matayo 17:5-7) Wakati wanasimama, mitume hao tatu wanamuona tu Yesu peke yake. Maono yameisha. Wakati usiku unakucha na wanaanza kushuka kutoka kwenye mulima, Yesu anawaambia hivi: “Musimuambie mutu yeyote maono hayo mupaka wakati Mwana wa binadamu atafufuliwa kutoka kwa wafu.”—Matayo 17:9.

Kuonekana kwa Eliya katika maono kunaamusha ulizo. Mitume wanauliza hivi: “Sababu gani basi, waandishi wanasema ni lazima Eliya akuje kwanza?” Yesu anawajibu hivi: “Ninawaambia ninyi kwamba Eliya amekwisha kuja, na hawakumutambua.” (Matayo 17:10-12) Yesu iko anazungumuza juu ya Yohana Mubatizaji, mwenye alitimiza daraka kama lile la Eliya. Eliya alitayarisha njia kwa ajili ya Elisha, na Yohana alitayarisha njia kwa ajili ya Kristo.

Kwa kweli, maono hayo yalimutia Yesu nguvu na mitume wake! Yanaonyesha utukufu wenye Kristo atakuwa nao katika Ufalme wake. Kwa hiyo, wanafunzi waliona “Mwana wa binadamu akikuja katika Ufalme wake,” kama vile Yesu alikuwa ameahidi. (Matayo 16:28) Wakati walikuwa kwenye mulima, ‘walijionea kwa macho utukufu wake.’ Hata kama Wafarisayo walipenda wapate alama ili wakuwe hakika kama Yesu ndiye Mufalme mwenye Mungu alichagua, Yesu hakuwapatia hata alama moja. Lakini wanafunzi wa karibu wa Yesu walipewa nafasi ya kuona namna anageuzwa sura, na hilo linaonyesha kuwa unabii mbalimbali juu ya Ufalme ni wa kweli. Kwa hiyo, Petro alifikia kuandika hivi: “Tuko na neno la kiunabii lenye limefanywa kuwa hakika zaidi.”—2 Petro 1:16-19.