Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 49

Anahubiri Katika Galilaya na Anazoeza Mitume

Anahubiri Katika Galilaya na Anazoeza Mitume

MATAYO 9:35–10:15 MARKO 6:6-11 LUKA 9:1-5

  • YESU ANAFANYA TENA SAFARI YA KUHUBIRI KATIKA GALILAYA

  • ANATUMA MITUME WAENDE KUHIBIRI

Yesu amekuwa akihubiri sana kwa miaka mbili hivi. Je, sasa ni wakati wa kupumuzika na kujifurahisha? Kuliko kufanya hivyo, Yesu anapanua kazi yake ya kuhubiri kwa “kutembelea miji na vijiji vyote [vya Galilaya], akifundisha katika masinagogi yao na kuhubiri habari njema ya Ufalme na kuponyesha kila namna ya ugonjwa na kila namna ya uzaifu.” (Matayo 9:35) Mambo yenye anaona yanamuhakikishia kuwa kuko lazima ya kupanua kazi ya kuhubiri. Lakini atafanya hivyo namna gani?

Wakati iko anasafiri, Yesu anaona watu wenye wako na lazima ya kuponyeshwa kiroho na kupata kitulizo. Wako kama kondoo wenye hawana muchungaji, wenye kuchunwa ngozi na kutupwa huku na huku. Anawasikilia huruma na kuambia wanafunzi wake hivi: “Ndiyo, mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi wako kidogo. Kwa hiyo, mumuombe Bwana wa mavuno atume wafanyakazi katika mavuno yake.”—Matayo 9:37, 38.

Yesu anajua kile kitasaidia. Anaita mitume hao 12 na kuwagawanya wawili-wawili ili waende kuhubiri. Kisha anawapatia maagizo haya yenye kuwa wazi: “Musiende katika barabara ya mataifa, wala musiingie katika muji wowote wa Wasamaria; lakini tofauti na hilo, muende tu kwa kondoo wenye kupotea wa nyumba ya Israeli. Wakati munaenda, muhubiri na kusema: ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia.’”—Matayo 10:5-7.

Ufalme wenye wanapaswa kuhubiri ni ule wenye Yesu alizungumuzia katika sala ya mufano. ‘Ufalme umekaribia’ katika maana ya kwamba, Mufalme mwenye Mungu amechagua, ni kusema, Yesu, tayari iko hapo. Lakini, ni nini itaonyesha kabisa kuwa wanafunzi wake wanawakilisha Ufalme huo? Yesu anawapatia uwezo wa kuponyesha wagonjwa na hata kufufua wafu, na anawaambia wafanye hivyo kwa bure. Sasa, namna gani mitume watahangaikia mahitaji yao wenyewe, kama vile chakula chao cha kila siku?

Yesu anaambia wanafunzi wake wasijitayarishie vitu vya kimwili kwa ajili ya safari hiyo ya kuhubiri. Hawapaswe kubeba zahabu, feza, ao shaba kwenye mikaba yao ya kuwekea feza. Hawapaswe hata kubeba mufuko wa chakula kwa ajili ya safari wala manguo ingine ao viatu. Sababu gani? Yesu anawahakikishia hivi: “Mufanyakazi anastahili chakula chake.” (Matayo 10:10) Watu wenye wanakuta wenye wanapendezwa na ujumbe wao watasaidia wanafunzi na mambo ya lazima. Yesu anasema hivi: “Kila mahali kwenye mutaingia katika nyumba, mukae mule mupaka wakati mutatoka katika eneo hilo.”—Marko 6:10.

Yesu anawatolea pia maagizo juu ya namna ya kuanzisha mazungumuzo na wenye-nyumba juu ya ujumbe wa Ufalme, kwa kusema hivi: “Wakati munaingia katika nyumba, musalimie watu wa nyumba hiyo. Kama nyumba hiyo inastahili, amani yenye munaitakia ikuwe juu yake; lakini kama haistahili, amani yenu iwarudilie ninyi. Kila mahali kwenye mutu hawapokee wala kusikiliza maneno yenu, wakati munatoka katika nyumba hiyo ao muji huo, mukungute mavumbi yenye kuwa kwenye miguu yenu.”—Matayo 10:12-14.

Inaweza hata kufika kuwa watu wa muji muzima ao kijiji wakatae ujumbe wao. Ni nini itafikia miji na vijiji kama hivyo? Yesu anaonyesha wazi kuwa watapatwa na hukumu kali. Anaeleza hivi: “Kwa kweli ninawaambia ninyi, itakuwa mwepesi zaidi kwa inchi ya Sodoma na Gomora katika Siku ya Hukumu kuliko kwa muji huo.”—Matayo 10:15.