Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 34

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Mbili

Yesu Anachagua Mitume Kumi na Mbili

MARKO 3:13-19 LUKA 6:12-16

  • MITUME KUMI NA MBILI

Kumepita karibu mwaka moja na nusu, tangu Yohana Mubatizaji aseme kuwa Yesu ni Mwana-Kondoo wa Mungu. Wakati Yesu alianza utumishi wake, hesabu fulani ya wanaume wenye mioyo mizuri walifikia kuwa wanafunzi wake, kama vile Andrea, Simoni Petro, Yohana, pengine Yakobo (ndugu ya Yohana), Filipo, na Bartolomayo (mwenye kuitwa pia Natanaeli). Kisha, wengine wengi walijiunga nao na kumufuata Kristo.—Yohana 1:45-47.

Sasa Yesu anataka kuchagua mitume wake. Mitume hao watakuwa marafiki wake wa sana na watapata mazoezi ya pekee. Lakini mbele ya kuwachagua, Yesu anaenda kwenye mulima, pengine mulima wenye kuwa karibu na Bahari ya Galilaya karibu na Kapernaumu. Anapitisha usiku muzima katika sala, pengine anamuomba Mungu hekima na baraka yake. Siku yenye kufuata anaita wanafunzi wake na kuchagua 12 kati ya wanafunzi wake ili wakuwe mitume.

Yesu anachagua watu sita wenye tulitaja kwenye mwanzo wa habari hii, na pia Matayo, mwenye Yesu alikuta kwenye biro ya kodi. Wengine tano wenye Yesu anachagua ni Yuda (mwenye kuitwa pia Tadayo, “mwana wa Yakobo”), Simoni Mukananayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, na Yuda Iskariote.—Matayo 10:2-4; Luka 6:16.

Mupaka sasa mitume hawa 12 wamekuwa wanasafiri pamoja na Yesu, na anawajua muzuri. Wengi kati yao ni watu wa jamaa yake. Bila shaka Yakobo na Yohana ni binamu wa Yesu. Na kama vile watu fulani wanawaza, Alfayo alikuwa ndugu ya Yosefu, baba mulezi wa Yesu; kwa hiyo, mwana wa Alfayo, ni kusema, mutume Yakobo, alipaswa kuwa binamu ya Yesu.

Kwa kweli, haiko vigumu kwa Yesu kukumbuka majina ya mitume wake. Lakini wewe unaweza kukumbuka majina yao? Jambo lenye linaweza kukusaidia ni kukumbuka kama kuko mitume wawili wenye kuitwa Simoni, wawili wenye kuitwa Yakobo, na wawili wenye kuitwa Yuda. Simoni (Petro) iko na ndugu mwenye kuitwa Andrea, na Yakobo (mwana wa Zebedayo) iko na ndugu mwenye kuitwa Yohana. Hiyo ndiyo siri ya kukumbuka majina ya mitume munane. Wengine ine ni mukusanya-kodi (Matayo), ule mwenye alifikia kuwa na mashaka (Tomasi), ule mwenye alialikwa akiwa chini ya muti (Natanaeli), na rafiki ya Natanaeli (Filipo).

Mitume kumi na moja wanatoka Galilaya, eneo kwenye Yesu alikomalia. Natanaeli anatoka Kana. Filipo, Petro, na Andrea wanatoka Betsaida. Petro na Andrea walifikia kuhamia Kapernaumu, kwenye pengine Matayo alikuwa anaishi. Yakobo na Yohana pia wanaishi katika Kapernaumu ao karibu na muji huo, na walikuwa wanafanya kazi yao ya kuvua samaki karibu na muji huo. Yuda Iskariote, mwenye alifikia kumutoa Yesu, inaonekana ni yeye tu ndiye anatoka Yudea.