Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 54

Yesu Ni “Mukate wa Uzima”

Yesu Ni “Mukate wa Uzima”

YOHANA 6:25-48

  • YESU NI “MUKATE KUTOKA MBINGUNI”

Upande wa mashariki mwa Bahari ya Galilaya, Yesu alikulisha kwa njia ya muujiza maelfu ya watu na kisha akawaponyoka wakati walitafuta kumufanya akuwe mufalme. Usiku huo alitembea kwenye bahari yenye upepo mukali na kumuokoa Petro, mwenye alitembea pia juu ya maji lakini akaanza kuzama kwa sababu imani yake iliregea. Yesu alituliza pia upepo, pengine ili kuepusha wanafunzi wake na hatari ya kuvunjikiwa na mashua na kuzama.

Sasa Yesu amerudia upande wa mangaribi mwa bahari, katika eneo la Kapernaumu. Wote wenye alikulisha kwa njia ya muujiza wanamupata na kumuuliza: “Ulifika hapa wakati gani?” Yesu anawakemea na kuwaambia kama wako wanamutafuta na tumaini la kuwa watapata tena chakula. Anawashauria wasifanye ‘kazi kwa ajili ya chakula chenye kinaharibikaka, lakini wafanye kazi kwa ajili ya chakula chenye kinadumu kwa ajili ya uzima wa milele.’ Kwa hiyo, wanauliza hivi: “Tufanye nini ili tutimize kazi za Mungu?”—Yohana 6:25-28.

Pengine wanafikiria kazi zenye kuzungumuziwa katika Sheria, lakini Yesu yeye anazungumuzia kazi ya maana zaidi. Anasema hivi: “Hii ndiyo kazi ya Mungu, kwamba ninyi muamini ule mwenye huyo alimutuma.” Hata kama amekwisha kuwafanyia mambo mengi, watu hawaonyeshe imani katika Yesu. Wanamuomba awafanyie alama fulani ili wamuamini. Wanamuuliza, “Ni kazi gani yenye unafanya? Mababu zetu walikula mana katika jangwa, kama vile imeandikwa: ‘Aliwapatia mukate kutoka mbinguni ili wakule.’”—Yohana 6:29-31; Zaburi 78:24.

Kuhusu ombi lao la kuona alama, Yesu anakazia ule mwenye kuwa kabisa Chanzo cha miujiza. Anasema hivi: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, Musa hakuwapatia ninyi mukate kutoka mbinguni, lakini Baba yangu anawapatia ninyi mukate wa kweli kutoka mbinguni. Kwa maana mukate wa Mungu ni ule mwenye anashuka kutoka mbinguni na anapatia ulimwengu uzima.” Hawaelewe maneno yake, kwa hiyo wanamuomba hivi: “Bwana, tupatie mukate huo sikuzote.” (Yohana 6:32-34) Lakini, ni “mukate” gani wenye Yesu iko anazungumuzia?

Anaeleza hivi: “Mimi ndio mukate wa uzima. Kila mutu mwenye ananifuata hatasikia njaa hata kidogo, na kila mutu mwenye ananiamini hatasikia kiu hata kidogo. Lakini kama vile niliwaambia ninyi, mumeniona hata hivyo hamuamini. . . . Sikushuka kutoka mbinguni ili kufanya mapenzi yangu, lakini ili kufanya mapenzi ya ule mwenye alinituma. Haya ndiyo mapenzi ya ule mwenye alinituma, kwamba nisipoteze hata mumoja kati ya wote wenye amenipatia, lakini niwafufue katika siku ya mwisho. Kwa maana haya ndiyo mapenzi ya Baba yangu, kwamba kila mutu mwenye anakubali Mwana na kumuamini akuwe na uzima wa milele.”—Yohana 6:35-40.

Hilo linawafanya wakasirike, na Wayahudi wanaanza kunungunika juu yake. Namna gani anaweza kusema kama yeye ni “mukate wenye ulishuka kutoka mbinguni”? (Yohana 6:41) Kwao, Yesu ni mutoto tu mwenye wazazi wake ni wanadamu kutoka Galilaya katika muji wa Nazareti. Watu wanauliza hivi: “Je, huyu haiko Yesu mwana wa Yosefu, mwenye tunajua baba yake na mama yake?”—Yohana 6:42.

Yesu anawaambia hivi: “Muache kunungunika kati yenu wenyewe. Hakuna mutu mwenye anaweza kuja kwangu isipokuwa Baba mwenye alinituma amuvute, na mimi nitamufufua katika siku ya mwisho. Imeandikwa katika Manabii: ‘Wote watafundishwa na Yehova.’ Kila mutu mwenye amesikiliza Baba na amejifunza, anakuja kwangu. Haiko kwamba kuko mwanadamu yeyote mwenye amekwisha kumuona Baba, isipokuwa ule mwenye alitoka kwa Mungu; huyo amemuona Baba. Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye anaamini iko na uzima wa milele.”—Yohana 6:43-47; Isaya 54:13.

Mwanzoni, wakati alizungumuza na Nikodemo, Yesu alitaja uzima wa milele na akaonyesha kama ili kupata uzima huo inaomba kuwa na imani katika Mwana wa binadamu. Alisema: “Kila mutu mwenye anamuamini [Mwana muzaliwa-pekee wa Mungu] asiharibiwe lakini apate uzima wa milele.” (Yohana 3:15, 16) Lakini sasa anazungumuza na watu wengi zaidi, na anawaambia kama iko na daraka la kuwasaidia wapate uzima wa milele, uzima wenye mutu hawezi kupata kwa kula mana ao mukate wenye watu wanazoea kula katika Galilaya. Kwa hiyo, namna gani watu wanaweza kupata uzima wa milele? Yesu anarudilia maneno yake kwa kusema hivi: “Mimi ndio mukate wa uzima.”—Yohana 6:48.

Mazungumuzo hayo kuhusu mukate wenye ulitoka mbinguni yanaendelea; yanafika mwisho wakati Yesu iko anafundisha katika sinagogi moja ya Kapernaumu.