Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 20

Muujiza wa Pili Katika Kana

Muujiza wa Pili Katika Kana

MARKO 1:14, 15 LUKA 4:14, 15 YOHANA 4:43-54

  • YESU ANAHUBIRI KWAMBA “UFALME WA MUNGU UMEKARIBIA”

  • ANAPONYESHA KIJANA MWANAUME KWA MBALI

Kisha kufanya siku mbili hivi katika Samaria, Yesu anaenda katika eneo la nyumbani. Amehubiri sana katika Yudea, lakini harudie Galilaya ili kupumuzika. Hata hivyo, anaanzisha utumishi mukubwa zaidi katika inchi kwenye alikomalia. Inawezekana Yesu hatazamie kuwa watamupokea muzuri katika Galilaya, kwa sababu kama vile alisema, “nabii haheshimiwe katika inchi yake mwenyewe.” (Yohana 4:44) Kuliko kubakia pamoja naye, wanafunzi wake wanarudia katika familia zao na wanarudilia pia kazi zenye walikuwa wanafanya.

Yesu anaanza kuhubiri ujumbe gani? Ujumbe ni huu: “Ufalme wa Mungu umekaribia. Mutubu, na mukuwe na imani katika habari njema.” (Marko 1:15) Watu wanatenda namna gani? Kwa kweli, Wagalilaya wengi wanamupokea muzuri, na kumupatia heshima. Hawamupokee hivyo kwa sababu tu ya ujumbe wake. Watu fulani kutoka Galilaya walikuwa kwenye Pasaka kumepita miezi fulani na waliona miujiza yenye Yesu alifanya.—Yohana 2:23.

Katika Galilaya, Yesu anaanzia wapi utumishi wake mukubwa? Inawezekana ni katika Kana, kwenye aligeuza maji kuwa divai kwenye karamu ya ndoa. Wakati iko katika Kana kwa mara hii ya pili, Yesu anapata habari juu ya kijana mwanaume mwenye kuwa mugonjwa sana, karibu kufa. Ni mutoto wa mutumishi fulani wa Herode Antipa, mufalme mwenye alifikia kutoa ruhusa ya kukata Yohana Mubatizaji kichwa. Mutumishi huyo anasikia kuwa Yesu ametoka Yudea na kuenda Kana. Kwa hiyo, mwanaume huyo anatoka Kapernaumu kwenye alikuwa anaishi na kuenda Kana ili kumuona Yesu. Mutumishi huyo mwenye huzuni nyingi anamulilia Yesu hivi: “Bwana, shuka ukuje mbele mutoto wangu mudogo akufe.”—Yohana 4:49.

Yesu anajibu kwa maneno yenye yanapaswa kushangaza mwanaume huyo: “Uende; mwana wako iko muzima.” (Yohana 4:50) Mutumishi wa Herode anaamini maneno ya Yesu na anaanza safari yake ya kurudia nyumbani. Katika safari yake ya kurudia anakutana na watumwa wake, wenye walikuja haraka ili kumupatia habari njema. Ndiyo, mutoto wake ni muzima na iko na afya ya muzuri! Anauliza hivi: “Alipona saa ngapi?” Anapenda kuchunguza ikiwa wakati mutoto alipona unapatana kabisa na wakati Yesu alimuambia kama mutoto wake ni muzima.

Wanamujibu hivi: “Homa ilimutoka jana saa saba (7).”—Yohana 4:52.

Mutumishi huyo anatambua kabisa kama ni saa ileile ndio Yesu alimuambia, “Mwana wako ni muzima.” Kisha jambo hilo kutokea, mwanaume huyo, mwenye kuwa tajiri kiasi cha kuwa na watumwa, na nyumba yake yote wanakuwa wanafunzi wa Kristo.

Kwa hiyo, Kana ni nafasi kwenye Yesu anafanya miujiza mbili; aligeuza maji kuwa divai na kisha anaponyesha kijana mwanaume kwa mbali, kwenye kilometre 26. Kwa kweli, hiyo haiko tu ndiyo miujiza yenye amekwisha kufanya. Lakini, muujiza huo wa kuponyesha ni wa maana sana kwa sababu ni muujiza wenye Yesu anafanya wakati anafika tena Galilaya. Inaonekana wazi kuwa ni yeye ndiye nabii mwenye kukubaliwa na Mungu, lakini ni kwa kiasi gani huyo ‘nabii ataheshimiwa katika inchi yake mwenyewe’?

Hilo litajulikana wazi wakati Yesu ataenda Nazareti. Ni nini inamungojea huko?