Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 32

Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?

Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?

MATAYO 12:9-14 MARKO 3:1-6 LUKA 6:6-11

  • ANAPONYESHA MUKONO WA MWANAUME FULANI SIKU YA SABATO

Kwenye siku ingine ya Sabato, Yesu anaenda kwenye sinagogi fulani, pengine katika Galilaya. Huko anakuta mwanaume mumoja mwenye kuwa na mukono wenye kukauka. (Luka 6:6) Waandishi na Wafarisayo wako wanaangalia Yesu kwa uangalifu. Sababu gani? Wanaonyesha waziwazi mawazo yao wakati wanauliza hivi: “Je, inaruhusiwa kuponyesha siku ya Sabato?”—Matayo 12:10.

Viongozi wa dini ya Kiyahudi wanaamini kuwa kuponyesha mutu kunaruhusiwa siku ya Sabato ikiwa tu uzima uko katika hatari. Kwa mufano, hairusiwe siku ya Sabato kuunganisha mufupa ao kufunga sehemu yenye kuteguka, hali zenye hazitie uzima katika hatari. Kwa kweli, waandishi na Wafarisayo hawaulize Yesu maulizo kwa sababu wanahangaikia kabisa mateso ya mwanaume huyo. Wako wanajikaza kupata visababu ili kumuhukumu Yesu.

Lakini, Yesu anajua mawazo yao ya mubaya. Anatambua kama wamekuwa na mawazo yenye kuvuka mipaka na yenye haitegemee Maandiko kuhusu kuvunja sheria yenye kukataza kufanya kazi siku ya Sabato. (Kutoka 20:8-10) Amekwisha kulaumiwa bila sababu juu ya matendo yake ya muzuri. Sasa Yesu anafanya jambo lenye litatokeza mabishano makubwa kwa kuambia ule mutu mwenye kuwa na mukono wenye kupooza hivi: “Simama na ukuje katikati.”—Marko 3:3.

Yesu anaangalia waandishi na Wafarisayo, na kuwaambia hivi: “Kama uko na kondoo moja, kisha kondoo huyo anaangukia katika shimo siku ya Sabato, je, kuko mutu yeyote kati yenu mwenye hatamukamata na kumutosha ndani?” (Matayo 12:11) Kwa sababu kuwa na kondoo ni kama vile kuweka feza, sasa hawangeacha kondoo huyo katika shimo mupaka siku yenye kufuata; kondoo huyo angekufa wakati huo na kufanya mutu apoteze. Zaidi ya hilo, Maandiko yanasema hivi: “Mutu mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa anatunza wanyama wake wa kufugwa.”—Methali 12:10.

Yesu anafanya ulinganisho wenye usawaziko kwa kusema hivi: “Kama ni vile, mwanadamu ni wa maana sana kupita kondoo! Kwa hiyo, inaruhusiwa kufanya jambo la muzuri siku ya Sabato.” (Matayo 12:12) Kwa hiyo, Yesu havunje Sabato kwa kuponyesha mutu huyo. Viongozi hao wa dini wanashindwa kupinga mawazo hayo yenye kufaa, na yenye kuonyesha huruma. Wanabakia kimya.

Yesu anahuzunishwa na mawazo yao ya mubaya, na anawaangalia kwa kasirani. Kisha anaambia mutu huyo hivi: “Nyoosha mukono wako.” (Matayo 12:13) Wakati mutu huyo ananyoosha mukono wake wenye kupooza, unarudishwa muzima. Hili ni jambo lenye linapaswa kumuletea mutu huyo furaha, lakini hilo linakuwa na matokeo gani kwa wale wenye wanajaribu kumukamata Yesu katika mutego?

Kuliko kufurahi kuwa mukono wa mutu huyo umerudishwa kuwa muzima, Wafarisayo wanatoka inje na mara moja wanaanza kufanya mukutano juu ya Yesu “pamoja na wafuasi wa chama cha Herode, ili kumuua.” (Marko 3:6) Bila shaka, katika chama hicho cha kisiasa ao cha politike, muko pia watu wa kikundi cha dini wenye kuitwa Wasadukayo. Kwa kawaida, Wasadukayo na Wafarisayo wanapingana kati yao, lakini sasa wanajiunga kabisa pamoja ili kumupinga Yesu.