Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 30

Uhusiano wa Yesu Pamoja na Baba Yake

Uhusiano wa Yesu Pamoja na Baba Yake

YOHANA 5:17-47

  • MUNGU NI BABA YA YESU

  • AHADI YA UFUFUO

Wakati Wayahudi fulani wanamushitaki Yesu kuwa anavunja Sabato kwa kumuponyesha mwanaume fulani, Yesu anajibu hivi: “Baba yangu anaendelea kufanya kazi mupaka sasa, na mimi ninaendelea kufanya kazi.”—Yohana 5:17.

Lakini, mambo yenye Yesu anafanya hayakatazwe na sheria ya Mungu juu ya Sabato. Anaiga matendo ya muzuri ya Baba yake kwa kuhubiri na kuponyesha watu. Kwa hiyo, Yesu anaendelea kufanya matendo ya muzuri kila siku. Lakini jibu lenye anapatia wale wenye kumushitaki linawafanya wakasirike hata zaidi, na wanatafuta kumuua Yesu. Sababu gani wanakasirika?

Zaidi ya kuwa na mawazo yenye makosa kama Yesu iko anavunja Sabato kwa kuponyesha watu, wanaona kuwa Yesu amefanya kosa kubwa kwa kusema kama yeye ni Mwana wa Mungu. Wanaona kama anatukana kwa kumuona Mungu kuwa Baba yake; wanaona kuwa wakati Yesu anasema kama Yehova ni Baba yake anajifanya sawasawa na Mungu. Lakini, Yesu haogope na anajibu kwa kuwafasiria zaidi juu ya uhusiano wake wa pekee pamoja na Mungu. Anasema hivi: “Baba anapenda Mwana na anamuonyesha mambo yote yenye yeye mwenyewe anafanya.”—Yohana 5:20.

Baba ndiye Mupaji-Uzima, na zamani alionyesha hilo kwa kupatia wanaume fulani uwezo wa kufufua watu. Yesu anaongeza hivi: “Kama vile Baba anafufua wafu na kuwafanya kuwa wazima, ni vile Mwana pia anafanya kuwa wazima wale wenye anataka.” (Yohana 5:21) Maneno hayo ni yenye maana sana na yanatoa tumaini kwa ajili ya wakati wenye kuja. Hata leo, Mwana iko anafufua watu kiroho. Ndiyo sababu Yesu anasema hivi: “Kila mutu mwenye anasikia neno langu na kumuamini Ule mwenye alinituma iko na uzima wa milele, na haingie katika hukumu lakini amevuka kutoka katika kifo na kuingia katika uzima.”—Yohana 5:24.

Hakuna maandishi yenye kuonyesha kuwa Yesu amekwisha kabisa kufufua mutu mwenye alikuwa amekufa kimwili, lakini anaambia wale wenye kumushitaki kuwa ufufuo kama huo utafanyika. Anasema hivi: “Saa inakuja yenye wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na kutoka.”—Yohana 5:28, 29.

Hata kama Yesu iko na daraka kubwa zaidi, anaonyesha waziwazi kuwa Mungu ni mukubwa kuliko yeye, kwa kusema hivi: “Siwezi kufanya jambo lolote kwa uamuzi wangu mwenyewe. . . . Sitafute mapenzi yangu mwenyewe, lakini mapenzi ya ule mwenye alinituma.” (Yohana 5:30) Hata hivyo, Yesu anazungumuzia daraka lake la maana katika kusudi la Mungu, jambo lenye alikuwa hajafanya mupaka sasa mbele ya watu wengi. Lakini zaidi ya ushuhuda wa Yesu mwenyewe, wale wenye kumushitaki wanajua mengi zaidi juu ya mambo hayo. Yesu anawakumbusha hivi: “Mumetuma watu kwa Yohana [Mubatizaji], na ametoa ushahidi juu ya kweli.”—Yohana 5:33.

Inawezekana wale wenye kumushitaki Yesu walikuwa wamesikia jambo hilo kumepita karibu miaka mbili; Yohana aliambia viongozi wa dini ya Kiyahudi juu ya Ule mwenye kuja nyuma yake, mwenye aliitwa “Nabii” na “Kristo.” (Yohana 1:20-25) Yesu anawakumbusha namna walimuheshimu Yohana mwenye sasa ni mufungwa. Anasema hivi: “Kwa wakati mufupi mulikuwa tayari kufurahi katika mwangaza wake.” (Yohana 5:35) Hata hivyo, Yesu anatoa ushahidi mukubwa zaidi kuliko Yohana Mubatizaji.

“Kazi hizi zenye ninafanya [kutia ndani muujiza wa kuponyesha wenye ametoka tu kufanya] zinatoa ushahidi kwamba Baba alinituma.” Zaidi ya hilo, Yesu anaongeza hivi: “Baba mwenye alinituma ametoa ushahidi yeye mwenyewe juu yangu.” (Yohana 5:36, 37) Kwa mufano, Mungu alitoa ushahidi juu ya Yesu wakati alibatizwa.—Matayo 3:17.

Kwa kweli, wale wenye kumushitaki Yesu hawana sababu yoyote ya kukosa kumuamini. Maandiko yenye wanasema kuwa wanachunguza yanatoa ushahidi juu yake. Yesu anamalizia hivi: “Kama mungemuamini Musa, mungeniamini mimi pia, kwa maana aliandika juu yangu. Lakini kama hamuamini mambo yenye aliandika, namna gani mutaamini mambo yenye ninasema?”—Yohana 5:46, 47.