Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 22

Wanafunzi Ine Watakuwa Wavuvi wa Watu

Wanafunzi Ine Watakuwa Wavuvi wa Watu

MATAYO 4:13-22 MARKO 1:16-20 LUKA 5:1-11

  • YESU ANAALIKA WANAFUNZI WAKE ILI WAMUFUATE WAKATI WOTE

  • WAVUVI WA SAMAKI WANAKUWA WAVUVI WA WATU

Kisha watu wa Nazareti kujaribu kumuua, Yesu anaenda katika muji wa Kapernaumu, pembeni na Bahari ya Galilaya, yenye kuitwa pia “bahari ya Genesareti.” (Luka 5:1) Hilo linatimiza unabii wenye kuwa katika kitabu cha Isaya wenye kusema kama watu wa Galilaya wenye kuishi pembeni ya bahari wangeona mwangaza mukubwa.—Isaya 9:1, 2.

Ndiyo, hapa Galilaya, Yesu anaendelea kutangaza kama “Ufalme wa mbinguni umekaribia.” (Matayo 4:17) Yesu anakutana na wanafunzi wake ine. Mwanzoni walisafiri pamoja naye, lakini kisha kurudia pamoja naye kutoka Yudea, walirudilia kazi yao ya kuvua samaki. (Yohana 1:35-42) Lakini sasa, ni wakati wa kuwa pamoja na Yesu wakati wote ili awazoeze kuendelea na kazi ya kuhubiri wakati atakuwa ameenda.

Wakati Yesu anatembea pembeni ya bahari, anaona Simoni Petro, ndugu yake Andrea, na wavuvi wenzao wakitengeneza nyavu zao. Yesu anapanda ndani ya mashua ya Petro, na anamuomba aipeleke mbali na inchi kavu. Wakati wako mbali kidogo, Yesu anakaa na kuanza kufundisha watu wengi sana wenye kuwa kwenye inchi kavu kweli juu ya Ufalme.

Kisha, Yesu anamuambia Petro hivi: “Peleka mashua mahali penye maji mengi, kisha mushushe nyavu zenu, muvue samaki.” Petro anamujibu hivi: “Mwalimu, tumetumika sana usiku wote na hatukupata kitu, lakini kwa sababu umesema, nitashusha nyavu.”—Luka 5:4, 5.

Wanashusha nyavu na wanakamata samaki wengi sana hivi kwamba nyavu zinaanza kupasuka! Wanaita haraka wenzao wenye kuwa katika mashua ingine wakuje kuwasaidia. Bila kukawia mashua yote mbili inajaa samaki wengi hivi kwamba inakuwa karibu kuzama. Wakati Petro anaona hivyo, anapiga magoti mbele ya Yesu na kusema hivi: “Ondoka kwangu, Bwana, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi.” Yesu anamujibu: “Acha kuogopa. Kuanzia sasa utakuwa unavua watu wakiwa wazima.”—Luka 5:8, 10.

Yesu anaambia Petro na Andrea hivi: “Munifuate, na mimi nitawafanya ninyi kuwa wavuvi wa watu.” (Matayo 4:19) Anaita pia wavuvi wengine wawili wa samaki, Yakobo na Yohana, watoto wa Zebedayo. Wao pia wanakubali bila kusita. Kwa hiyo, watu hao ine wanaacha kazi yao ya kuvua samaki na wanakuwa wanafunzi wa kwanza wa wakati wote wa Yesu.