Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 31

Wanakata Masuke ya Nafaka Siku ya Sabato

Wanakata Masuke ya Nafaka Siku ya Sabato

MATAYO 12:1-8 MARKO 2:23-28 LUKA 6:1-5

  • WANAFUNZI WANAKATA MASUKE YA NAFAKA SIKU YA SABATO

  • YESU NI “BWANA WA SABATO”

Sasa, Yesu na wanafunzi wake wanasafiri kuenda upande wa kaskazini, katika Galilaya. Ni kipindi cha kuchipuka kwa majani, na mbegu zimekwisha kukomaa. Kwa sababu ya njaa, wanafunzi wa Yesu wanakata masuke ya nafaka na kula. Lakini siku hiyo ni ya Sabato, na Wafarisayo wanaangalia kile wanafunzi wako wanafanya.

Kumbuka kama hivi karibuni, Wayahudi katika Yerusalemu walipenda kumuua Yesu, kwa kumushitaki kuwa anavunja Sabato. Sasa Wafarisayo wanaleta shitaka lingine lenye kutegemea matendo ya wanafunzi. Wanamuambia Yesu hivi: “Angalia! Wanafunzi wako wanafanya jambo lenye hairuhusiwe kufanya siku ya Sabato.”—Matayo 12:2.

Wafarisayo wanasema kuwa kukata masuke na kutosha maganda kwa mikono ili kula ni kazi ya kuvuna na kupiga-piga mbegu. (Kutoka 34:21) Mawazo yao yenye kuvuka mipaka kuhusu matendo yenye yanaweza kuonwa kuwa kazi, inafanya Sabato ikuwe muzigo. Lakini, kusudi la Sabato ilikuwa kufanya siku hiyo ikuwe yenye kuleta furaha na yenye kujenga kiroho. Yesu anapinga mawazo yao yenye makosa kwa kutumia mifano ili kuonyesha kuwa Yehova Mungu hakutaka hata kidogo sheria Yake juu ya Sabato itumiwe hivyo.

Mufano moja wenye Yesu anatoa ni wa Daudi na watu wake. Wakati walisikia njaa, walienda kwenye tabenakulo na kula mikate ya toleo. Mikate hiyo, yenye ilikuwa tayari imeondolewa mbele ya Yehova na kubadilishwa na mikate ingine yenye imetoka tu kutengenezwa, kwa kawaida ni makuhani tu ndio walipaswa kuikula. Hata hivyo, katika hali hiyo, Daudi na watu wake hawakulaumiwa kwa sababu walikula mikate hiyo.—Mambo ya Walawi 24:5-9; 1 Samweli 21:1-6.

Katika mufano wa pili, Yesu anasema hivi: “Je, hamukusoma katika Sheria kwamba kila siku ya Sabato makuhani katika hekalu wanavunja Sabato na wanabakia bila kosa?” Yesu anapenda kusema kuwa hata siku ya Sabato, makuhani wanachinja wanyama kwa ajili ya toleo na wanafanya kazi zingine kwenye hekalu. Yesu anasema hivi: “Lakini ninawaambia ninyi, hapa kuko mutu mukubwa kuliko hekalu.”—Matayo 12:5, 6; Hesabu 28:9.

Tena, kwa kutumia Maandiko, Yesu anasema hivi: “Kama mungeelewa maana ya maneno haya, ‘Ninataka rehema hapana zabihu,’ hamungelaumu watu wenye hawana kosa.” Anamalizia kwa kusema hivi: “Kwa maana Mwana wa binadamu ni Bwana wa Sabato.” Yesu iko anazungumuzia wakati wenye atakuwa Mufalme kwa miaka elfu.—Matayo 12:7, 8; Hosea 6:6.

Wanadamu wameteseka sana katika ulimwengu huu wenye kutawaliwa na Shetani, mwenye jeuri na vita vinaendelea kuongezeka. Mambo yatakuwa tofauti kabisa chini ya utawala wa Sabato kubwa wa Kristo. Katika utawala huo, Yesu atatutolea wakati wa mapumuziko wenye tuko nao lazima na wenye tunangojea kwa hamu!