Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 69

Baba yao Ni Nani: Abrahamu ao Ibilisi?

Baba yao Ni Nani: Abrahamu ao Ibilisi?

YOHANA 8:37-59

  • WAYAHUDI WANAJITAPA KUWA ABRAHAMU NI BABA YAO

  • MBELE ABRAHAMU AKUWE, YESU ALIKUWA

Yesu angali katika Yerusalemu kwa ajili ya Sikukuu ya Vibanda, na anaendelea kufundisha kweli za maana. Wayahudi fulani wenye walikuwa hapo wametoka tu kumuambia hivi: “Sisi ni uzao wa Abrahamu na hatujakuwa watumwa wa mutu yeyote hata siku moja.” Yesu anawajibu hivi: “Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Abrahamu. Lakini munatafuta kuniua, kwa sababu neno langu halifanye maendeleo kati yenu. Ninasema mambo yenye niliona wakati nilikuwa pamoja na Baba yangu, lakini ninyi munafanya mambo yenye mulisikia kutoka kwa baba yenu.”—Yohana 8:33, 37, 38.

Yesu iko wazi: Baba yake iko tofauti na baba yao. Wayahudi hawaelewe kile Yesu anapenda kusema, kwa hiyo, wanarudilia maneno yao: “Baba yetu ni Abrahamu.” (Yohana 8:39; Isaya 41:8) Kwa njia ya kimwili, wao ni uzao wake. Kwa hiyo, wanaona kuwa wako na imani kama ile ya rafiki ya Mungu, Abrahamu.

Lakini, Yesu anawatolea jibu hili lenye haliwafurahishe: “Ninyi mungekuwa watoto wa Abrahamu, mungekuwa munafanya kazi za Abrahamu.” Bila shaka, mwana wa kweli anapaswa kuiga baba yake. Yesu anaongeza hivi: “Lakini sasa munatafuta kuniua, mimi mwenye nimewaambia kweli yenye nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya vile.” Kisha Yesu anawaambia maneno haya yenye wanashindwa kuelewa: “Ninyi munafanya kazi za baba yenu.”—Yohana 8:39-41.

Wayahudi hawajaelewa tu mutu mwenye Yesu iko anazungumuzia. Wanajiona kabisa kuwa watoto wa Mungu, wanasema hivi: “Hatukuzaliwa kutokana na uasherati; tuko na Baba mumoja, Mungu.” Lakini, Mungu ni Baba yao kabisa? Yesu anawaambia, “Kama Mungu angekuwa Baba yenu, mungenipenda, kwa maana nilitoka kwa Mungu na niko hapa. Sikukuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, lakini Yeye ndiye alinituma.” Yesu anauliza ulizo na kisha anajibu ulizo hilo yeye mwenyewe: “Sababu gani hamuelewe mambo yenye ninasema? Kwa sababu hamuwezi kusikiliza neno langu.”—Yohana 8:41-43.

Yesu amejaribu kuonyesha matokeo yenye wanaweza kupata kwa sababu ya kumukataa. Lakini sasa anasema hivi moja kwa moja: “Ninyi mumetoka kwa baba yenu Ibilisi, na munataka kufanya tamaa za baba yenu.” Baba yao iko namna gani? Yesu anaonyesha tabia yake kwa kusema hivi: “Huyo alikuwa muuaji wakati alianza, na hakusimama imara katika kweli.” Yesu anaongeza hivi: “Ule mwenye anatoka kwa Mungu anasikiliza maneno ya Mungu. Ndiyo sababu hamusikilize, kwa sababu hamutoke kwa Mungu.”—Yohana 8:44, 47.

Maneno hayo yanakasirikisha sana Wayahudi, na wanajibu hivi: “Je, hatuseme kweli wakati tunasema, ‘Wewe ni Musamaria na uko na pepo muchafu’?” Wanamuita Yesu “Musamaria,” ili kumuzarau. Lakini Yesu hakaze akili juu ya matusi yao, anawajibu hivi: “Mimi sina pepo muchafu, lakini ninamuheshimia Baba yangu, na ninyi munanivunjia heshima.” Hilo ni jambo nzito kwa sababu Yesu anatoa ahadi hii ya ajabu: “Kama mutu yeyote anashika neno langu, hataona kifo hata siku moja.” Yesu hatake kusema kuwa mitume wake na wengine wenye wanamufuata hawatapatwa hata kidogo na kifo cha kimwili. Lakini, anataka kusema kuwa hawataona hata kidogo uharibifu wa milele, ni kusema, “kifo cha pili,” kuharibiwa bila tumaini la kufufuliwa.—Yohana 8:48-51; Ufunuo 21:8.

Lakini Wayahudi hawaelewe kuwa Yesu iko anasema kwa njia ya mufano. Wanasema hivi: “Sasa tunajua uko na pepo muchafu. Abrahamu alikufa, na manabii vilevile, lakini wewe unasema, ‘Kama mutu yeyote anashika neno langu, hataonja kifo hata siku moja.’ Je, wewe ni mukubwa kuliko Abrahamu baba yetu, mwenye alikufa? . . . Unajiona kuwa nani?”—Yohana 8:52, 53.

Ni wazi kuwa Yesu iko anaonyesha kama yeye ni Masiya. Lakini, kuliko kujibia mara moja ulizo lao kuhusu kile iko, Yesu anasema hivi: “Kama ninajitukuza mimi mwenyewe, utukufu wangu hauko kitu. Baba yangu ndiye ananitukuza, ule mwenye munasema ni Mungu wenu. Na bado ninyi hamujamujua, lakini mimi ninamujua. Na kama ningesema simujue, ningekuwa muongo, kama ninyi.”—Yohana 8:54, 55.

Sasa, Yesu anazungumuzia tena babu yao muaminifu kwa kusema hivi: “Abrahamu alifurahi sana katika tumaini la kuona siku yangu, na aliiona na kufurahi.” Ndiyo, kwa kuonyesha imani katika ahadi ya Mungu, Abrahamu alingojea kwa hamu kuja kwa Masiya. Wayahudi hawamuamini. Wanasema hivi: “Wewe haujakuwa hata na miaka makumi tano (50), na je, umekwisha kumuona Abrahamu?” Yesu anawajibu hivi: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mbele ya Abrahamu akuwe, mimi nilikuwa.” Yesu iko anazungumuzia maisha yake akiwa malaika mwenye nguvu mbinguni mbele akuje katika dunia.—Yohana 8:56-58.

Wayahudi, wanakasirika kwa sababu Yesu anasema kuwa alikuwa mbele ya Abrahamu, kwa hiyo wanatafuta kumupiga majiwe. Lakini Yesu anaponyoka bila kuumizwa.