Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 75

Yesu Anaonyesha Siri ya Kupata Furaha

Yesu Anaonyesha Siri ya Kupata Furaha

LUKA 11:14-36

  • ANAFUKUZA PEPO WACHAFU KUPITIA “KIDOLE CHA MUNGU”

  • SIRI YA KUPATA FURAHA YA KWELI

Yesu ametoka tu kurudilia maagizo yake kuhusu sala, lakini haiko jambo hilo tu ndilo anarudilia tena na tena katika utumishi wake. Wakati alikuwa anafanya miujiza katika Galilaya, Yesu alipambana na shitaka la uongo lenye kusema kuwa alikuwa anafanya miujiza kupitia nguvu za mutawala wa pepo wachafu. Sasa, katika Yudea shitaka hilo linaamushwa tena.

Wakati Yesu anafukuza pepo muchafu mwenye kuwa ndani ya mwanaume mumoja na mwenye anamuzuia kusema, watu wanashangaa. Lakini, haikuwe hivyo kwa maadui wake. Wanaamusha tena shitaka lilelile la uongo. Wanasema hivi: “Anafukuza pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli, mutawala wa pepo wachafu.” (Luka 11:15) Wengine wenye wanatafuta Yesu afanye mambo mengine zaidi ili kujua yeye ni nani, wanamuomba afanye alama fulani kutoka mbinguni.

Wakati anatambua kuwa wako wanatafuta kumujaribu, Yesu anawajibu namna alijibu maadui kama hao wenye alikutana nao katika Galilaya. Anasema kuwa kila ufalme wenye umegawanyika na kujipinga wenyewe utaanguka. Anafikiri nao hivi: “Kama Shetani amegawanyika juu yake mwenyewe, ufalme wake utasimama namna gani?” Kisha Yesu anawaambia moja kwa moja hivi: “Kama ninafukuza pepo wachafu kupitia kidole cha Mungu, kwa kweli, Ufalme wa Mungu umekwisha kuwafikia ninyi.”—Luka 11:18-20.

Maneno “kidole cha Mungu,” yenye Yesu anataja yanapaswa kukumbusha wasikilizaji wake mambo yenye yalifanyika zamani katika historia ya Israeli. Wale wenye walikuwa katika nyumba ya Farao wenye waliona namna Musa anafanya muujiza, walisema kwa sauti kubwa hivi: “Ni kidole cha Mungu!” Pia, ni “kidole cha Mungu” kiliandika Amri Kumi kwenye mabamba ya majiwe. (Kutoka 8:19; 31:18) Vilevile, ni “kidole cha Mungu,” ni kusema, roho yake takatifu, ao nguvu yake ya utendaji ndiyo inamupatia sasa Yesu uwezo wa kufukuza pepo wachafu na kuponyesha wagonjwa. Kwa hiyo, Ufalme wa Mungu umekwisha kuwafikia maadui hawa, kwa sababu Yesu, Mufalme wa Ufalme mwenye amechaguliwa, tayari iko hapo akitimiza kazi hizo za ajabu.

Uwezo wa Yesu wa kufukuza pepo wachafu unaonyesha waziwazi kuwa iko na mamlaka juu ya Shetani, kama vile tu mutu mwenye nguvu nyingi anaweza kushambulia mulinzi mwenye kuwa na silaha na kupata ushindi juu yake. Yesu anarudilia pia mufano wake kuhusu roho muchafu mwenye anamutoka mwanaume mumoja. Ikiwa mwanaume huyo harudishe mahali penye kukosa vitu vya muzuri, roho huyo atarudia na roho wengine saba, na kufanya hali ya mwanaume huyo ikuwe mubaya zaidi kuliko ile ya kwanza. (Matayo 12:22, 25-29, 43-45) Kwa hiyo, hali iko hivyo kwa taifa la Israeli.

Mwanamuke mumoja mwenye kumusikiliza Yesu anafikia kusema kwa sauti kubwa hivi: “Lenye furaha ni tumbo la uzazi lenye lilikuchukua na maziwa yenye ulinyonya!” Wanamuke Wayahudi walitumaini kama watakuwa mama ya nabii fulani, zaidi sana mama ya Masiya. Kwa hiyo, pengine mwanamuke huyo anafikiri kuwa Maria anaweza kuwa mwenye furaha sana kwa sababu yeye ni mama ya mwalimu kama huyo. Lakini, Yesu anarekebisha mawazo ya mwanamuke huyo kwa kueleza kile kinaweza kabisa kuleta furaha. Anasema hivi: “Hapana, lakini, wenye furaha ni wale wenye wanasikia neno la Mungu na kulishika!” (Luka 11:27, 28) Yesu hajasemaka hata siku moja kuwa watu wanapaswa kupatia Maria heshima ya pekee. Lakini, mwanaume ao mwanamuke yeyote anaweza kupata furaha ya kweli ikiwa anamutumikia Mungu kwa uaminifu. Mutu hapate furaha hiyo kwa sababu ni wa jamaa ya mutu fulani ao kwa sababu ya mambo yenye anatimiza.

Kama vile Yesu alifanya katika Galilaya, anakemea watu kwa sababu wanamuomba afanye alama fulani kutoka mbinguni. Yesu anasema kuwa hakuna alama hata moja yenye itatolewa isipokuwa tu “alama ya Yona.” Yona alikuwa alama kupitia siku tatu zenye alifanya ndani ya samaki na kupitia kazi yake ya kuhubiri kwa ujasiri, kazi yenye ilisaidia Waninawi watubu. Yesu anasema hivi: “Lakini muangalie! hapa kuko kitu kikubwa kuliko Yona.” (Luka 11:29-32) Pia, Yesu ni mukubwa zaidi kuliko Sulemani, mwenye alikuwa na hekima yenye malkia wa Sheba alikuja kusikia.

Yesu anaongeza hivi: “Wakati mutu amewasha taa, haiweke mahali kwenye kujificha, ao chini ya kitunga, lakini anaiweka juu ya kinara cha taa.” (Luka 11:33) Pengine anataka kusema kuwa kufundisha na kufanya miujiza mbele ya watu hao ni kama vile kuficha mwangaza wa taa. Kwa sababu macho yao yamekengeushwa, wanakosa kusudi la miujiza yake.

Yesu ametoka tu kufukuza pepo muchafu na kufanya mwanaume mwenye hakukuwa anasema aanze kusema. Hilo linapaswa kuchochea watu wamutukuze Mungu na kuambia wengine mambo yenye Yehova iko anatimiza. Kwa hiyo, Yesu anatolea kila mumoja wa maadui wake onyo hili: “Ukuwe muangalifu ili mwangaza wenye kuwa ndani yako usikuwe giza. Kwa hiyo, kama mwili wako wote ni wenye mwangaza na hakuna sehemu yoyote yenye kuwa na giza, wote utakuwa wenye mwangaza kama vile wakati taa inakuangazia kwa miali yake.”—Luka 11:35, 36.