Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 80

Muchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo

Muchungaji Mwema na Mazizi ya Kondoo

YOHANA 10:1-21

  • YESU ANAZUNGUMUZA JUU YA MUCHUNGAJI MWEMA NA MAZIZI YA KONDOO

Wakati anaendelea kufundisha katika Yudea, Yesu anatumia jambo lenye litakuwa mwepesi kwa wasikilizaji wake kuelewa: kondoo na mazizi ya kondoo. Lakini iko anazungumuza kwa njia ya mufano. Pengine Wayahudi wanakumbuka maneno haya ya Daudi: “Yehova ni Muchungaji wangu. Sitakosa kitu. Ananilalisha katika malisho yenye majani mengi.” (Zaburi 23:1, 2) Katika zaburi ingine, Daudi alitolea taifa mwaliko huu: “Tupige magoti mbele ya Yehova Mutengenezaji wetu. Kwa maana yeye ni Mungu wetu, na sisi tuko watu wa malisho yake.” (Zaburi 95:6, 7) Ndiyo, tangu wako chini ya Sheria, Waisraeli wamekuwa wakifananishwa na kundi la kondoo.

“Kondoo” hawa wamekuwa katika “zizi la kondoo” katika maana ya kwamba walizaliwa chini ya agano la Sheria ya Musa. Sheria ilikuwa kama vile ukuta, wenye uliwalinda ili wasiambukizwe na tabia za mubaya za watu wenye hawakukuwa chini ya mupango huo. Lakini Waisraeli fulani walitendea mubaya kondoo wa Mungu. Yesu anasema hivi: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mutu mwenye haingie katika zizi la kondoo kupitia kwenye mulango, lakini anapanda na kuingia kupitia njia nyingine, ni mwizi na muporaji. Lakini ule mwenye anaingia kupitia kwenye mulango ndiye muchungaji wa kondoo.”—Yohana 10:1, 2.

Pengine watu wanafikiria wanaume wenye wamejitangaza kuwa Masiya, ao Kristo. Wanaume hao wako kama vile wezi na waporaji. Watu hawapaswe kufuata wanaume hao wenye wanadanganya watu. Lakini, wanapaswa kufuata “muchungaji wa kondoo.” Yesu anasema hivi juu ya muchungaji huyo:

“Mulinzi wa mulango anamufungulia, na kondoo wanasikiliza sauti yake. Anaita kondoo wake mwenyewe kwa majina yao na anawapeleka inje. Kisha kupeleka inje kondoo wake wote, anaenda mbele yao, na kondoo wanamufuata, kwa sababu wanajua sauti yake. Hawatafuata mugeni hata kidogo lakini watamukimbia, kwa sababu hawajue sauti ya wageni.”—Yohana 10:3-5.

Mbele ya hapo, Yohana Mubatizaji, kama vile mulinzi wa mulango, alionyesha kuwa Yesu ndiye muchungaji mwenye kondoo hao wa mufano wenye kuwa chini ya Sheria walipaswa kufuata. Na kondoo fulani, katika Galilaya na hapa katika Yudea, wametambua sauti ya Yesu. ‘Anawatosha inje’ ili kuwapeleka wapi? Na ni nini itatokea ikiwa wanamufuata? Watu fulani wenye kusikiliza mufano huu wanaweza kujiuliza hivyo, kwa sababu ‘hawaelewe kile iko anawaambia.’—Yohana 10:6.

Yesu anafasiria hivi: “Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, mimi ndiye mulango wa kondoo. Wale wote wenye wamekuja pa nafasi yangu ni wezi na waporaji; lakini kondoo hawakuwasikiliza. Mimi ndiye mulango; kila mutu mwenye anaingia kupitia mimi ataokolewa, na ataingia na kutoka na kupata malisho.”—Yohana 10:7-9.

Ni wazi kwamba, Yesu iko anazungumuzia jambo fulani la mupya. Wasikilizaji wake wanajua kuwa yeye haiko mulango wenye kuongoza kwenye agano la Sheria, wenye umekuwako kwa mamia ya miaka. Kwa hiyo, anapaswa kuwa iko anasema kama kondoo wenye ‘anatosha inje’ wanapaswa kuingia katika zizi lingine. Na hilo litakuwa na matokeo gani?

Yesu anafasiria zaidi daraka lake kwa kusema hivi: “Mimi nimekuja ili wapate uzima na waupate kwa wingi. Mimi ndiye muchungaji mwema; muchungaji mwema anatoa uzima wake kwa ajili ya kondoo.” (Yohana 10:10, 11) Mbele ya hapo, Yesu alitia wanafunzi wake moyo kwa kuwaambia hivi: “Musiogope, kundi ndogo, kwa maana Baba yenu amekubali kuwapatia ninyi Ufalme.” (Luka 12:32) Kwa kweli, wale wenye wanafanyiza “kundi ndogo” ni watu wenye Yesu ataongoza katika zizi la mupya, ili waweze ‘kupata uzima na waupate kwa wingi.’ Ni baraka kabisa kuwa katika kundi hilo!

Lakini, Yesu hamalizie jambo hilo pale. Anasema hivi: “Na niko na kondoo wengine, wenye hawako wa zizi hili; hao pia lazima niwalete, na watasikiliza sauti yangu, na watakuwa kundi moja, muchungaji mumoja.” (Yohana 10:16) “Kondoo wengine” hao, “hawako wa zizi hili.” Kwa hiyo, wanapaswa kuwa wa zizi lingine, tofauti na “kundi ndogo” wenye watariti Ufalme. Mazizi haya mbili ya kondoo yako na matumaini mbili tofauti. Lakini, kondoo wa mazizi yote mbili watafaidika na daraka la Yesu. Anasema hivi: “Ndiyo sababu Baba ananipenda, kwa sababu ninatoa uzima wangu.”—Yohana 10:17.

Watu wengi kati ya watu hao wanasema hivi: “Iko na pepo muchafu na amepoteza akili.” Lakini wengine wanaonyesha kuwa wako wanamusikiliza kwa uangalifu na wako tayari kufuata Muchungaji Mwema. Wanasema hivi: “Haya hayako maneno ya mutu mwenye pepo muchafu. Je, pepo muchafu anaweza kufungua macho ya vipofu?” (Yohana 10:20, 21) Ni wazi kwamba wako wanafikiria jambo lenye Yesu alifanya mbele ya hapo la kuponyesha mwanaume mumoja mwenye alizaliwa kipofu.