Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA  73

Musamaria Anaonyesha Kuwa Yeye Ni Jirani wa Kweli

Musamaria Anaonyesha Kuwa Yeye Ni Jirani wa Kweli

LUKA 10:25-37

  • NAMNA MUTU ANAWEZA KURITI UZIMA WA MILELE

  • MUSAMARIA MWEMA

Wakati Yesu angali karibu na Yerusalemu, Wayahudi wengi wanamukaribia. Wamoja wanapenda awafundishe na wengine wanapenda kumujaribu. Mumoja wao, mutu fulani mwenye kujua sana Sheria, anauliza hivi: “Mwalimu, nifanye nini ili niriti uzima wa milele?”—Luka 10:25.

Yesu anatambua kuwa mwanaume huyo haulize tu kwa sababu anapenda kujua. Pengine iko anamujaribu Yesu ili atoe jibu fulani lenye litakwaza Wayahudi. Yesu anatambua kuwa mwanaume huyo tayari iko na mawazo fulani. Kwa hiyo, Yesu anatumia hekima ili kutoa jibu lenye litafanya mwanaume huyo afunue mawazo yake.

Yesu anamuuliza hivi: “Ni nini imeandikwa katika Sheria? Wewe unasoma namna gani?” Mwanaume huyo amejifunza Sheria ya Mungu, kwa hiyo, anatoa jibu lenye kutegemea Sheria hiyo. Anataja maneno yenye kuwa katika Kumbukumbu la Torati 6:5 na Mambo ya Walawi 19:18, kwa kusema: “‘Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote’ na ‘jirani yako kama wewe mwenyewe.’” (Luka 10:26, 27) Je, hilo ndilo jibu?

Yesu anaambia mwanaume huyo hivi: “Umejibu muzuri; endelea kufanya vile na utapata uzima.” Lakini hilo linamaliza mazungumuzo? Mwanaume huyo hapendi tu kupata jibu lenye ni la kweli; iko anatafuta “kujionyesha mwenye kufanya mambo yenye kuwa sawa,” na kuhakikisha kwamba mawazo yake yako sawa na kwamba iko na haki ya kutendea wengine vile iko anawatendea. Kwa hiyo, anauliza hivi: “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” (Luka 10:28, 29) Ulizo hilo linaonekana kuwa mwepesi, lakini liko na maana kubwa. Namna gani?

Wayahudi wanaamini kuwa neno “jirani” linahusu tu wale wenye wanafuata desturi za Wayahudi, na inaonekana kuwa andiko la Mambo ya Walawi 19:18 linaunga mukono jambo hilo. Kwa kweli, Muyahudi anaweza hata kusema kuwa ‘hairuhusiwe’ kujiunga na mutu mwenye haiko Muyahudi. (Matendo 10:28) Kwa hiyo, mwanaume huyu na pengine wanafunzi fulani wa Yesu mwenyewe wanaona kama watakuwa wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa ikiwa wanatendea Wayahudi wenzao kwa wema. Lakini wanaona kuwa hawawezi kutendea kwa wema mutu mwenye haiko Muyahudi; mutu huyo haiko kabisa “jirani.”

Namna gani Yesu atarekebisha mawazo hayo bila kukwaza mwanaume huyo na Wayahudi wengine? Anafanya hivyo kwa kueleza hadisi fulani: “Mutu fulani alikuwa anashuka kutoka Yerusalemu kuenda Yeriko na akaanguka katika mikono ya wanyanganyi; wakamuvua nguo, wakamupiga, kisha wakaenda na kumuacha akiwa karibu kufa.” Yesu anaendelea: “Ikatokea kwamba kuhani fulani alikuwa anapita katika barabara hiyo, lakini wakati alimuona, akapita ngambo ingine ya barabara. Vilevile, Mulawi mumoja wakati alifika pale na kumuona, akapita ngambo ingine ya barabara. Lakini Musamaria fulani mwenye alikuwa anasafiri katika barabara hiyo akafika mahali alikuwa, na wakati alimuona, akamusikilia huruma.”—Luka 10:30-33.

Mwanaume mwenye Yesu anaelezea hadisi hii anajua muzuri kuwa makuhani wengi na watumishi wa hekalu Walawi wanaishi katika Yeriko. Kutoka kwenye hekalu ili kurudia Yeriko, wanapaswa kufanya safari ya kilometre 23 hivi. Barabara inaweza kuwa yenye hatari, kwa sababu wanyanganyi wanajificha katika barabara hiyo ili kutendea watu mubaya. Ikiwa kuhani na Mulawi wanakuta Muyahudi mwenzao katika magumu, hawapaswe kumusaidia? Katika hadisi hii, Yesu anaonyesha kuwa hawakumusaidia. Ule mwenye alimusaidia alikuwa Musamaria, mwanaume mwenye kuwa kati ya watu wenye Wayahudi wanazarau.—Yohana 8:48.

Namna gani ule Musamaria alisaidia Muyahudi huyo mwenye aliumizwa? Yesu anaendelea kwa kusema hivi: “Akamukaribia, akamwanga mafuta na divai juu ya vidonda vyake, na akavifunga. Kisha akamupandisha kwenye munyama wake, akamupeleka kwenye nyumba ya kupangisha wageni na kumutunza. Siku yenye ilifuata, akakamata dinari mbili, akazipatia musimamizi wa ile nyumba, na akamuambia: ‘Umutunze, na kila kitu chenye utatumia zaidi ya hiki, nitakulipa wakati nitarudia.’”—Luka 10:34, 35.

Kisha kueleza hadisi hiyo, Mwalimu Mukubwa, Yesu, anauliza mwanaume huyo ulizo hili lenye kumuchochea afikiri: “Ni nani kati ya watu hao watatu (3) mwenye unaona alijifanya kuwa jirani wa ule mutu mwenye alianguka katika mikono ya wanyanganyi?” Pengine mwanaume huyo atajisikia mubaya ikiwa anasema kuwa ni “Musamaria,” kwa hiyo anajibu hivi: “Ni ule mwenye alimutendea kwa rehema.” Kisha, Yesu anafanya somo la hadisi hiyo likuwe wazi kabisa kwa kushauria mwanaume huyo hivi: “Uende, na ufanye vilevile.”—Luka 10:36, 37.

Hiyo ni njia ya muzuri sana ya kufundisha! Ikiwa Yesu aliambia tu mwanaume huyo kuwa watu wenye hawako Wayahudi wako pia majirani, mwanaume huyo na Wayahudi wengine wangekubali jambo hilo? Pengine hapana. Lakini, kwa kueleza hadisi yenye kuwa mwepesi, akitumia mambo yenye wasikilizaji wanajua muzuri, jibu la ulizo, “Kwa kweli jirani yangu ni nani?” linakuwa wazi. Jirani wa kweli ni mutu mwenye anaonyesha upendo na wema; sifa zenye Maandiko yanatuomba tuonyeshe.