Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 78

Musimamizi-Nyumba Mwaminifu, Endelea Kuwa Tayari!

Musimamizi-Nyumba Mwaminifu, Endelea Kuwa Tayari!

LUKA 12:35-59

  • MUSIMAMIZI-NYUMBA MWAMINIFU ANAPASWA KUENDELEA KUWA TAYARI

  • YESU ANAKUJA KULETA MUGAWANYIKO

Yesu amefasiria kuwa ni “kundi ndogo” ndio watapata nafasi katika Ufalme wa mbinguni. (Luka 12:32) Lakini kupata zawadi hiyo ya ajabu ni jambo la kuchukua kwa uzito. Kwa kweli, Yesu anaendelea kukazia kwamba ili mutu afikie kuwa katika Ufalme ni jambo la maana akuwe na moyo muzuri.

Ndiyo sababu Yesu anashauria wanafunzi wake waendelee kuwa tayari kwa ajili ya kuja kwake. Anasema hivi: “Muvae nguo na mukuwe tayari na taa zenu zikuwe zenye kuwaka, na mukuwe kama watu wenye wanangojea bwana wao arudie kutoka kwenye ndoa, ili wakati atakuja na kupiga hodi, wamufungulie mara moja. Wenye furaha ni watumwa wenye wakati bwana wao anakuja, anawakuta wako wanakesha!”—Luka 12:35-37.

Ni mwepesi kwa wanafunzi kuelewa hali yenye Yesu iko anazungumuzia katika mufano wake. Watumishi wenye anazungumuzia wako tayari, wakingojea kurudia kwa bwana wao. Yesu anaeleza hivi: “Kama [bwana] anakuja katika kesha la pili [kuanzia karibu saa tatu ya usiku mupaka saa sita ya usiku], ao hata kesha la tatu (3) [kuanzia saa sita ya usiku mupaka karibu saa kenda ya usiku], na anawakuta wako tayari, wao ni wenye furaha!”—Luka 12:38.

Hilo haliko tu shauri kuhusu kuwa watumishi ao wafanyakazi wa nyumbani wenye bidii, lakini linamaanisha mambo mengi zaidi. Namna Yesu, Mwana wa binadamu, anajitia katika mufano huo inafanya jambo hilo likuwe wazi. Anaambia wanafunzi wake: “Ninyi pia, muendelee kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa yenye hamutazamie.” (Luka 12:40) Kwa hiyo, wakati fulani wenye kuja, Yesu atafika. Anapenda wafuasi wake, zaidi sana wale wa “kundi ndogo,” wakuwe tayari.

Petro anapenda aelewe muzuri maana ya maneno ya Yesu. Kwa hiyo anauliza hivi: “Bwana, ni sisi tu unaambia mufano huo ao ni watu wote?” Kuliko kumujibia Petro moja kwa moja, Yesu anatoa mufano wenye kuwa na uhusiano na ule wa kwanza. Anasema hivi: “Ni nani kwa kweli musimamizi-nyumba mwaminifu, mwenye busara, mwenye bwana wake atamuweka asimamie watumishi wake ili aendelee kuwapatia kipimo chao cha chakula kwa wakati wenye kufaa? Mwenye furaha ni mutumwa huyo kama bwana wake wakati atakuja atamukuta iko anafanya vile! Kwa kweli ninawaambia ninyi, atamuweka juu ya mali zake zote.”—Luka 12:41-44.

Ni wazi kuwa katika mufano wa kwanza, “bwana” mwenye kuzungumuziwa ni Yesu, Mwana wa binadamu. Bila shaka, “musimamizi-nyumba mwaminifu, mwenye busara” anatia ndani wale wenye kuwa sehemu ya “kundi ndogo” na ambao watapewa Ufalme. (Luka 12:32) Yesu iko anasema kuwa watu fulani wa kundi hilo watakuwa wakitolea “watumishi wake” chakula, ni kusema, “kipimo chao cha chakula kwa wakati wenye kufaa.” Kwa hiyo Petro na wanafunzi wengine wenye Yesu iko anafundisha na kukulisha kiroho wanafikia kuelewa kuwa wakati wenye kuja kutakuwa kipindi fulani chenye Mwana wa binadamu atakuja. Na katika kipindi hicho, mipango itafanywa ili kukulisha kiroho wafuasi wa Yesu, ni kusema, “watumishi” wa Bwana.

Yesu anakazia kwa njia ingine sababu gani wanafunzi wake wanapaswa kuwa waangalifu kuhusu namna yao ya kuwa. Kwa sababu inawezekana mutu afikie kuanza kukosa kukamata mambo kwa uzito na kufikia hata kupingana na ndugu na dada zake. Yesu anasema hivi: “Lakini kama mutumwa huyo anasema katika moyo wake, ‘Bwana wangu anakawia kuja,’ na anaanza kupiga watumishi wanaume na watumishi wanamuke na kula na kunywa na kulewa, bwana wa mutumwa huyo atakuja siku yenye hakumutazamia na saa yenye hajue, na atamupatia azabu kwa ukali mukubwa zaidi na kumupatia sehemu na wale wenye hawako waaminifu.”—Luka 12:45, 46.

Yesu anasema kama alikuja “kuwasha moto katika dunia.” Na amefanya hivyo, kwa kuzungumuzia mambo yenye yanaleta mabishano yenye kuwa kama moto na kufikia kuunguza desturi na mafundisho ya uongo. Hilo linagawanya hata watu wenye wangepaswa kuwa katika umoja, kwa kuleta mugawanyiko “kati ya baba na mwana, kati ya mwana na baba, kati ya mama na binti, kati ya binti na mama, kati ya mama-mukwe na binti-mukwe, na kati ya binti-mukwe na mama-mukwe.”—Luka 12:49, 53.

Maneno hayo yalihusu zaidi sana wanafunzi wake. Kisha Yesu anaanza sasa kuzungumuza na watu wenye walikuwa hapo. Wengi kati ya watu hao walifanya vichwa vigumu kwa kukataa kukubali ushuhuda wenye kuonyesha kuwa yeye ni Masiya; kwa hiyo anawaambia hivi: “Wakati munaona wingu linatokea upande wa mangaribi, mara moja munasema, ‘Upepo unakuja,’ na inakuwa vile. Na wakati munaona kama upepo wa kusini unavuma, munasema, ‘Kutakuwa joto kubwa,’ na inakuwa vile. Wanafiki, munajua namna ya kuchunguza hali ya dunia na ya anga, lakini sababu gani hamujue kuchunguza wakati huu?” (Luka 12:54-56) Ni wazi kuwa hawako tayari.