Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 79

Sababu Gani Uharibifu Uko Unakuja

Sababu Gani Uharibifu Uko Unakuja

LUKA 13:1-21

  • YESU ANAFUNDISHA SOMO FULANI KUPITIA MISIBA MBILI

  • MWANAMUKE KILEMA ANAPONYESHWA SIKU YA SABATO

Yesu amejikaza katika njia nyingi kuchochea watu wafikirie urafiki wao pamoja na Mungu. Nafasi ingine inajitokeza kisha mazungumuzo yake pamoja na watu wenye kuwa inje ya nyumba ya Mufarisayo mumoja.

Wamoja kati ya watu hao wanazungumuzia musiba fulani wenye ulitokea. Wanamuelezea juu ya “Wagalilaya wenye [Gavana Muroma Pontio] Pilato alichanganya damu yao pamoja na zabihu zao.” (Luka 13:1) Wanataka kusema nini?

Pengine Wagalilaya hao walikuwa watu wenye waliuawa wakati maelfu ya Wayahudi walimupinga Pilato juu ya kutumikisha feza za hazina ya hekalu ili kujenga mufereji wa kuleta maji katika Yerusalemu. Pengine Pilato alipata feza hizo kwa kusikilizana na wakubwa wa hekalu. Pengine wale wenye kueleza musiba huo wanafikiri kuwa Wagalilaya walipatwa na musiba huo kwa sababu ya matendo yao ya mubaya. Yesu hakubali jambo hilo.

Anauliza hivi: “Je, munawaza Wagalilaya hao walikuwa watenda-zambi wabaya sana kuliko Wagalilaya wengine wote kwa sababu mambo hayo yaliwapata?” Jibu lake ni hapana. Lakini, anatumia tukio hilo ili kutolea Wayahudi onyo hili: “Kama hamutubu, ninyi pia mutaharibiwa kama wao.” (Luka 13:2, 3) Kisha Yesu anazungumuzia musiba mwingine wenye pengine ulitokea hivi karibuni na wenye pengine uko na uhusiano na ujenzi wa mufereji huo, kwa kuuliza hivi:

“Wale kumi na munane (18) wenye munara uliangukia kule Siloamu, na kuwaua—je, munawaza walikuwa na hatia kubwa kuliko watu wengine wote wenye kuishi Yerusalemu?” (Luka 13:4) Watu wanaweza kufikiri kuwa watu hao walikufa kwa sababu ya matendo yao ya mubaya. Tena, Yesu anapinga jambo hilo. Anajua kuwa “wakati na mambo yenye hayatazamiwe” yanafikia watu na pengine hilo ndilo lilifanya musiba huo utokee pia. (Mhubiri 9:11) Lakini, tukio hilo linapaswa kufundisha watu hao jambo fulani. Yesu anasema hivi: “Kama hamutubu, ninyi pia mutaharibiwa kama wao.” (Luka 13:5) Lakini, sababu gani iko anakazia somo hilo sasa?

Ni kwa sababu ya kipindi cha wakati chenye amefikia katika utumishi wake. Kwa hiyo, anatoa mufano huu: “Mutu fulani alikuwa na muti wa tini wenye kupandwa katika shamba lake la mizabibu, na akakuja kutafuta matunda juu ya muti huo lakini hakupata hata moja. Kisha akamuambia mufanyakazi wa shamba la mizabibu, ‘Kwa miaka tatu (3) nimekuwa nikikuja kutafuta matunda kwenye muti huu wa tini, lakini sikupata hata moja. Uukate! Sababu gani uendelee kuacha udongo bila faida?’ Akamujibu ‘Bwana, acha muti huu kwa mwaka mwingine mumoja, nichimbe kuuzunguka na kuutilia mbolea. Kama unazaa matunda wakati wenye kuja, ni muzuri; lakini kama hauzae, basi utaukata.’”—Luka 13:6-9.

Kwa zaidi ya miaka tatu, Yesu amekuwa akijikaza kusaidia Wayahudi wakomalishe imani. Hata hivyo, ni watu wadogo tu ndio wamekuwa wanafunzi wake na wanaweza kuonwa kuwa matunda ya kazi yake ya jasho. Sasa, katika mwaka wa ine wa utumishi wake, anaongeza tena bidii. Ni kama vile alikuwa anachimba na kuweka mbolea kwenye muti wa tini, ni kusema, Wayahudi, kwa kuhubiri na kufundisha katika Yudea na Perea. Anapata matokeo gani? Ni hesabu kidogo tu ya Wayahudi ndio wanapendezwa. Kwa ujumla, taifa lote linakataa kutubu na sasa litaangamizwa.

Kukosa kupendezwa huko kunaonekana tena muda kidogo kisha, kwenye siku ya Sabato. Yesu iko anafundisha katika sinagogi fulani. Anaona mwanamuke mumoja mwenye, kwa sababu pepo muchafu iko anamutesa, mwili wake ulikuwa umejikunja mara mbili kwa miaka 18. Yesu anamusikilia huruma; kwa hiyo anamuambia hivi: “Mwanamuke, umefunguliwa kutoka katika uzaifu wako.” (Luka 13:12) Yesu anaweka mikono yake juu ya mwanamuke huyo, na mara moja anasimama wima na kuanza kutukuza Mungu.

Jambo hilo linakasirikisha mukubwa-musimamizi wa sinagogi, na anasema hivi: “Kuko siku sita (6) za kufanya kazi; basi, mukuje muponyeshwe siku hizo, lakini hapana siku ya Sabato.” (Luka 13:14) Musimamizi huyo hakatae kuwa Yesu iko na nguvu za kuponyesha watu; lakini, iko analaumu watu kwa sababu wako wanakuja ili waponyeshwe siku ya Sabato! Yesu anamujibu kwa kumuambia waziwazi hivi: “Wanafiki, je, kila mumoja wenu hamufungue ngombe-dume wake ao punda wake katika kibanda siku ya Sabato na kumupeleka akunywe? Je, mwanamuke huyu, ambaye ni binti ya Abrahamu na mwenye Shetani alikuwa amemufunga kwa miaka kumi na munane (18), haingefaa afunguliwe kutoka katika kifungo hiki siku ya Sabato?”—Luka 13:15, 16.

Maadui wake wanasikia haya, lakini watu wengi wanafurahi kwa sababu ya mambo ya ajabu yenye wako wanaona Yesu anafanya. Kisha Yesu anarudilia hapa katika Yudea mifano mbili ya kiunabii kuhusu Ufalme, yenye alizungumuzia mbele ya hapo, wakati alikuwa katika mashua kwenye Bahari ya Galilaya.—Matayo 13:31-33; Luka 13:18-21.