Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 66

Iko Katika Yerusalemu kwa Ajili ya Sikukuu ya Tabenakulo

Iko Katika Yerusalemu kwa Ajili ya Sikukuu ya Tabenakulo

YOHANA 7:11-32

  • YESU ANAFUNDISHA KATIKA HEKALU

Watu wengi wamemujua Yesu muzuri katika miaka yenye amefanya tangu kubatizwa kwake. Maelfu ya Wayahudi wameona miujiza yake, na habari kuhusu miujiza yake imejulikana katika inchi yote. Sasa, kwenye Sikukuu ya Tabenakulo (ao, ya Vibanda) katika Yerusalemu, watu wengi wako wanamuangalia.

Watu wako na maoni tofauti kabisa juu ya Yesu. Wamoja wanasema, “Yeye ni mutu muzuri.” Wengine wanasema: “Hapana. Anapotosha watu.” (Yohana 7:12) Mazungumuzo hayo ya chini-chini yanafanyika siku za kwanza-kwanza za sikukuu hiyo. Hata hivyo, hakuna ule mwenye iko na ujasiri wa kumusemea Yesu mbele ya watu wengi kwa sababu watu wengi wanaogopa namna viongozi Wayahudi watatenda.

Katikati ya sikukuu, Yesu anaingia katika hekalu. Watu wengi wanashangazwa na uwezo wake wa ajabu wa kufundisha. Hajasomaka hata siku moja masomo ya kirabi, kwa hiyo, Wayahudi wanaulizana hivi: “Namna gani mutu huyu alijua hivi Maandiko, ijapokuwa hakusoma kwenye masomo?”—Yohana 7:15.

Yesu anaeleza hivi: “Mambo yenye ninafundisha haiko yangu, lakini ni ya ule mwenye alinituma. Kama mutu yeyote anatamani kufanya mapenzi Yake, atajua ikiwa mafundisho haya yanatoka kwa Mungu ao ninasema mambo yenye nilijitungia.” (Yohana 7:16, 17) Mafundisho ya Yesu yanapatana na Sheria ya Mungu, kwa hiyo, ni wazi kabisa kwamba anapenda utukufu umuendee Mungu, haiko yeye.

Kisha Yesu anawaambia hivi: “Musa aliwapatia Sheria, haiko vile? Lakini hakuna hata mumoja wenu mwenye anatii Sheria. Sababu gani munatafuta kuniua?” Inawezekana wamoja kati ya watu hao ni wageni kutoka inje ya muji, wenye hawajue kama watu wako wanatafuta kumuua Yesu. Wanaona kuwa hakuna sababu hata moja ya kuua mwalimu kama huyo. Kwa hiyo, wanawaza kuwa Yesu amevurugika ndiyo sababu anasema hivyo. Wanasema hivi: “Uko na pepo muchafu. Ni nani anatafuta kukuua?”—Yohana 7:19, 20.

Kwa kweli, mwaka moja na nusu mbele ya hapo, viongozi Wayahudi walipenda kumuua Yesu kisha yeye kuponyesha mwanaume mumoja siku ya Sabato. Sasa Yesu anazungumuza nao kwa njia yenye kuwafanya wafikiri na anaonyesha waziwazi kuwa ni watu wenye hawana usawaziko. Anawakumbusha kwamba chini ya Sheria, mutoto mwanaume alipaswa kutahiriwa siku ya munane, hata kama ni siku ya Sabato. Kisha anawauliza: “Kama mutu anatahiriwa siku ya sabato ili Sheria ya Musa isivunjwe, je, ninyi munanikasirikia sana kwa sababu nilifanya mutu apone kabisa siku ya sabato? Muache kuhukumu kulingana na namna mutu anaonekana kwa inje, lakini muhukumu kwa hukumu yenye kuwa sawa.”—Yohana 7:23, 24.

Watu wa Yerusalemu wenye wanajua hali hiyo wanasema hivi: “Huyu ndiye mutu mwenye [watawala] wanatafuta kuua, haiko vile? Lakini muone! anazungumuza mbele ya watu, na hawamuambie jambo lolote. Je, watawala wamejua kwa hakika kwamba huyu ndiye Kristo?” Sasa, sababu gani watu hawaamini kuwa Yesu ndiye Kristo? Wanasema hivi: “Tunajua mutu huyu ametoka wapi; lakini wakati Kristo atakuja, hakuna mutu mwenye atajua alitoka wapi.”—Yohana 7:25-27.

Palepale katika hekalu, Yesu anawajibu hivi: “Ninyi munanijua na munajua nilitoka wapi. Na mimi sikukuja kwa uamuzi wangu mwenyewe, lakini Ule mwenye alinituma ni wa kweli, na ninyi hamumujue. Mimi ninamujua, kwa sababu mimi ni muwakilishi kutoka kwake, na Yeye alinituma.” (Yohana 7:28, 29) Wakati wanasikia hivyo, wanajaribu kumukamata Yesu, ili kumutia katika gereza ao kumuua. Hata hivyo, wanashindwa kwa sababu wakati haujafika ili Yesu akufe.

Lakini, watu wengi wanakuwa kabisa na imani katika yeye. Alitembea juu ya maji, alituliza upepo, alikulisha maelfu ya watu kwa njia ya muujiza kwa kutumia mikate kidogo na samaki wadogo, aliponyesha wagonjwa, aliponyesha vilema, alifungua macho ya vipofu, aliponyesha wenye ukoma, na hata alifufua wafu. Kwa kweli, wako na sababu ya kuuliza hivi: “Wakati Kristo atakuja, hatafanya alama nyingi kuliko zenye mutu huyu amefanya, haiko vile?”—Yohana 7:31.

Wakati Wafarisayo wanasikia watu wanasema hivyo, wao pamoja na wakubwa wa makuhani wanatuma walinzi ili wamukamate Yesu.