Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 71

Wafarisayo Wanauliza Maulizo Mwanaume Mwenye Alikuwa Kipofu

Wafarisayo Wanauliza Maulizo Mwanaume Mwenye Alikuwa Kipofu

YOHANA 9:19-41

  • WAFARISAYO WANAULIZA MAULIZO MWANAUME MWENYE ALIKUWA KIPOFU

  • VIONGOZI WA DINI NI “VIPOFU”

Wafarisayo hawaamini kuwa Yesu aliponyesha mutu mwenye alikuwa kipofu tangu kuzaliwa kwake, kwa hiyo, wanaita wazazi wake. Wazazi hao wanajua kuwa hilo linaweza kufanya ‘wafukuzwe katika sinagogi.’ (Yohana 9:22) Ikiwa wangetengwa na Wayahudi wengine, familia ingepata magumu makubwa katika uhusiano wao pamoja na watu wengine na katika hali yao ya feza.

Wafarisayo wanauliza maulizo mbili: “Je, huyu ndiye mwana wenu mwenye munasema alizaliwa kipofu? Basi, namna gani sasa anaona?” Wazazi wanajibu hivi: “Tunajua kama huyu ni mwana wetu na kwamba alizaliwa kipofu. Lakini namna gani anaona sasa, hatujue; ao ni nani alimufungua macho, hatujue.” Hata kama mutoto wao aliwaambia mambo yenye yalitokea, wazazi hao wako waangalifu katika namna yao ya kujibu. Wanasema hivi: “Mumuulize. Ni mutu muzima. Anapaswa kujisemea yeye mwenyewe.”—Yohana 9:19-21.

Kwa hiyo, Wafarisayo wanaita tena mwanaume huyo na kuanza kumuogopesha kwa kumuambia kuwa wanajua kweli kumuhusu Yesu. Wanamuambia hivi: “Patia Mungu utukufu; tunajua kwamba mutu huyu ni mutenda-zambi.” Mwanaume huyo mwenye alikuwa kipofu anaepuka shitaka lao kwa kusema hivi: “Kama yeye ni mutenda-zambi, mimi sijue.” Hata hivyo, anasema hivi: “Jambo moja lenye ninajua ni kwamba nilikuwa kipofu, lakini sasa ninaona.”—Yohana 9:24, 25.

Wafarisayo hawapendi kuachia mambo pale, kwa hiyo wanaendelea kumuuliza: “Alikufanyia nini? Namna gani alifungua macho yako?” Mwanaume huyo anaonyesha ujasiri kwa kujibu: “Nimekwisha kuwaambia, lakini hamukusikiliza. Sababu gani munataka kusikia tena jambo hilo? Ninyi pia munataka kuwa wanafunzi wake?” Wafarisayo wanakasirika sana, na kuambia mwanaume huyo: “Wewe ni mwanafunzi wa mutu huyo, lakini sisi ni wanafunzi wa Musa. Tunajua kama Mungu alisema na Musa; lakini mutu huyu, hatujue alitoka wapi.”—Yohana 9:26-29.

Mutu huyo mwenye kuomba-omba anashangaa na kusema: “Hakika hili ni jambo lenye kushangaza, kwamba hamujue alitoka wapi, ijapokuwa alifungua macho yangu.” Mwanaume huyo anatoa mawazo yenye kupatana na akili kuhusu mutu mwenye Mungu anasikiliza na kukubali. Anasema: “Tunajua kuwa Mungu hasikilize watenda-zambi, lakini kama mutu yeyote anamuogopa Mungu na kufanya mapenzi yake, yeye anamusikiliza mutu huyo. Tangu zamani haijasikiwa hata siku moja kuwa mutu fulani amefungua macho ya mutu mwenye alizaliwa kipofu.” Hilo linafanya mwanaume huyo amalizie kwa kusema: “Kama mutu huyo hakutoka kwa Mungu, hangefanya jambo lolote hata kidogo.”—Yohana 9:30-33.

Wafarisayo wanashindwa kupinga maneno ya mutu huyo mwenye kuomba-omba. Kwa hiyo, wanamutukana kwa kusema: “Wee wote ulizaliwa katika zambi, na sasa je, unatufundisha sisi?” Na wanamutupa inje.—Yohana 9:34.

Wakati Yesu anasikia mambo yenye yalitokea, anamupata mwanaume huyo na kumuuliza: “Je, unaamini Mwana wa binadamu?” Mwanaume huyo mwenye aliponyeshwa anajibu hivi: “Na huyo ni nani, Bwana, ili nimuamini?” Bila kuacha mashaka yoyote, Yesu anamuambia hivi: “Umemuona, na kwa kweli, yeye ndiye anasema na wewe.”—Yohana 9:35-37.

Mwanaume huyo anajibu hivi: “Ninamuamini, Bwana.” Pia, anaonyesha imani na heshima kwa kuinama mbele ya Yesu. Na Yesu anasema maneno haya yenye kuwa na maana kubwa: “Nilikuja katika ulimwengu huu kwa ajili ya hukumu hii, ili wale wenye hawaone waweze kuona na wale wenye wanaona wakuwe vipofu.”—Yohana 9:38, 39.

Wafarisayo, wenye wako hapo, wanajua kuwa hawako vipofu. Lakini tuseme nini juu ya daraka lao lenye wamejipatia la kuwa viongozi wa kiroho? Ili kujitetea, wanauliza hivi: “Je, sisi pia ni vipofu?” Yesu anawajibu hivi: “Kama mungekuwa vipofu, hamungekuwa na zambi. Lakini sasa munasema, ‘Tunaona.’ Zambi yenu inabakia.” (Yohana 9:40, 41) Kama hawangekuwa walimu katika Israeli, ingeeleweka kuwa wanamukataa Yesu kuwa Masiya. Lakini, kwa kuwa ni watu wenye kujua Sheria, kumukataa Yesu ni zambi nzito kwao.