Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 89

Anafundisha Katika Perea Wakati Iko Anaenda Yudea

Anafundisha Katika Perea Wakati Iko Anaenda Yudea

LUKA 17:1-10 YOHANA 11:1-16

  • KUKWAZA MUTU NI JAMBO NZITO

  • UKUWE MWENYE KUSAMEHE NA UONYESHE IMANI

Kwa wakati fulani, Yesu amekuwa “upande mwingine wa Yordani” katika eneo lenye kuitwa Perea. (Yohana 10:40) Anaenda sasa sehemu ya kusini kuelekea Yerusalemu.

Yesu haiko peke yake. Wanafunzi wake wanasafiri pamoja naye, na pia “watu wengi sana,” kutia ndani wakusanya-kodi na watenda-zambi. (Luka 14:25; 15:1) Wafarisayo na waandishi wenye kulaumu maneno na matendo ya Yesu, wako pia pale. Wako na mambo mengi ya kufikiria kisha kusikiliza mifano ya Yesu kuhusu kondoo mwenye alipotea, mutoto mwenye alipotea, na mufano wa tajiri na Lazaro.—Luka 15:2; 16:14.

Pengine, akikumbuka maneno yenye kulaumu na zarau ya viongozi wa dini, Yesu anakazia uangalifu wake kwa wanafunzi wake. Anagusia mambo yenye alikuwa amefundisha kule Galilaya.

Kwa mufano Yesu anasema: “Lazima mambo yenye kuleta vikwazo yakuje. Lakini, ole kwa mutu mwenye yatakuja kupitia yeye! . . . Mujiangalie ninyi wenyewe. Kama ndugu yako anatenda zambi, umukemee, na kama anatubu, umusamehe. Hata kama anakutendea zambi mara saba (7) kwa siku, na anarudia kwako mara saba (7), akisema, ‘Ninatubu,’ unapaswa kumusamehe.” (Luka 17:1-4) Pengine maelezo hayo ya mwisho yanakumbusha Petro ulizo lenye aliuliza kuhusu kusamehe mupaka mara saba.—Matayo 18:21.

Je, wanafunzi wataweza kutenda kulingana na maneno ya Yesu? Wakati wanamuambia Yesu, “Utupatie imani zaidi,” anawahakikishia hivi: “Kama mungekuwa na imani yenye ukubwa wa mbegu ya haradali, mungeambia muti huu wa muforsadi mweusi, ‘Ongoka na upandwe katika bahari!’ na ungewatii.” (Luka 17:5, 6) Ndiyo, hata imani kidogo inaweza kutimiza mambo makubwa.

Yesu anaendelea kufundisha kuwa ni jambo la maana kuwa munyenyekevu na kuwa na mawazo yenye usawaziko kuhusu mutu yeye mwenyewe, kwa kuambia mitume hivi: “Ni nani kati yenu mwenye kama iko na mutumwa mwenye kulima ao mwenye kuchunga wanyama, anaweza kumuambia wakati anarudia kutoka katika shamba, ‘Kuja hapa mara moja na ukule kwenye meza’? Lakini, je, hatamuambia, ‘Nitayarishie chakula changu cha mangaribi, na uvae aproni na unitumikie mupaka nimalize kula na kunywa, na kisha unaweza kula na kunywa’? Hatashukuru mutumwa huyo kwa sababu alifanya mambo yenye aliombwa afanye, haiko vile? Vilevile, wakati mumefanya mambo yote yenye muliombwa kufanya, museme: ‘Sisi ni watumwa wenye hawana mafaa yoyote. Mambo yenye tumefanya ni yale tulipaswa kufanya.’”—Luka 17:7-10.

Kila mutumishi wa Mungu anapaswa kuelewa kwamba ni jambo la maana kutia ibada yetu kwa Mungu pa nafasi ya kwanza. Zaidi ya hilo, kila mutu anapaswa kukumbuka pendeleo lenye iko nalo la kumuabudu Mungu kama mutu wa nyumba yake.

Inaonekana kwamba kisha tu hapo, mujumbe mwenye alitumwa na Maria na Marta anafika. Maria na Marta ni dada za Lazaro, na wanaishi kule Betania ya Yudea. Mujumbe huyo anasema hivi: “Bwana, ona! ule mwenye unamupenda sana ni mugonjwa.”—Yohana 11:1-3.

Hata kama anapata habari kwamba rafiki yake Lazaro ni mugonjwa sana, huzuni haimuregeze kabisa Yesu. Lakini, anasema: “Kusudi la ugonjwa huu haiko kuleta kifo, lakini ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu atukuzwe kupitia huo.” Anafanya pale siku mbili, kisha anaambia wanafunzi wake: “Tuende tena Yudea.” Hawafurahie jambo hilo na kumuambia hivi: “Rabi, juzijuzi tu Wayudea walikuwa wanatafuta kukupiga majiwe, na je, unaenda tena kule?”—Yohana 11:4, 7, 8.

Yesu anajibu: “Kuko saa kumi na mbili (12) za muchana, haiko vile? Kama mutu anatembea muchana, hajikwae kwenye kitu, kwa sababu anaona mwangaza wa ulimwengu huu. Lakini kama mutu yeyote anatembea usiku, anajikwaa, kwa sababu mwangaza hauko ndani yake.” (Yohana 11:9, 10) Pengine anapenda kusema kwamba, wakati wa utumishi wenye Mungu alimuwekea haujamalizika. Mbele umalizike, Yesu anapaswa kutumia wakati wake mufupi wenye anabakia nao mupaka mwisho.

Yesu anaongeza: “Rafiki yetu Lazaro amelala usingizi, lakini ninasafiri kuenda kule ili kumuamusha.” Pengine wanawaza kama Lazaro anapumuzika tu na kwamba atapona, wanafunzi wanasema: “Bwana, kama amelala usingizi, atapona.” Yesu anawaambia hivi waziwazi: “Lazaro amekufa. . . . Lakini tuende kumuona.”—Yohana 11:11-15.

Tomasi anajua kama Yesu anaweza kuuawa kule Yudea, lakini anataka kumuunga mukono, kwa hiyo anawaambia wanafunzi wenzake hivi: “Sisi pia tuende, ili tukufe pamoja naye.”—Yohana 11:16.