Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 84

Kuwa Mwanafunzi wa Yesu Ni Daraka Nzito

Kuwa Mwanafunzi wa Yesu Ni Daraka Nzito

LUKA 14:25-35

  • DARAKA LA KUWA MWANAFUNZI WA YESU

Yesu amefundisha mambo ya maana wakati alikuwa anakula chakula kwenye nyumba ya kiongozi mumoja wa Wafarisayo. Wakati Yesu anaendelea na safari yake ya kuenda Yerusalemu, watu wengi sana wanasafiri pamoja naye. Sababu gani? Je, wako kabisa tayari kuwa wanafunzi wake wa kweli hata kama hilo linaomba nini?

Wakati wako katika safari, Yesu anawaambia jambo fulani lenye pengine linaweza kukwaza wamoja kati yao. Anasema hivi: “Kama mutu yeyote anakuja kwangu na hachukie baba yake, mama yake, bibi yake, watoto wake, ndugu na dada zake, ndiyo, hata uzima wake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.” (Luka 14:26) Lakini, anataka kusema nini wakati anasema hivyo?

Yesu haiko anataka kusema kama wale wenye wanakuwa wafuasi wake wanapaswa kabisa-kabisa kuchukia watu wa jamaa yao. Lakini, iko anapenda kusema kuwa wanapaswa kuwachukia katika maana ya kwamba wanapaswa kuwaonyesha upendo kidogo kuliko ule wenye wanaonyesha Yesu, ni kusema, hawapaswe kuwa kama ule mwanaume katika mufano wa Yesu mwenye alikataa mwaliko wa maana kwa sababu tu ametoka kuoa. (Luka 14:20) Biblia inasema kuwa Yakobo, babu ya Wayahudi, alichukia Lea na kupenda Raheli, maana yake, upendo wenye Yakobo alikuwa nao kwa Lea ulikuwa wa kidogo kuliko ule wenye alikuwa nao kwa Raheli.—Mwanzo 29:31.

Ona kwamba Yesu anasema kuwa mwanafunzi anapaswa kuchukia “hata uzima wake mwenyewe,” ao nafsi yake. Ni kusema kama, mwanafunzi wa kweli anapaswa kumupenda Yesu kuliko vile anapenda uzima wake; anapaswa kuwa tayari kupoteza uzima wake ikiwa inaomba hivyo. Ni wazi kwamba, kuwa mwanafunzi wa Kristo ni daraka nzito. Haiko uamuzi wa kukamata hivihivi tu, bila kufikiri kwa uangalifu.

Mwanafunzi anapaswa kujua kuwa daraka hilo linaweza kumufanya akuwe katika magumu, na kuteswa; kwa sababu Yesu anasema hivi: “Kila mutu mwenye habebe muti wake wa mateso na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu.” (Luka 14:27) Ndiyo, mwanafunzi wa kweli wa Yesu anapaswa kuwa tayari kuteswa, kama vile pia Yesu aliteswa. Yesu alisema hata kama atakufa katika mikono ya maadui wake.

Kwa hiyo, watu fulani kati ya wale wenye kusafiri pamoja na Yesu wako na lazima ya kuchunguza kwa uangalifu mambo yenye yanaombwa ili kuwa mwanafunzi wa Kristo. Yesu anatoa mufano ili kukazia jambo hilo. Anasema hivi: “Kwa mufano, ni nani kati yenu mwenye akitaka kujenga munara hakae kwanza na kuhesabia garama, ili aone kama iko na kiasi cha kutosha kuumaliza? Kama hafanye vile, anaweza kuweka musingi lakini anashindwa kumaliza munara.” (Luka 14:28, 29) Kwa hiyo, mbele ya kuwa wanafunzi wa Yesu, wale wenye wako wanasafiri pamoja naye ili kuenda Yerusalemu walipaswa kuwa wameazimia kabisa kutimiza daraka hilo. Yesu anatumia mufano mwengine ili kukazia jambo hilo:

“Ni mufalme gani mwenye kuwa na maaskari elfu kumi (10 000) mwenye anaenda kukutana katika vita na mufalme mwingine, ambaye hakae kwanza na kufanya shauri aone kama ataweza kupata ushindi juu ya ule mwenye anakuja kupigana naye akiwa na maaskari elfu makumi mbili (20 000)? Ikiwa kwa kweli hawezi kupata ushindi juu yake, basi wakati ule mufalme mwingine angali mbali, yeye anatuma baraza la mabalozi na kuomba amani.” Ili kukazia wazo lake, Yesu anasema hivi: “Vilevile, mukuwe hakika kwamba, hakuna hata mumoja wenu mwenye anaweza kuwa mwanafunzi wangu kama haachane na vitu vyake vyote.”—Luka 14:31-33.

Bila shaka, Yesu haiko anazungumuzia tu wale wenye wako wanamufuata kwenye barabara. Wote wenye wanafikia kumujua Kristo wanapaswa kuwa tayari kufanya mambo yenye iko anasema hapa. Maana yake nini? Ni kusema, wanapaswa kuwa tayari kuachana na kila kitu chenye wako nacho—mali yao, hata uzima wao—ikiwa wanapenda kuwa wanafunzi wake. Wanapaswa kufikiri na kusali kwa ajili ya jambo hilo.

Sasa Yesu anazungumuzia jambo lenye alizungumuzia kwenye Mahubiri ya Mulimani wakati alisema kuwa wanafunzi wake ni “chumvi ya dunia.” (Matayo 5:13) Inawezekana alitaka kusema kuwa kama vile chumvi inalinda kitu kisioze, wanafunzi wake wanaweza kusaidia watu ili hali yao ya kiroho na mwenendo wao visiharibike. Sasa, kadiri utumishi wake unakaribia mwisho, Yesu anasema hivi: “Kwa kweli chumvi ni ya muzuri. Lakini chumvi ikipoteza nguvu yake, itakolezwa na nini?” (Luka 14:34) Wasikilizaji wake wanajua kuwa chumvi fulani yenye ilipatikana wakati huo haikuwa safi. Ilichangana na udongo na kwa hiyo haikuwa na mafaa.

Kwa hiyo, Yesu iko anaonyesha kuwa hata wale wenye wamekuwa wanafunzi wake tangu zamani hawapaswe kuregeza musimamo wao. Ikiwa jambo hilo lingetokea, hawangekuwa na faida yoyote, kama vile chumvi yenye imepoteza nguvu yake. Ulimwengu ungefikia kuwazarau. Zaidi ya hilo, hawangekuwa na mafaa mbele ya Mungu, na wangefikia hata kuchafua jina lake. Yesu anaonyesha sababu gani tunapaswa kuepuka jambo hilo litufikie. Anasema hivi: “Ule mwenye kuwa na masikio ya kusikiliza, asikilize.”—Luka 14:35.