Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 86

Mutoto Mwenye Alipotea Anarudia

Mutoto Mwenye Alipotea Anarudia

LUKA 15:11-32

  • MUFANO WA MUTOTO MWENYE ALIPOTEA

Inawezekana Yesu angali katika Perea, mashariki mwa Muto Yordani. Ametoka kutoa mufano wa kondoo na wa feza ya kichele ya drakma yenye ilipotea. Mifano yote mbili hiyo inatufundisha kwamba tunapaswa kufurahi wakati mutenda-zambi anatubu na kumurudilia Mungu. Wafarisayo na waandishi wamekuwa wakimulaumu Yesu kwa sababu anakaribisha watu kama hao. Lakini, mifano hiyo miwili ya Yesu inawafundisha Wafarisayo na waandishi jambo fulani? Wanaelewa namna Baba yetu wa mbinguni anajisikia wakati watenda-zambi wanatubu? Yesu anatoa sasa mufano wenye kugusa moyo wenye kukazia somo hilohilo la maana.

Mufano huo unahusu baba mwenye kuwa na watoto wawili. Mwenye kuzungumuziwa sana katika mufano huu ni mutoto wake mudogo. Wafarisayo na waandishi, na pia watu wengine wenye kumusikiliza Yesu wanapaswa kujifunza somo fulani kupitia mutoto huyo. Lakini, mambo yenye Yesu anasema kuhusu baba na mutoto wake mukubwa ni ya maana, kwa sababu namna wanatenda inaweza pia kutufundisha jambo fulani. Kwa hiyo fikiria watu hao watatu wakati Yesu anatoa mufano huu:

“Mutu fulani alikuwa na wana wawili. Na ule mudogo akamuambia baba yake, ‘Baba, nipatie sehemu ya mali yenye ni fungu langu.’ Basi akawagawia mali yake.” (Luka 15:11, 12) Ona kwamba ule mwana mudogo haombe uriti kwa sababu baba yake amekufa. Baba yake angali muzima. Lakini mutoto huyo anataka kupata sehemu yake sasa ili akuwe huru na kuitumia vile anapenda. Mutoto huyo anafanya nini?

Yesu anaeleza: “Kisha siku kidogo, ule mwana mudogo akakusanya pamoja vitu vyake vyote na akasafiri kuenda inchi ya mbali, na akiwa kule akatumia mubaya mali yake kwa kuishi maisha ya upotovu.” (Luka 15:13) Kuliko kubakia nyumbani kwenye kuwa usalama, pamoja na baba mwenye kuhangaikia na kutunza muzuri watoto wake, mutoto huyu anahamia katika inchi ingine. Katika inchi hiyo, anaharibu uriti wake kwa kuishi maisha ya raha, na ya uasherati. Kisha anaanza kuteseka, kama vile Yesu anaendelea kusema:

“Wakati alikuwa ametumia kila kitu, njaa kali ikatokea katika inchi hiyo yote, na akakuwa na uhitaji. Hata akaenda na kushikamana na raia mumoja wa inchi hiyo, mwenye alimutuma katika mashamba yake ili achunge nguruwe. Na alitamani kujishibisha na maganda ya karuba yenye nguruwe hao walikuwa wanakula, lakini hakuna mutu mwenye alikuwa anamupatia kitu.”—Luka 15:14-16.

Kulingana na Sheria ya Mungu, nguruwe ni munyama muchafu, lakini mutoto huyu analazimika kutumika kama muchungaji wa nguruwe. Anasikia njaa sana, yenye inamufanya atamani kula chakula chenye kwa kawaida, ni wanyama tu ndio wanapaswa kula, ni kusema, nguruwe wenye iko anachunga. Katika hali hiyo ya mateso na ya kukosa tumaini, ‘anarudiwa na fahamu zake.’ Anafanya nini? Anajiambia hivi: “Baba yangu iko na wafanyakazi wengi na wako na mukate wa kutosha, lakini hapa mimi ninakufa na njaa! Nitaondoka na kusafiri kuenda kwa baba yangu na kumuambia: “Baba, nimetenda zambi juu ya mbingu na juu yako. Sistahili tena kuitwa mwana wako. Unifanye kama mumoja wa wafanyakazi wako.’” Kisha anaondoka na kuenda kwa baba yake.—Luka 15:17-20.

Baba yake atatenda namna gani? Atamukasirikia na kumufokea kwa sababu ya upumbavu wake wa kuondoka nyumbani? Baba huyo atamutendea mubaya na kukataa kumukaribisha? Kama ingekuwa wewe, ungetenda namna gani? Ikiwa mutoto wako mwanaume ao mwanamuke ndiye alifanya hivyo ungefanya nini?

MUTOTO MWENYE ALIPOTEA ANAPATIKANA

Yesu anaeleza vile baba anajisikia na vile anatenda: “Wakati [mwana] alikuwa angali mbali, baba yake akamuona na akamusikilia huruma, akamukimbilia, akamukumbatia kwa upole wote na kumubusu.” (Luka 15:20) Hata kama baba amesikia namna mutoto wake alijitia katika maisha ya mubaya sana, anamukaribisha. Viongozi Wayahudi wanasema kuwa wanamujua Yehova na kumuabudu. Je, wanaelewa kupitia mufano huu namna Baba yetu wa mbinguni anajisikia wakati watenda-zambi wanatubu? Je, watatambua kwamba Yesu amekuwa akionyesha roho hiyohiyo ya ukaribishaji?

Bila shaka baba huyo mwenye utambuzi, kupitia uso wenye huzuni wa mutoto wake anatambua kwamba ni mwenye kutubu. Tena, hatua ya kwanza ya upendo yenye baba anafanya ya kumupokea, inafanya ikuwe mwepesi kwa mutoto wake kuungama zambi zake. Yesu anaeleza: “Kisha ule mwana akamuambia, ‘Baba, nimetenda zambi juu ya mbingu na juu yako. Sistahili tena kuitwa mwana wako.’”—Luka 15:21.

Baba anatolea watumwa wake amri hii: “Haraka! mulete kanzu ya muzuri zaidi na mumuvalishe, na mutie pete kwenye mukono wake na viatu kwenye miguu yake. Mulete pia kitoto-dume cha ngombe chenye kunona, mukichinje, tukule na tufurahi, kwa maana huyu mwana wangu alikuwa amekufa lakini amekuwa muzima tena; alikuwa amepotea na amepatikana.” Kisha wanaanza “kujifurahisha.”—Luka 15:22-24.

Wakati huo, mutoto mukubwa wa baba huyo iko katika shamba. Yesu anasema hivi kumuhusu: “Wakati alikuwa anarudia na kukaribia nyumba, akasikia sauti ya muziki na dansi. Basi akaita mutumishi mumoja na kumuuliza kama kuko nini. Akamuambia, ‘Ndugu yako amerudia, na baba yako amechinja kitoto-dume cha ngombe chenye kunona kwa sababu alimupata tena akiwa na afya ya muzuri.’ Lakini akakasirika na akakataa kuingia ndani. Basi baba yake akatoka inje na akaanza kumubembeleza. Akamuambia baba yake, ‘Angalia! Nimekutumikia kwa miaka mingi na hakuna siku nilivunja amri yako hata moja, lakini haujanipatia hata siku moja mbuzi mudogo ili nifurahi pamoja na marafiki wangu. Lakini wakati tu huyu mwana wako amefika, mwenye alitumia mubaya mali yako pamoja na makahaba, umemuchinjia kitoto-dume cha ngombe chenye kunona.’”—Luka 15:25-30.

Kama ule mutoto mukubwa, ni nani wenye wamekuwa wakilaumu rehema na hali ya kuhangaikia watu yenye Yesu alionyesha watu wa kawaida na watenda-zambi? Ni waandishi na Wafarisayo. Hali yao ya kumulaumu Yesu kwa sababu amekuwa akikaribisha watenda-zambi ndiyo imefanya atoe mufano huu. Bila shaka, kila mutu mwenye kulaumu Mungu kwa sababu anaonyesha rehema, anapaswa kuchukua mufano huu kwa uzito.

Yesu anamalizia mufano wake kwa kueleza jambo lenye baba huyo alimuambia mutoto wake mukubwa: “Mwana wangu, umekuwa pamoja na mimi sikuzote, na mali yangu yote ni yako. Hata hivyo iliomba tufurahi na kushangilia, kwa maana ndugu yako alikuwa amekufa lakini amekuwa muzima tena; alikuwa amepotea na amepatikana.”—Luka 15:31, 32.

Yesu haonyeshe jambo lenye ule mutoto mukubwa anafanya kisha hapo. Lakini, kisha kifo na ufufuo wa Yesu, “makuhani wengi sana wakaanza kutii imani.” (Matendo 6:7) Pengine kati yao kulikuwa watu fulani wenye walimusikia Yesu akizungumuzia mufano huo wenye kugusa moyo kuhusu mutoto mwenye alipotea. Ndiyo, walikuwa hata na nafasi ya kurudiwa na akili, kutubu, na kumurudilia Mungu.

Tangu siku hiyo, wanafunzi wa Yesu wanaweza na wanapaswa kujifunza mambo ya lazima kupitia mufano huu muzuri. Jambo la kwanza ni kwamba, kuliko kuenda huku na huku ili kutafuta raha katika “inchi ya mbali,” ni jambo la hekima kabisa kubakia katika usalama wenye kuwa kati ya watu wa Mungu, chini ya ulinzi wa Baba yetu mwenye kutupenda na mwenye kututimizia mahitaji yetu.

Jambo lingine lenye tunaweza kujifunza ni kwamba ikiwa yeyote kati yetu anaacha njia ya Mungu, anapaswa kurudia kwa unyenyekevu kwa Baba yetu ili akubaliwe tena naye.

Jambo lingine lenye tunaweza tena kujifunza linaonekana kupitia tofauti kati ya namna baba huyo na mutoto wake mukubwa walitenda. Baba alikuwa tayari kukaribisha na kusamehe mutoto wake, lakini ule mutoto wake mukubwa aliweka kinyongo na kukataa kumukaribisha ndugu yake. Ni wazi kwamba, watumishi wa Mungu wanapaswa kuwa tayari kusamehe na kukaribisha mutu mwenye alikuwa amepotea lakini anatubu kikweli na kurudia kwenye ‘nyumba ya Baba.’ Tuendelee basi kufurahi kwamba ndugu yetu mwenye ‘alikuwa amekufa iko muzima tena’ na kwamba mwenye ‘alikuwa amepotea amepatikana.’