Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 87

Tumia Hekima Yenye Kutenda kwa Kupanga Mambo Mbele ya Wakati

Tumia Hekima Yenye Kutenda kwa Kupanga Mambo Mbele ya Wakati

LUKA 16:1-13

  • MUFANO KUHUSU MUSIMAMIZI-NYUMBA MWENYE HAIKO MWAMINIFU

  • “MUJIFANYIE MARAFIKI” KUPITIA MALI ZENU

Mufano wenye Yesu anatoka tu kuzungumuzia kuhusu mwana mupotevu, unapaswa kuwa umewafundisha wakusanya-kodi, waandishi na Wafarisayo wenye wameusikiliza, kwamba Mungu iko tayari kusamehe watenda-zambi wenye kutubu. (Luka 15:1-7, 11) Yesu anazungumuza sasa na wanafunzi wake. Anatumia mufano mwengine, mara hii ni kuhusu mutu tajiri mwenye anapata habari kama musimamizi-nyumba wake hatumike muzuri.

Yesu anaeleza kama musimamizi nyumba ameshitakiwa kuwa ametumia mubaya mali ya bwana wake. Kwa hiyo, bwana anasema kama musimizi-nyumba huyo atafukuzwa. Musimamizi-nyumba anajiuliza: “Nitafanya nini, kwa kuwa bwana wangu ananitosha kwenye kazi ya usimamizi? Sina nguvu za kulima, na ninasikia haya kuombaomba.” Kwa hiyo anasema hivi: “Aha! Ninajua kile nitafanya, ili wakati nitatoshwa kwenye kazi ya usimamizi, watu wanikaribishe katika nyumba zao.” Mara moja anaita wale wenye kuwa na madeni, anawauliza: “Uko na deni la ngapi la bwana wangu?”—Luka 16:3-5.

Wa kwanza anajibu: “Vipimo mia moja (100) vya mafuta ya zeituni.” Hiyo ni kama litre 2 200 ya mafuta. Pengine mutu huyo mwenye alijikopesha alikuwa na shamba kubwa la mizeituni ao alikuwa mufanya-biashara mwenye aliuzisha mafuta. Musimamizi-nyumba anamuambia: “Kamata cheti chako cha mapatano, ukae na uandike haraka makumi tano (50) [litre 1 100].”—Luka 16:6.

Musimamizi-nyumba huyo anamuuliza mwengine: “Na wewe, uko na deni la ngapi?” Anajibu: “Vipimo vikubwa mia moja (100) vya ngano.” Ni kama litre 22 000. Musimamizi-nyumba anamuambia ule mwenye deni: “Kamata cheti chako cha mapatano uandike makumi munane (80).” Kwa hiyo anamupunguzia deni kwa asilimia 20 (20%).—Luka 16:7.

Musimamizi-nyumba huyo angali anasimamia mambo ya feza ya bwana wake, kwa hiyo kwa upande fulani iko na mamlaka ya kuamua kupunguza madeni yenye watu wako nayo kwa bwana wake. Kwa kupunguza madeni yao, musimamizi huyo anajifanyia marafiki na watu wenye wanaweza kumutendea mema kisha kufukuzwa kwenye kazi.

Kisha wakati kupita, bwana wake anatambua jambo lenye lilitokea. Hata kama jambo hilo lilifanya apoteze mali yake, anafurahishwa na musimamizi-nyumba huyo na kumupongeza kwa sababu “alitumia hekima yenye kutenda, hata kama hakukuwa anafanya mambo yenye kuwa sawa.” Yesu anaongeza: “Wana wa mupangilio huu wa mambo wanajua namna ya kutendea watu wa kizazi chao kwa hekima zaidi kuliko wana wa mwangaza.”—Luka 16:8.

Yesu haunge mukono njia yenye musimamizi-nyumba ametumia, wala hatie moyo kufanya biashara yenye udanganyifu. Kwa hiyo basi, anapenda kufundisha nini? Anashauria wanafunzi wake hivi: “Mujifanyie marafiki kupitia mali zenye kupatikana katika njia yenye haiko sawa, ili wakati zitaisha, wawapokee katika makao ya milele.” (Luka 16:9) Ndiyo kuko somo hapa kuhusu kuona mbali na kutumia hekima yenye kutenda. “Wana wa mwangaza,” ni kusema, watumishi wa Mungu, wanapaswa kutumia vitu vyao vya kimwili kwa hekima, wakifikiri kuhusu wakati wenye kuja wa milele.

Ni Yehova na Mwana wake tu ndio wanaweza kupokea mutu katika Ufalme wa mbinguni ao katika Paradiso duniani. Tunapaswa kukomalisha kwa bidii urafiki pamoja nao kwa kutumia mali yetu ya kimwili ili kuunga mukono faida za Ufalme. Wakati wetu wenye kuja wa milele utakuwa salama wakati zahabu, feza, na utajiri mwengine wa kimwili hautakuwa na kazi tena na utaharibishwa.

Yesu anasema tena kwamba wale wenye kutunza na kutumia kwa uaminifu mali zozote ao vitu vyao vya kimwili watakuwa waaminifu katika kutunza vitu vya maana sana. Basi Yesu anasema: “Kwa hiyo, kama ninyi hamukujionyesha kuwa waaminifu kuhusiana na mali zenye kupatikana katika njia yenye haiko sawa, ni nani atawapatia mali ya kweli [kama vile mambo ya Ufalme]?”—Luka 16:11.

Yesu iko anaonyesha wanafunzi wake kwamba wataombwa mambo mengi kama wanapenda wapokelewe “katika makao ya milele.” Mutu hawezi kuwa mutumishi wa kweli wa Mungu na wakati huohuo akuwe mutumwa wa mali ya kimwili yenye haipatane na mambo yenye kuwa sawa. Yesu anamalizia hivi: “Hakuna mutumishi mwenye anaweza kutumikia mabwana wawili, kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine, ao atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kuwa watumwa wa Mungu na wa Utajiri.”—Luka 16:9, 13.