Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 100

Mufano Wake wa Mina Kumi

Mufano Wake wa Mina Kumi

LUKA 19:11-28

  • YESU ANATOA MUFANO WA MINA KUMI

Hata kama Yesu iko anaenda Yerusalemu, inawezekana angali kwa Zakayo pamoja na wanafunzi wake. Wanaamini kwamba “Ufalme wa Mungu” uko karibu kutawala na kwamba Yesu ndiye atakuwa Mufalme wa Ufalme huo. (Luka 19:11) Hawaelewe muzuri jambo hilo, kama vile tu wanashindwa kuelewa kwamba Yesu anapaswa kufa. Kwa hiyo, anawatolea mufano ili kuwasaidia waone kwamba Ufalme ungali mbali.

Anasema: “Mutu fulani wa familia ya kifalme alisafiri kuenda inchi ya mbali ili afanywe kuwa mufalme na kisha arudie.” (Luka 19:12) Safari kama hiyo ilipaswa kuchukua wakati murefu. Bila shaka, Yesu ndiye ule “mutu wa familia ya kifalme” mwenye anasafiri kuenda “inchi ya mbali,” ni kusema, mbinguni, kwenye Baba yake atamupatia mamlaka ya ufalme.

Katika mufano huu, mbele aende, “mutu wa familia ya kifalme” anaita watumwa kumi na anapatia kila mumoja wao mina ya feza, na kuwaambia: “Mufanye nazo biashara mupaka wakati nitakuja.” (Luka 19:13) Mina ya feza iko na samani kubwa. Mina moja inalingana na mushahara wa miezi tatu wa mufanyakazi katika shamba.

Pengine wanafunzi wanatambua kwamba wanafananishwa na watumwa kumi hao wa mufano huo, kwa sababu Yesu amekwisha kuwafananisha na wafanyakazi katika mavuno. (Matayo 9:35-38) Bila shaka hakuwaomba walete mavuno ya nafaka. Lakini, mavuno hayo ni kuleta wanafunzi wengine wenye wanaweza kupata fasi katika Ufalme wa Mungu. Wanafunzi wanatumia kila kitu chenye wako nacho ili kutokeza wariti wengi wa Ufalme.

Yesu anafunua mambo gani mengine katika mufano huu? Anasema kwamba raia “walimuchukia [mutu wa familia ya kifalme] na walituma baraza la mabalozi wamufuate na kusema, ‘Hatutaki mutu huyu akuwe mufalme juu yetu.’” (Luka 19:14) Wanafunzi wanajua kwamba Wayahudi hawamukubali Yesu, na wengine wanataka hata kumuua. Kisha Yesu kufa na kuenda mbinguni, Wayahudi kwa ujumla wanaonyesha namna wanamuona Yesu kwa kutesa wanafunzi wake. Wapinzani hao wanaonyesha waziwazi kwamba hawapendi Yesu akuwe Mufalme.—Yohana 19:15, 16; Matendo 4:13-18; 5:40.

Namna gani wale watumwa kumi, wanatumia mina yao mupaka ule “mutu wa familia ya kifalme” afanywe kuwa “mufalme” na arudie? Yesu anaeleza hivi: “Mwishowe wakati alirudia kisha kupokea ufalme, aliita watumwa wenye alikuwa amepatia feza, ili ajue walipata faida gani kwa kufanya biashara. Basi wa kwanza akakuja na kusema, ‘Bwana, mina yako moja imeleta faida ya mina kumi (10).’ Akamuambia, ‘Umefanya muzuri, mutumwa mwema! Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo ndogo sana, ukuwe na mamlaka juu ya miji kumi (10).’ Kisha wa pili akakuja, na kusema, ‘Bwana, mina yako moja, imeleta faida ya mina tano (5).’ Akamuambia huyo pia, ‘Na wewe ukuwe na mamlaka juu ya miji tano (5).’”—Luka 19:15-19.

Kama wanafunzi wanaelewa kwamba wako kama watumwa wenye walitumia kabisa kila kitu chenye wako nacho ili kufanya wanafunzi wengi zaidi, wanaweza kuendelea kuwa hakika kwamba Yesu atafurahi. Na wanaweza kutumainia kupata zawabu kwa sababu ya bidii ya namna hiyo. Bila shaka, wanafunzi wote wa Yesu hawako katika hali ileile ya maisha, ao hawana nafasi ao uwezo uleule. Lakini Yesu, mwenye alipewa ‘ufalme,’ atatambua na kubariki bidii yao ya kufanya wanafunzi.—Matayo 28:19, 20.

Ona tofauti yenye Yesu anaonyesha wakati anamalizia mufano wake: “Lakini [mutumwa] mwingine akakuja, akisema, ‘Bwana, mina yako ndiyo hii; niliifunga katika kitambaa nikaificha. Unaona, nilikuogopa kwa sababu wewe ni mutu mugumu; unachukua kitu chenye haukuweka akiba, na unavuna kile haukupanda.’ Akamuambia, ‘Ninakuhukumu kwa maneno yako mwenyewe, mutumwa muovu. Ulijua kama mimi ni mutu mugumu, mwenye kuchukua kitu chenye sikuweka akiba na kuvuna kitu chenye sikupanda, haiko vile? Basi sababu gani haukutia feza zangu katika banke? Kisha wakati ningekuja, ningezikamata pamoja na faida.’ Kisha akaambia wale wenye walikuwa wanasimama pembeni yake, ‘Mumunyanganye ile mina na muipatie ule mwenye kuwa na mina kumi (10).’”—Luka 19:20-24.

Kwa kushindwa kuongeza mali ya ufalme ya bwana wake, mutumwa huyo anapata shida. Mitume wanangojea kwa hamu wakati Yesu atatawala katika Ufalme wa Mungu. Kwa hiyo kupitia mambo yenye anasema kuhusu mutumwa huyo wa mwisho, pengine wanaelewa kwamba ikiwa hawatumike kwa bidii, hawatapata nafasi katika Ufalme huo.

Maneno ya Yesu yanapaswa kuchochea wanafunzi waaminifu waongeze bidii yao. Anamalizia hivi: “Ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye kuwa na kitu, ataongezewa, lakini ule mwenye hana, atanyanganywa hata kile chenye iko nacho.” Anaongeza kwamba maadui wake, wenye hawataki ‘akuwe mufalme wao,’ wataharibishwa. Kisha Yesu anaendelea na safari yake kuelekea Yerusalemu.—Luka 19:26-28.