Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 97

Mufano wa Wafanyakazi Katika Shamba la Mizabibu

Mufano wa Wafanyakazi Katika Shamba la Mizabibu

MATAYO 20:1-16

  • WAFANYAKAZI WA “MWISHO” KATIKA SHAMBA LA MIZABIBU WANAKUWA WA “KWANZA”

Yesu ametoka tu kuwaambia wasikilizaji wake katika Perea kwamba “wengi wenye kuwa wa kwanza watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa kwanza.” (Matayo 19:30) Anakazia maneno hayo kupitia mufano kuhusu wafanyakazi katika shamba la mizabibu. Anasema hivi:

“Ufalme wa mbinguni ni kama bwana wa nyumba mwenye alitoka asubui sana ili kutafuta wafanyakazi kwa ajili ya shamba lake la mizabibu. Kisha kupatana na wafanyakazi hao kwamba atawalipa dinari moja kwa siku, akawatuma katika shamba lake la mizabibu. Wakati alitoka tena karibu saa tatu (3), akaona wengine wamesimama bila kazi katika soko; na hao akawaambia, ‘Ninyi pia, muende katika shamba langu la mizabibu, na nitawapatia mushahara wenye kufaa.’ Basi wakaenda. Tena akatoka karibu saa sita (6) na saa kenda (9) na akafanya vilevile. Mwishowe, akatoka karibu saa kumi na moja (11), akakuta wengine wamesimama bila kufanya kitu, na akawauliza, ‘Sababu gani mumesimama hapa muchana wote bila kazi?’ Wakamujibu, ‘Kwa sababu hakuna mutu alitupatia kazi.’ Akawaambia, ‘Ninyi pia muende katika shamba langu la mizabibu.’”—Matayo 20:1-7.

Pengine wasikilizaji wa Yesu wanafikiria Yehova Mungu wakati wanasikia maneno “Ufalme wa mbinguni” na “bwana wa nyumba.” Maandiko yanamutaja Yehova kuwa mwenye shamba la mizabibu, lenye kufananisha taifa la Israeli. (Zaburi 80:8, 9; Isaya 5:3, 4) Wale wenye kuwa katika agano la Sheria wanafananisha wafanyakazi katika shamba la mizabibu. Kwa hiyo, Yesu hazungumuzie wakati wenye umekwisha kupita. Anazungumuzia hali yenye kuwa katika wakati wake.

Viongozi wa dini, kama Wafarisayo wenye wametoka kumujaribu Yesu kuhusu jambo la kuvunja ndoa, ni wao walipaswa kuendelea kumutumikia Mungu. Wako kama wafanyakazi wa wakati wote wenye wanatazamia mushahara wote, ni kusema, dinari moja kwa kazi ya siku moja.

Makuhani na wengine katika kikundi hiki wanaona Wayahudi wa kawaida kuwa wanamutumikia Mungu kidogo, kama vile wafanyakazi wa saa kidogo katika shamba la mizabibu la Mungu. Katika mufano huu wa Yesu, wao ndio watu wenye wanaitwa kwenye kazi “karibu saa tatu (3)” ao nyuma sana katika siku ya kazi, ni kusema, saa sita, saa kenda na mwishowe saa kumi na moja kisha muchana.

Wanaume na wanamuke wenye kumufuata Yesu wanaonwa kama “watu wenye kulaaniwa.” (Yohana 7:49) Walipitisha wakati mwingi wa maisha yao katika kazi ya kuvua samaki ao kazi zingine. Kisha, mwishoni mwa mwaka wa 29 wakati wetu, “mwenye shamba la mizabibu” anamutuma Yesu kuwaita watu hao wapole wafanye kazi ya Mungu wakiwa wanafunzi wa Kristo. Wao ndio watu wa “mwisho” wenye Yesu anazungumuzia, wafanyakazi wa shamba la mizabibu wenye waliitwa saa kumi na moja.

Kwa kumalizia mufano wake, Yesu anaeleza jambo lenye linatokea mwisho wa siku ya kazi: “Wakati ilikuwa mangaribi, mwenye shamba la mizabibu akamuambia musimamizi wa wafanyakazi wake, ‘Ita wafanyakazi na uwalipe mushahara wao, uanze na wale wa mwisho na kumaliza na wale wa kwanza.’ Wakati wale watu wa saa kumi na moja (11) walikuja, kila mumoja akapokea dinari moja. Kwa hiyo, wakati wale wa kwanza walikuja, waliwaza watapokea zaidi, lakini wao pia wakalipwa dinari moja. Wakati waliipokea wakaanza kumunungunikia bwana wa nyumba na kusema, ‘Watu hawa wa mwisho walifanya kazi kwa saa moja tu; lakini umewalipa sawasawa na sisi wenye tulifanya kazi ngumu muchana wote katika jua kali!’ Lakini akamujibu mumoja wao na kusema, ‘Mwenzangu, sikutendee mubaya. Ulipatana na mimi dinari moja, haiko vile? Kamata mushahara wako na uende. Ninataka kupatia huyu wa mwisho sawasawa na wewe. Je, sina haki ya kufanya kile ninataka na mali yangu? Ao jicho lako ni lenye wivu kwa sababu mimi ni mwema?’ Kwa njia hiyo, wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho.”—Matayo 20:8-16.

Pengine wanafunzi wanajiuliza kuhusu sehemu hiyo ya mwisho ya mufano wa Yesu. Namna gani viongozi wa dini, wenye wanajiona kuwa wa “kwanza,” watakuwa wa “mwisho”? Na namna gani wanafunzi wa Yesu wanakuwa wa “kwanza”?

Wanafunzi wa Yesu, wenye Wafarisayo na wengine wanaona kuwa wa, “mwisho,” wanakuwa katika mustari wa “kwanza,” na kupata mushahara wao wote. Kupitia kifo cha Yesu, Yerusalemu la duniani litaharibiwa, kisha Mungu atachagua taifa la mupya, “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16; Matayo 23:38) Yohana Mubatizaji alitaja watu kama hao wakati alizungumuzia ubatizo wenye kuja wa roho takatifu. Wale wenye walikuwa wa “mwisho” wanakuwa wa kwanza kupokea ubatizo huo na kupewa pendeleo la kuwa mashahidi wa Yesu “mupaka kwenye sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Matendo 1:5, 8; Matayo 3:11) Kama wanafunzi wanaelewa mabadiliko makubwa yenye Yesu anazungumuzia, wanaweza kuwazia namna watapambana na mateso makali kutoka kwa viongozi wa dini, wenye wamekuwa wa “mwisho.”