Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 93

Mwana wa Binadamu Atafunuliwa

Mwana wa Binadamu Atafunuliwa

LUKA 17:20-37

  • UFALME UKO KATIKATI YAO

  • ITAKUWA NAMNA GANI WAKATI YESU ATAFUNULIWA?

Yesu angali Samaria ao Galilaya. Sasa Wafarisayo wanamuuliza kuhusu kuja kwa Ufalme wenye wanawazia kwamba utakuja kwa utukufu na itakuwa tukio lenye mambo mengi. Lakini, Yesu anawaambia: “Ufalme wa Mungu hautakuja kwa njia yenye kuonekana na watu wote; na watu hawatasema, ‘Muangalie hapa!’ ao, ‘Pale!’ Kwa maana muangalie! Ufalme wa Mungu uko katikati yenu.”—Luka 17:20, 21.

Watu fulani wanaweza kuwaza kwamba Yesu iko anasema kama Ufalme unatawala katika mioyo ya watumishi wa Mungu. Lakini, haiwezi kuwa vile, kwa sababu Ufalme hauko katika mioyo ya wale Wafarisayo wenye kuzungumuza na Yesu. Lakini Ufalme uko katikati yao kwa sababu Yesu, Mufalme wa Ufalme wa Mungu mwenye amechaguliwa iko pale katikati yao.—Matayo 21:5.

Pengine kisha Wafarisayo kuenda, Yesu anatolea wanafunzi wake maelezo zaidi kuhusu kuja kwa Ufalme huo. Kuhusu kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme, anawaonya kwanza hivi: “Siku zitakuja wakati mutatamani kuona moja ya siku za Mwana wa binadamu, lakini hamutaiona.” (Luka 17:22) Maneno hayo ya Yesu yanaonyesha kama utawala wa Mwana wa binadamu katika Ufalme utakuwa wakati wenye kuja. Pengine mbele wakati huo ufike, wanafunzi fulani wanaweza kuanza kuungojea kwa hamu, lakini wanapaswa kuendelea kungojea mupaka wakati wenye uliwekwa na Mungu wa kuja kwa Mwana wa binadamu.

Yesu anaendelea hivi: “Watu watawaambia ninyi, ‘Muangalie pale!’ ao, ‘Muangalie hapa!’ Musiende wala musiwafuate. Kwa maana kama vile umeme wa radi unawaka kutoka upande mumoja wa mbingu mupaka upande mwingine wa mbingu, ni vile Mwana wa binadamu atakuwa katika siku yake.” (Luka 17:23, 24) Namna gani wanafunzi wa Yesu watalindwa ili wasifuate masiya wa uongo? Yesu anasema kwamba kuja kwa Masiya wa kweli kutakuwa kama vile mwangaza wa radi wenye unaonekana katika eneo kubwa. Ushuhuda wa kuwapo kwake katika mamlaka ya Ufalme utaonekana waziwazi na watazamaji wote wenye kuwa macho.

Kisha Yesu analinganisha siku hiyo na matukio ya zamani ili kuonyesha tabia zenye watu watakuwa nazo wakati huo wenye kuja: “Kama vile ilikuwa katika siku za Noa, ni vile itakuwa katika siku za Mwana wa binadamu. . . . Pia, kama vile ilikuwa katika siku za Loti: walikuwa wanakula, walikuwa wanakunywa, walikuwa wananunua, walikuwa wanauzisha, walikuwa wanapanda, walikuwa wanajenga. Lakini ile siku yenye Loti alitoka Sodoma, kulinyesha mvua ya moto na kiberiti kutoka mbinguni na kuwaharibu wote. Itakuwa vilevile ile siku yenye Mwana wa binadamu atafunuliwa.”—Luka 17:26-30.

Yesu haseme kama watu wa siku za Noa na siku za Loti waliharibiwa kwa sababu walifuatilia mambo ya kawaida ya maisha kama vile kula, kunywa, kununua, kuuzisha, kupanda, na kujenga. Noa na Loti na familia zao pia walifanya mambo fulani kati ya hayo. Lakini watu wengine walifanya mambo hayo bila kufikiria hata kidogo mapenzi ya Mungu na hawakujua waliishi wakati gani. Kwa hiyo, Yesu anawashauria wanafunzi wake wafikirie mapenzi ya Mungu na kuyafanya kwa bidii. Kwa kufanya hivyo, anawaonyesha njia ya kuokoka, ni kusema, njia ya kuendelea kuishi, wakati Mungu ataleta uharibifu wakati wenye kuja.

Wanafunzi wanapaswa kuepuka kukengeushwa na “vitu vyenye kuwa nyuma,” ni kusema, mambo ya ulimwengu yenye kuwazunguka. Yesu anasema: “Siku hiyo mutu mwenye kuwa kwenye sehemu ya juu ya nyumba lakini vitu vyake viko katika nyumba asishuke kuvikamata, vilevile mutu mwenye kuwa katika shamba asirudilie vitu vyenye kuwa nyuma. Mukumbuke bibi ya Loti.” (Luka 17:31, 32) Aligeuka nguzo ya chumvi.

Yesu anaendelea na maelezo yake kuhusu namna mambo yatakuwa wakati Mwana wa binadamu atatawala akiwa Mufalme. Anawaambia hivi wanafunzi wake: “Usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mumoja atachukuliwa, lakini mwingine ataachwa.” (Luka 17:34) Kwa hiyo wamoja wataokoka, lakini wengine wataachwa, ni kusema, watapoteza uzima wao.

Wanafunzi wanauliza: “Wapi, Bwana?” Yesu anajibu: “Mahali kwenye kuwa maiti, tai pia watakusanyika pale pamoja.” (Luka 17:37) Ndiyo, wamoja kati yao watakuwa kama tai wenye kuona mbali. Wanafunzi hao watajikusanya kwenye kuwa Kristo wa kweli, Mwana wa binadamu. Wakati huo wenye kuja, Yesu atawapatia wanafunzi wake kweli yenye kuokoa uzima wa wale wenye kuwa na imani.