Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 91

Lazaro Anafufuliwa

Lazaro Anafufuliwa

YOHANA 11:38-54

  • UFUFUO WA LAZARO

  • SANHEDRINI INAPANGA KUMUUA YESU

Kisha Yesu kukutana na Maria na Marta karibu na Betania, wanaenda wote kwenye kaburi la Lazaro. Kaburi hilo ni pango lenye mwingilio wake unafunikwa na jiwe. Yesu anasema: “Mutoshe lile jiwe.” Marta anakuwa na wasiwasi kwa sababu haelewe jambo lenye Yesu anataka kufanya. Anasema: “Bwana, kufikia sasa lazima anapaswa kuwa ananuka, kwa maana ni siku ine (4).” Lakini Yesu anamuambia: “Je, sikukuambia kwamba ukiamini utaona utukufu wa Mungu?”—Yohana 11:39, 40.

Basi wanatosha jiwe. Kisha Yesu anaangalia juu na kusali hivi: “Baba, ninakushukuru kwa sababu umenisikia. Kwa kweli, nilijua kwamba sikuzote wewe unanisikia; lakini nilisema kwa sababu ya watu wengi wenye wanasimama kunizunguka, ili waamini kwamba ulinituma.” Sala ya Yesu mbele ya watu wengi inaonyesha kama jambo lenye anataka kufanya litatendeka kwa nguvu ya Mungu. Kisha Yesu anasema kwa sauti ya juu: “Lazaro, kuja huku inje!” Na Lazaro anatoka, miguu na mikono yake ikiwa imefungwa kwa vitambaa, na uso wake ukiwa umefungwa kwa kitambaa. Yesu anasema: “Mumufungue na mumuache aende.”—Yohana 11:41-44.

Wayahudi wengi wenye wamekuja kufariji Maria na Marta wanaona muujiza huu na wanamuamini Yesu. Lakini wengine wanaenda kuambia Wafarisayo mambo yenye Yesu amefanya. Wafarisayo na wakubwa wa makuhani wanafanya mukutano wa tribinali kubwa ya Wayahudi yenye kuitwa Sanhedrini. Kuhani mukubwa Kayafa iko pia katika baraza hilo. Wamoja wanasema hivi: “Tufanye nini, kwa maana mutu huyu anafanya alama nyingi? Kama tunamuacha aendelee vile, wote watamuamini, na Waroma watakuja na kukamata mahali petu na taifa letu.” (Yohana 11:47, 48) Hata kama wamesikia ushahidi wa watu wenye walijionea Yesu ‘akifanya alama nyingi,’ watu hawa hawafurahie mambo yenye Mungu iko anafanya kupitia Yesu. Jambo la kwanza lenye wanahangaikia ni cheo na mamlaka yao.

Kufufuliwa kwa Lazaro ni pigo kubwa kwa Wasadukayo wenye hawaamini ufufuo. Sasa Kayafa, Musadukayo anasema: “Ninyi hamujue jambo lolote hata kidogo, na hamuelewe kwamba ni kwa faida yenu mutu mumoja akufe kwa ajili ya watu kuliko taifa lote liharibiwe.”—Yohana 11:49, 50; Matendo 5:17; 23:8.

Kwa sababu ya cheo takatifu cha Kayafa, Mungu anamuwezesha kusema hivyo—haseme hivyo “kwa kujitungia.” Kayafa anamaanisha kwamba Yesu anapaswa kufa ili kumuzuia asiendelee kupunguza mamlaka na ushawishi wa viongozi wa dini ya Wayahudi. Lakini wakati huohuo, unabii wa Kayafa unaonyesha kwamba kupitia kifo chake, Yesu angetoa bei ya ukombozi haiko tu kwa Wayahudi, lakini kwa “watoto [wote] wa Mungu wenye walitawanyika.”—Yohana 11:51, 52.

Kayafa anafikia kusadikisha Sanhedrini ifanye mipango ya kumuua Yesu. Je, inawezekana kwamba, Nikodemo mutu mwenye kuwa katika Sanhedrini, mwenye hamuchukie Yesu, anamufunulia mipango hiyo? Ikuwe hivyo ao hapana, Yesu anatoka Yerusalemu ili kuepuka kifo mbele wakati wenye uliwekwa na Mungu ufike.