Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 82

Utumishi wa Yesu Katika Perea

Utumishi wa Yesu Katika Perea

LUKA 13:22–14:6

  • KUJIKAZA SANA ILI KUINGIA KUPITIA MULANGO MWEMBAMBA

  • YESU ANAPASWA KUFA KATIKA YERUSALEMU

Yesu amekuwa akifundisha na kuponyesha watu katika Yudea na Yerusalemu. Kisha, anavuka Muto Yordani ili kuenda kufundisha kutoka muji mupaka muji katika wilaya ya Perea. Lakini kisha muda mufupi, atarudia katika Yerusalemu.

Wakati Yesu iko katika Perea, mwanaume mumoja anamuuliza hivi: “Bwana, wale wenye wataokolewa wako kidogo?” Pengine mwanaume huyo anajua namna viongozi wa dini wanakuwaka na mabishano kati yao kuhusu wale wenye wataokolewa; ikiwa ni wengi ao ni wachache tu. Kuliko kuzungumuzia jambo la kujua ni watu ngapi ndio wataokolewa, Yesu anazungumuzia kile mutu anapaswa kufanya ili aokolewe. Anasema hivi: “Mujikaze sana ili muingie kupitia mulango mwembamba.” Ndiyo, inaomba kujikaza, kupiganisha. Juu ya nini? Yesu anaeleza hivi: “Wengi watatafuta kuingia lakini hawataweza.”—Luka 13:23, 24.

Yesu anatoa mufano ili kuonyesha kuwa ni jambo la maana kujikaza sana. Anasema hivi: “Wakati mwenye nyumba atasimama na kufunga mulango, mutasimama inje mukipiga hodi kwenye mulango, na kusema, ‘Bwana, utufungulie.’ . . . Lakini atawaambia, ‘Sijue munatoka wapi. Mutoke mbele yangu, ninyi wote wenye kufanya mambo yenye hayako sawa!’”—Luka 13:25-27.

Hilo linaonyesha magumu yenye yatapata mutu mwenye anachelewa—inaonekana anafika wakati wenye yeye mwenyewe anaona kuwa unafaa—na anakuta mulango umefungwa. Angepaswa kufika mbele ya wakati, hata kama aliona kuwa wakati huo haufae kwake. Ni hivyo kwa watu wengi wenye wangepata faida kwa kumuona Yesu pale akiwafundisha. Walishindwa kukamata nafasi hiyo ili kutia ibada ya kweli pa nafasi ya kwanza katika maisha yao. Wengi kati ya watu wenye Yesu alikuwa ametumwa kwao, hawakukubali mupango wenye Mungu amekamata ili kuokoa watu. Yesu anasema kuwa ‘watalia na kusaga meno’ wakati watatupwa inje. Lakini, watu “kutoka mashariki na mangaribi,” ni kusema, watu kutoka mataifa yote, “watakaa kwenye meza katika Ufalme wa Mungu.”—Luka 13:28, 29.

Yesu anaeleza hivi: “Kuko wale wa mwisho [kama vile watu wenye hawako Wayahudi na Wayahudi wa hali ya chini] wenye watakuwa wa kwanza, na kuko wale wa kwanza [Wayahudi wenye kuwa na vyeo vya kidini wenye wanajivuna kwa sababu ni wa kizazi cha Abrahamu] wenye watakuwa wa mwisho.” (Luka 13:30) Watu hao wenye kukosa shukrani watakuwa “wa mwisho,” ni kusema, hawataingia hata kidogo katika Ufalme wa Mungu.

Sasa, Wafarisayo fulani wanakuja kumuona Yesu na kumutolea shauri hili: “Uende na utoke hapa, kwa sababu Herode [Antipa] anataka kukuua.” Pengine ni Mufalme Herode mwenyewe ndiye alianza kutangaza habari hiyo ya uongo ili kumusukuma Yesu akimbie eneo hilo. Pengine Herode anaogopa kuwa kwa njia fulani ataunga mukono kifo cha nabii mwingine, kama vile alifanya katika kifo cha Yohana Mubatizaji. Lakini Yesu anaambia Wafarisayo hivi: “Muende mumuambie ule mbweha, ‘Angalia! ninafukuza pepo wachafu na kuponyesha watu leo na kesho, na siku ya tatu (3) nitakuwa nimemaliza kazi yangu.’” (Luka 13:31, 32) Wakati Yesu anaita Herode “mbweha,” pengine iko anafikiria namna wanyama hao wanakuwaka wenye ujanja. Lakini, Yesu hatakubali Herode ao mutu mwengine yeyote amuongoze ao amusukume kufanya mambo haraka. Ataendelea kutimiza daraka lenye Baba yake alimupatia, na atafanya hivyo kulingana na vile Mungu amepanga, hapana kulingana na mupango wa mwanadamu.

Yesu anaendelea na safari yake ya kuenda Yerusalemu kwa sababu, kama vile anasema, “haiwezekane nabii auawe inje ya Yerusalemu.” (Luka 13:33) Hakuna unabii wa Biblia wenye ulitabiri kuwa Masiya anapaswa kufa katika muji huo, sasa, sababu gani Yesu anasema kuwa atauawa katika Yerusalemu? Kwa sababu, Yerusalemu ndio muji mukubwa, kwenye kuko tribinali kubwa ya Sanhedrini yenye kuwa na watu 71, na kwenye wale wenye wanashitakiwa kuwa manabii wa uongo wanasambishwa. Zaidi ya hilo, ni mahali kwenye zabihu za wanyama zinatolewa. Kwa hiyo, Yesu anatambua kuwa haitawezekana auawe mahali pengine.

Yesu anasema hivi kwa huzuni: “Yerusalemu, Yerusalemu, muuaji wa manabii na mwenye kupiga majiwe wale wenye walitumwa kwake—ni mara ngapi nilitaka kukusanya watoto wako, kama vile kuku anakusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake! Lakini hamukutaka. Angalia! Mumeachiwa nyumba yenu.” (Luka 13:34, 35) Taifa hilo liko linakataa Mwana wa Mungu na linapaswa kupatwa na matokeo ya tendo hilo!

Mbele Yesu aende katika Yerusalemu, kiongozi mumoja wa Wafarisayo anamualika nyumbani kwake siku ya Sabato ili kula chakula. Wale wenye walialikwa wako wanaangalia kwa uangalifu ili kuona kile Yesu atafanyia mwanaume mumoja mwenye kuwa hapo ambaye iko na ugonjwa wenye kufanya mwili uvimbe (ugonjwa wenye kutokea wakati maji yanajaa katika mwili, mara nyingi katika miguu). Yesu anauliza Mufarisayo huyo na watu wenye kujua sana Sheria: “Je, inaruhusiwa kuponyesha siku ya Sabato ao hapana?”—Luka 14:3.

Hakuna mutu mwenye anajibu. Yesu anaponyesha mwanaume huyo na kisha anawauliza hivi: “Ni nani kati yenu, ikiwa mwana wake ao ngombe-dume wake anaanguka ndani ya kisima siku ya Sabato hatamutosha ndani mara moja?” (Luka 14:5) Tena, wanashindwa kujibia ulizo hilo lenye hekima.