Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 139

Yesu Analeta Paradiso na Kumaliza Mugawo Wake

Yesu Analeta Paradiso na Kumaliza Mugawo Wake

1 WAKORINTO 15:24-28

  • MAMBO YENYE YATAPATA KONDOO NA MBUZI

  • WENGI WATAFURAHIA PARADISO DUNIANI

  • YESU ANAONYESHA KABISA KUWA YEYE NI NJIA, KWELI, NA UZIMA

Muda mufupi tu kisha kubatizwa kwake, Yesu alipambana na adui mwenye aliazimia kumuangusha hata mbele aanze kazi yake ya kuhubiri. Ndiyo, Shetani alijikaza mara kwa mara ili kumujaribu Yesu. Kisha, Yesu alisema hivi juu ya muovu huyo: “Mutawala wa ulimwengu anakuja, na hana uwezo juu yangu.”—Yohana 14:30.

Mutume Yohana aliona katika maono mambo yenye yatamupata ‘dragoni mukubwa, ule nyoka wa zamani, mwenye ni Ibilisi na Shetani.’ Adui huyo mukali wa wanadamu angefukuzwa kutoka mbinguni, “akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.” (Ufunuo 12:9, 12) Wakristo wako na sababu za muzuri za kuamini kuwa wanaishi katika “kipindi [hicho] kifupi cha wakati” na kuwa hivi karibuni “ule dragoni, ule nyoka wa zamani,” atafungwa katika abiso na hatatenda tena kwa miaka 1 000 wakati Yesu atakuwa akitawala katika Ufalme wa Mungu.—Ufunuo 20:1, 2.

Wakati huo, ni mambo gani yenye yatatokea katika dunia, makao yetu? Ni nani wenye wataishi ndani, na katika hali gani? Yesu mwenyewe alitoa majibu. Katika mufano wake wa kondoo na mbuzi, alionyesha jambo lenye wanadamu wenye haki watapata wakati wenye kuja, ni kusema, wale wenye kuwa mufano wa kondoo, na wenye kutii na kufanyia ndugu zake mambo ya muzuri. Pia alionyesha waziwazi mambo yenye wale wenye kutenda kwa njia tofauti watapata, ni kusema, wale wenye kuwa mufano wa mbuzi. Yesu alisema hivi: “Hawa [mbuzi] wataharibiwa milele, lakini wale wenye kufanya mambo yenye kuwa sawa [ni kusema, kondoo] wataingia katika uzima wa milele.”—Matayo 25:46.

Hilo linatusaidia kuelewa maneno yenye Yesu aliambia ule mutenda-zambi mwenye alikuwa anatundikwa pembeni yake. Yesu hakumuahidi mwanaume huyo zawadi yenye aliahidi mitume wake waaminifu, ni kusema, zawadi ya kutawala pamoja naye katika Ufalme wa mbinguni. Lakini, Yesu alimutolea mutenda-zambi huyo mwenye kutubu ahadi hii: “Kwa kweli ninakuambia leo, utakuwa pamoja na mimi katika Paradiso.” (Luka 23:43) Kwa hiyo, mwanaume huyo alipata tumaini la kuishi katika Paradiso, ni kusema, bustani yenye kupendeza. Inafaa kusema kwamba, wale wenye kuonyesha leo kuwa wako mufano wa kondoo na wenye watapata “uzima wa milele” watakuwa pia katika Paradiso hiyo.

Hilo linapatana na maelezo yenye mutume Yohana alitoa juu ya hali yenye itakuwa katika dunia. Alisema hivi: “Hema la Mungu liko pamoja na wanadamu, na atakaa pamoja nao, na watakuwa watu wake. Na Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao. Na atapanguza kila chozi katika macho yao, na kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwa tena. Mambo ya zamani yamepita.”—Ufunuo 21:3, 4.

Ili mutenda-zambi huyo apate uzima katika Paradiso, anapaswa kufufuliwa. Na haiko yeye tu ndiye atafufuliwa. Yesu alionyesha wazi jambo hilo wakati alisema hivi: “Musishangazwe na jambo hili, kwa maana saa inakuja yenye wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho watasikia sauti yake na watatoka, wale wenye walitenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, na wale wenye walizoea kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.”—Yohana 5:28, 29.

Lakini tuseme nini juu ya mitume waaminifu na hesabu fulani ya watu wengine wenye watakuwa pamoja na Yesu mbinguni? Biblia inasema hivi: “Watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, na watatawala wakiwa wafalme pamoja naye ile miaka elfu moja (1 000).” (Ufunuo 20:6) Wale wenye watatawala pamoja na Kristo ni wanaume na wanamuke wenye waliishi duniani. Kwa hiyo, wataonyesha kabisa huruma na kuelewa wale wenye watatawaliwa ambao watakuwa katika dunia.—Ufunuo 5:10.

Yesu atatumia zabihu yake ya ukombozi kwa wanadamu katika dunia na kuwaondolea laana ya zambi yenye waliriti. Yeye na watawala wenzake wataongoza wanadamu waaminifu kwenye ukamilifu. Ndiyo, wanadamu watafurahia uzima wenye Mungu alipenda wakuwe nao mwanzoni wakati aliambia Adamu na Eva wazae na wakuwe wengi na wajaze dunia. Hata kifo chenye kilitokana na zambi ya Adamu hakitakuwa tena!

Kwa hiyo, Yesu atakuwa ametimiza mambo yote yenye Yehova alimuomba afanye. Mwishoni mwa Utawala wake wa Miaka Elfu Moja, Yesu, atarudishia Baba yake Ufalme na familia ya wanadamu wakamilifu. Juu ya tendo hilo la ajabu lenye kuonyesha unyenyekevu wa Yesu, mutume Paulo aliandika hivi: “Wakati vitu vyote vitakuwa vimewekwa chini ya mamlaka yake, halafu Mwana mwenyewe atajiweka chini ya mamlaka ya Ule mwenye aliweka vitu vyote chini ya mamlaka yake, ili Mungu akuwe vitu vyote kwa kila mutu.”—1 Wakorinto 15:28.

Ni wazi kwamba, Yesu iko na daraka la maana katika kutimiza makusudi ya Mungu yenye utukufu. Na wakati makusudi hayo yanaendelea kutimia katika umilele wote, ataonyesha kuwa maneno yenye alisema juu yake mwenyewe ni ya kweli kabisa: “Mimi ndiye njia na kweli na uzima.”—Yohana 14:6.