Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 130

Yesu Anatolewa na Kupelekwa ili Auawe

Yesu Anatolewa na Kupelekwa ili Auawe

MATAYO 27:31, 32 MARKO 15:20, 21 LUKA 23:24-31 YOHANA 19:6-17

  • PILATO ANAJARIBU KUMUACHILIA YESU

  • YESU ANAHUKUMIWA NA ANAPELEKWA ILI AUAWE

Hata kama Yesu ametendewa mubaya sana na kuchekelewa, bidii ya Pilato ya kutaka kumufungua haichochee wakubwa wa makuhani na wale wenye kuwaunga mukono. Hawapendi jambo lolote liwazuie kuua Yesu. Wanaendelea kulalamika hivi: “Auawe kwenye muti! Auawe kwenye muti!” Pilato anajibu hivi: “Mumukamate ninyi wenyewe na mumuue, kwa maana mimi sione kosa lolote ndani yake.”—Yohana 19:6.

Wayahudi hawamusadikishe Pilato kuwa Yesu anastahili kifo kwa kutumia mashitaka ya politike, lakini tuseme nini juu ya mashitaka ya mambo ya dini? Wanarudilia shitaka la kuwa Yesu amekufuru, lenye walisema wakati walikuwa wanamusambisha mbele ya Sanhedrini. Wanasema hivi: “Sisi tuko na sheria, na kulingana na sheria anapaswa kufa, kwa sababu alijifanya mwenyewe kuwa mwana wa Mungu.” (Yohana 19:7) Hili ni shitaka la mupya kwa Pilato.

Anarudia ndani ya nyumba yake na kujaribu kutafuta njia ya kufungua mwanaume huyo mwenye ametendewa mubaya sana na mwenye bibi yake aliota ndoto juu yake. (Matayo 27:19) Tuseme nini juu ya shitaka hilo la mupya lenye Wayahudi wanatoa, la kusema kwamba mufungwa huyo ni “mwana wa Mungu”? Pilato anajua kwamba Yesu ni mutu wa Galilaya. (Luka 23:5-7) Lakini, anamuuliza hivi: “Umetoka wapi?” (Yohana 19:9) Je, Pilato alikuwa anajiuliza ikiwa pengine Yesu aliishi zamani, na kwa njia fulani alitoka kwa Mungu?

Pilato alikuwa amesikia moja kwa moja namna Yesu alimuambia kuwa yeye ni mufalme lakini Ufalme wake hauko sehemu ya ulimwengu huu. Yesu hapendi kurudilia mambo yenye alikuwa amesema, kwa hiyo, anabakia kimya. Kwa sababu Yesu anakataa kumujibu, Pilato anakasirika na anamuambia hivi kwa ukali: “Unakataa kusema na mimi? Haujue kama niko na mamlaka ya kukufungua na niko na mamlaka ya kukuua?”—Yohana 19:10.

Yesu anasema tu hivi: “Wewe haungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama haungepewa kutoka juu. Ndiyo sababu mutu mwenye alinitia katika mikono yako iko na zambi kubwa zaidi.” (Yohana 19:11) Inawezekana kuwa Yesu hafikirie tu mutu mumoja. Lakini anamaanisha kuwa Kayafa, wale wenye kumuunga mukono, na Yuda Iskariote wako na zambi kubwa zaidi kuliko Pilato.

Maneno ya Yesu na namna anajiendesha vinamushangaza Pilato, na anaogopa zaidi kuwa pengine Yesu ametoka kwa Mungu, kwa hiyo, anajaribu tena kumuachilia. Lakini, Wayahudi wanasema mambo mengine yenye yanapaswa kumuogopesha Pilato. Wanamuogopesha hivi: “Kama unamufungua mutu huyu, wewe hauko rafiki ya Kaisari. Kila mutu mwenye anajifanya mwenyewe kuwa mufalme anasema mubaya juu ya Kaisari.”—Yohana 19:12.

Pilato anatosha tena Yesu inje, anakaa kwenye kiti chake cha hukumu na kuambia watu hivi: “Muone! Mufalme wenu!” Lakini, Wayahudi hawabadilishe mawazo yao. Wanalalamika hivi: “Umuondoe! Umuondoe! Auawe kwenye muti!” Pilato anasema hivi: “Niue mufalme wenu?” Kwa muda murefu Wayahudi wameteswa na Utawala wa Roma; hata hivyo, wakubwa wa makuhani wanasema hivi: “Sisi hatuna mufalme isipokuwa Kaisari.”—Yohana 19:14, 15.

Kwa sababu ya kuogopa, Pilato anakubali ombi lenye Wayahudi wamefanya tena na tena, na anawatolea Yesu ili wamuue. Maaskari wanamutosha Yesu nguo ya rangi ya zambarau na wanamuvalisha nguo zake za inje. Wakati Yesu anapelekwa, anapaswa kubeba yeye mwenyewe muti wake wa mateso.

Sasa ni asubui ya Siku ya Tano tarehe 14 mwezi wa Nisani. Yesu amekuwa macho tangu Siku ya Ine asubui na ametendewa matendo mbalimbali ya mubaya yenye kuumiza sana. Yesu anajikaza sana kubeba muti huo muzito, lakini nguvu zinamuisha. Kwa hiyo, maaskari wanakaza mutu mumoja mwenye kupita amusaidie, ni kusema, Simoni wa Kirene ya Afrika abebe muti huo wa mateso mahali penye Yesu atauawa. Watu wengi wanawafuata, wamoja wanajipiga-piga kifua kwa uchungu kwa sababu wanahuzunishwa na mambo yenye yako yanatendeka.

Yesu anaambia hivi wanamuke wenye kulia: “Mabinti wa Yerusalemu, muache kunililia. Lakini mujililie ninyi wenyewe na watoto wenu; kwa maana muangalie! Siku zinakuja wakati watu watasema, ‘Wenye furaha ni wanamuke tasa, na matumbo ya uzazi yenye hayakuzaa, na maziwa yenye hayakunyonyesha!’ Kisha wataanza kuambia milima, ‘Mutuangukie!’ na vilima, ‘Mutufunike!’ Kama wanafanya mambo haya wakati muti ni mubichi, itakuwa namna gani wakati utakuwa umekauka?”—Luka 23:28-31.

Yesu anazungumuzia taifa la Wayahudi. Liko kama muti wenye kukauka wenye ungali na sehemu fulani ya mubichi kwa sababu Yesu angali na pia Wayahudi fulani wenye kumuamini. Wakati hao wataondolewa, kutabakia tu taifa lenye kukauka kiroho, kama muti wenye kufa. Watu watalia sana wakati majeshi ya Roma yataleta hukumu ya Mungu juu ya taifa hilo!