Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 136

Pembeni ya Bahari ya Galilaya

Pembeni ya Bahari ya Galilaya

YOHANA 21:1-25

  • YESU ANATOKEA KWENYE BAHARI YA GALILAYA

  • PETRO NA WENGINE WANAPASWA KULISHA KONDOO

Katika usiku wake wa mwisho pamoja na mitume wake, Yesu aliwaambia hivi: “Kisha kufufuliwa, nitawatangulia kuingia Galilaya.” (Mathayo 26:32; 28:7, 10) Sasa wengi kati ya wanafunzi wake wanaenda Galilaya, lakini watafanya nini huko?

Wakati fulani, Petro anaambia hivi mitume sita: “Ninaenda kuvua samaki.” Wote sita wanajibu hivi: “Sisi pia tutaenda pamoja na wewe.” (Yohana 21:3) Usiku wote hawakamate hata samaki moja. Wakati usiku unakaribia kucha, Yesu anatokea kwenye inchi kavu, lakini hawatambue ni nani. Yesu anasema hivi kwa sauti kubwa: “Watoto, muko na kitu cha kula?” Wanajibu hivi: “Hapana!” Yesu anawaambia hivi: “Mutupe wavu upande wa kuume wa mashua, na mutapata.” (Yohana 21:5, 6) Wanakamata samaki wengi sana mupaka wanashindwa kukokota wavu.

Yohana anamuambia Petro hivi: “Ni Bwana!” (Yohana 21:7) Mara moja Petro anavaa nguo yake ya inje yenye hakukuwa anavaa wakati alikuwa anavua samaki. Anajitupa katika bahari na kuogelea karibu metre 90 mupaka kwenye inchi kavu. Wengine wenye kuwa katika mashua wanafuata polepole, na wako wanakokota wavu yenye kujaa samaki.

Wakati wanafika kwenye inchi kavu, wanaona “moto wa makaa na samaki zilikuwa juu yake na mukate.” Yesu anasema hivi: “Mulete sehemu fulani ya samaki kati ya wale wenye mumevua sasa hivi.” Petro anatosha samaki katika wavu yenye kuwa na samaki wakubwa 153! Yesu anasema hivi: “Mukuje mukule chakula cha asubui.” Hakuna hata mumoja wao mwenye kuwa na ujasiri wa kumuuliza: “Wewe ni nani?” kwa sababu wanatambua kuwa ni Yesu. (Yohana 21:10-12) Hii ndiyo mara ya tatu anatokea mitume wakati wako pamoja.

Yesu anapatia kila mumoja wao mukate na samaki ili wakule. Kisha, pengine kwa kuangalia samaki wenye walikuwa wamevua, anauliza hivi: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda kuliko hawa?” Je, Petro anapenda sana kazi ya kuvua samaki kuliko kazi yenye Yesu anapenda afanye? Petro anajibu hivi: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Kwa hiyo, Yesu anamuambia hivi: “Lisha wana-kondoo wangu.”—Yohana 21:15.

Tena Yesu anamuuliza hivi: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Pengine anavurugika, anajibu hivi kwa moyo wote: “Ndiyo, Bwana, unajua ninakupenda.” Yesu anamuambia mambo yaleyale: “Chunga kondoo wangu wadogo.”—Yohana 21:16.

Yesu anamuuliza hivi kwa mara ya tatu: “Simoni mwana wa Yohana, je, unanipenda?” Sasa pengine Petro anajiuliza ikiwa Yesu iko na mashaka juu ya ushikamanifu wake. Petro anasema hivi kwa huruma: “Bwana, wewe unajua mambo yote; unajua kwamba ninakupenda.” Tena, Yesu anakazia jambo lenye Petro anapaswa kufanya: “Lisha kondoo wangu wadogo.” (Yohana 21:17) Kwa kweli, wale wenye kuongoza wanapaswa kutumikia wale wenye wanafikia kuwa kondoo wa Mungu.

Yesu alifungwa na kuuawa kwa sababu alifanya kazi yenye Mungu alimutuma afanye. Sasa anaonyesha kuwa Petro pia atatendewa hivyo. Anasema hivi: “Wakati ulikuwa kijana, ulikuwa unajivalisha mwenyewe na kutembea kila mahali ulitaka. Lakini wakati utazeeka, utanyoosha mikono yako na mutu mwingine atakuvalisha na kukupeleka mahali haupendi.” Lakini Yesu anamushauria hivi: “Endelea kunifuata.”—Yohana 21:18, 19.

Petro anaangalia mutume Yohana na kumuuliza hivi: “Bwana, itakuwa namna gani kwa mutu huyu?” Ndiyo, wakati wenye kuja wa mutume mwenye Yesu anapenda utakuwa namna gani? Yesu anajibu hivi: “Kama ni mapenzi yangu akae mupaka nikuje, hilo linakuangalia?” (Yohana 21:21-23) Petro anapaswa kumufuata Yesu bila kuhangaikia mambo yenye wengine wanafanya. Hata hivyo, Yesu anaonyesha kuwa Yohana ataishi muda murefu kuliko mitume wengine wote na kwamba atapewa maono juu ya kuja kwa Yesu katika nguvu ya Ufalme.

Kwa kweli, kuko mambo mengine mengi yenye Yesu alifanya yenye hayawezi kuenea katika vitabu vingi vya kukunjwa.