Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 101

Anatumia Chakula Katika Nyumba ya Simoni Katika Betania

Anatumia Chakula Katika Nyumba ya Simoni Katika Betania

MATAYO 26:6-13 MARKO 14:3-9 YOHANA 11:55–12:11

  • YESU ANARUDIA BETANIA, KARIBU NA YERUSALEMU

  • MARIA ANAMWANGA MAFUTA YENYE KUWA NA MARASHI KWENYE KICHWA CHA YESU

Yesu anatoka Yeriko na kuenda Betania. Kijiji cha Betania kinapatikana mahali penye kuwa juu; na inaomba kupanda kilometre 20, kwa kutumia njia zenye haziko za muzuri. Muji wa Yeriko uko kwenye metre karibu 250 chini ya usawa wa bahari, na kijiji cha Betania kiko kwenye metre karibu 610 juu ya usawa wa bahari. Lazaro na dada zake wawili wanaishi katika kijiji kidogo cha Betania chenye kuwa kwenye kilometre 3 hivi kutoka Yerusalemu, upande wa mashariki mwa Mulima wa Mizeituni.

Wayahudi wengi wamekwisha kufika Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. Wamekuja mbele “ili wajisafishe kulingana na desturi,” ikiwa wamegusa maiti ao kufanya jambo fulani lingine lenye limewachafua. (Yohana 11:55; Hesabu 9:6-10) Wamoja kati yao wenye wamefika mbele wanakusanyika kwenye hekalu. Wanajiuliza kama Yesu atakuja kwenye Pasaka.—Yohana 11:56.

Wanabishana sana kuhusu Yesu. Viongozi fulani wa dini wanapenda kumukamata Yesu ili kumuua. Wametoa hata maagizo kwamba mutu yeyote akijua kwenye Yesu iko, aende kuwaelezea “ili wamukamate.” (Yohana 11:57) Viongozi hawa wamekwisha kujaribu kumuua Yesu kisha yeye kumufufua Lazaro. (Yohana 11:49-53) Sasa tunaelewa sababu gani wengine wanajiuliza kama Yesu atajionyesha waziwazi tena.

Yesu anafika Betania Siku ya Tano, “siku sita (6) mbele ya Pasaka.” (Yohana 12:1) Siku mupya (Sabato, Nisani 8) inaanza wakati jua inashuka. Kwa hiyo, anamaliza safari yake mbele Sabato ianze. Hangesafiri kutoka Yeriko siku ya Sabato, ni kusema, kuanzia Siku ya Tano wakati jua inashuka mupaka Siku ya Posho wakati jua inashuka, kwa sababu sheria ya Wayahudi ilikataza sana kusafiri wakati huo. Pengine Yesu anaenda kwenye nyumba ya Lazaro, kama vile alifanya mbele.

Simoni, mwenye pia anaishi Betania, anaalika Yesu na marafiki zake, kutia ndani Lazaro, kwenye chakula Siku ya Posho, mangaribi. Simoni anaitwa “mwenye ukoma,” pengine ni kwa sababu zamani alikuwa na ugonjwa wa ukoma wenye Yesu aliponyesha. Kama kawaida yake, Marta anatumika tena kwa bidii ili kutumikia wageni. Maria anamukazia Yesu uangalifu, wakati huu anafanya jambo lenye linatokeza mabishano.

Maria anafungua chupa ndogo ya alabasta yenye kuwa na “ratili moja ya mafuta yenye marashi, nardo ya kweli.” (Yohana 12:3) Mafuta hii ni ya bei sana, samani yake (dinari 300) ni sawasawa na mushahara wa mwaka muzima! Maria anamwanga mafuta kwenye kichwa cha Yesu na kwenye miguu yake na kisha anatumia nywele zake ili kumupanguza miguu yake. Harufu ya marashi (parfum) hiyo inaenea nyumba yote.

Wanafunzi wanakasirika na kuuliza: “Sababu gani mafuta haya yenye marashi yamepotezwa bure?” (Marko 14:4) Yuda Iskariote anauliza: “Sababu gani mafuta haya yenye marashi hayakuuzishwa kwa dinari mia tatu (300) na feza hizo zipewe maskini?” (Yohana 12:5) Yuda hahangaikie kabisa maskini. Amekuwa akiiba feza katika kisanduku chenye feza ambacho anachunga kwa ajili ya wanafunzi.

Yesu anamutetea Maria, anasema: “Sababu gani munataka kusumbua mwanamuke huyu? Amenifanyia tendo la muzuri. Kwa maana maskini muko nao sikuzote, lakini hamutakuwa na mimi sikuzote. Wakati alitia mafuta haya yenye marashi kwenye mwili wangu, alifanya vile ili kunitayarisha kwa ajili ya maziko. Kwa kweli ninawaambia ninyi, kila mahali kwenye hii habari njema itahubiriwa katika ulimwengu wote, jambo lenye mwanamuke huyu alifanya litasemwa pia ili kumukumbuka.”—Matayo 26:10-13.

Yesu amefanya zaidi ya siku moja katika Betania, na habari inaenea kwamba iko katika eneo hilo. Wayahudi wengi wanakuja kwa Simoni, haiko tu juu ya kumuona Yesu lakini pia ili kumuona Lazaro, “mwenye [Yesu] alikuwa amefufua kutoka kwa wafu.” (Yohana 12:9) Sasa, wakubwa wa makuhani wanafanya shauri ili kuua Yesu na Lazaro. Wanajua kwamba jambo lingine lenye linafanya watu wengi wamuamini Yesu ni kwa sababu Lazaro amekuwa muzima tena. Viongozi hao wa dini ni waovu kabisa!