Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 134

Kaburi Liko Wazi, Kwa Sababu Yesu Ni Mwenye Kuishi!

Kaburi Liko Wazi, Kwa Sababu Yesu Ni Mwenye Kuishi!

MATAYO 28:3-15 MARKO 16:5-8 LUKA 24:4-12 YOHANA 20:2-18

  • YESU ANAFUFULIWA

  • MATUKIO KWENYE KABURI LA YESU

  • ANATOKEA WANAMUKE MBALIMBALI

Wanamuke wanashituka wakati wanaona kuwa kaburi liko wazi! Maria Magdalene anakimbia kwa “Simoni Petro na kwa ule mwanafunzi mwingine, mwenye Yesu alikuwa anapenda,” ni kusema, mutume Yohana. (Yohana 20:2) Lakini, wanamuke wengine wenye wamebakia kwenye kaburi wanaona malaika. Na ndani ya kaburi la ukumbusho kuko malaika mwingine, mwenye “amevaa kanzu nyeupe.”—Marko 16:5.

Malaika mumoja anawaambia hivi: “Musiogope, kwa maana ninajua munatafuta Yesu mwenye aliuawa kwenye muti. Haiko hapa, kwa maana amefufuliwa, kama vile alisema. Mukuje, muone mahali alikuwa amelala. Basi muende haraka na muambie wanafunzi wake kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu, kwa maana muangalie! anawatangulia kuingia Galilaya.” (Matayo 28:5-7) Kwa hiyo, “wakitetemeka na kushangaa sana,” wanamuke hao wanakimbia ili kuelezea wanafunzi.—Marko 16:8.

Kufikia sasa, Maria amepata Petro na Yohana. Kwa sauti yenye kuchoka, anasema hivi: “Wamemutosha Bwana katika kaburi, na hatujue wamemulalisha wapi.” (Yohana 20:2) Mara moja Petro na Yohana wanaanza kukimbilia kwenye kaburi. Yohana anakimbia mbio zaidi na kufika wa kwanza kwenye kaburi. Anachungulia ndani lakini anaona tu nguo zenye zilitumiwa ili kufunga mwili wa Yesu, lakini anabakia inje.

Wakati Petro anafika anaingia mara moja ndani ya kaburi. Anaona nguo za kitani na nguo yenye ilitumiwa ili kufunga kichwa cha Yesu. Sasa Yohana pia anaingia ndani, na anaamini habari yenye Maria aliwaelezea. Hata kama Yesu alikuwa amezungumuza na mitume wake juu ya jambo hilo, hawaelewe kuwa amefufuliwa. (Matayo 16:21) Wanavurugika, na wanaenda nyumbani. Lakini Maria, mwenye amerudia kwenye kaburi, anabakia hapo.

Wakati huohuo, wanamuke hao wengine wanaenda kuambia wanafunzi wa Yesu kuwa amefufuliwa. Wakati wako wanakimbia ili kufanya hivyo, Yesu anakutana nao na kuwaambia hivi: “Siku njema!” Wanaangukia kwenye miguu yake na ‘wanainama mbele yake.’ Kisha Yesu anasema hivi: “Musiogope! Muende, mujulishe ndugu zangu ili waende Galilaya, na kule wataniona.”—Matayo 28:9, 10.

Mbele ya hapo, wakati tetemeko lilitokea na malaika wakatokea, maaskari wenye walikuwa kwenye kaburi ‘walitetemeka, na kuwa kama wafu.’ Kisha kuamuka, waliingia katika muji na “kujulisha wakubwa wa makuhani mambo yote yenye yalikuwa yametokea.” Kisha makuhani wakazungumuza na wazee wa Wayahudi. Wakachukua uamuzi wa kuwapatia maaskari hao rushwa (kata-midomo) ili wafiche jambo hilo na waseme hivi: “Wanafunzi wake walikuja usiku na kumuiba wakati tulikuwa tumelala usingizi.”—Matayo 28:4, 11, 13.

Maaskari Waroma wanaweza kuuawa ikiwa wanalala usingizi wakati wanafanya ulinzi, kwa hiyo, makuhani wanawaahidi hivi: “Kama gavana anapata habari hiyo [uongo wao kwamba walikuwa wamelala], tutamufasiria kile kilifanyika, na hamutakuwa na sababu ya kuogopa.” (Matayo 28:14) Maaskari hao wanakubali rushwa hiyo na wanafanya mambo yenye makuhani wanaomba. Kwa hiyo, habari ya uongo kuwa mwili wa Yesu uliibwa inaenea kati ya Wayahudi.

Maria Magdalene angali analia kwenye kaburi. Wakati anakaribia ili kuangalia ndani ya kaburi hilo, anaona malaika wawili! Mumoja anakaa mahali penye kichwa cha Yesu kilikuwa na mwingine anakaa mahali miguu yake ilikuwa. Wanauliza hivi: “Mwanamuke, sababu gani unalia?” Maria anajibu hivi: “Wamemuondoa Bwana wangu, na sijue wamemulalisha wapi.” Wakati Maria anageuka anaona mutu mwingine. Mutu huyo anarudilia ulizo la malaika hao, anauliza hivi: “Unamutafuta nani?” Maria anafikiri kuwa mutu huyo ni mwenye kutunza bustani, kwa hiyo, anamuambia hivi: “Bwana, kama umemubeba, niambie umemulalisha wapi, na nitamutosha.”—Yohana 20:13-15.

Kwa kweli, Maria anazungumuza na Yesu mwenye amefufuliwa, lakini wakati huu hamutambue. Lakini, wakati anasema, “Maria!” anaelewa kuwa ni Yesu, anatambua namna Yesu anazoea kuzungumuza naye. Maria anasema hivi kwa furaha: “Raboni!” (neno lenye linamaanisha “Mwalimu!”). Lakini, kwa sababu anaogopa kuwa Yesu anakaribia kupanda mbinguni, anamubana sana. Kwa hiyo, Yesu anamuambia hivi: “Acha kunishika, kwa maana sijapanda kuenda kwa Baba. Lakini uende kwa ndugu zangu na uwaambie, ‘Ninapanda kuenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu.’”—Yohana 20:16, 17.

Maria anakimbia na kuenda mahali penye mitume na wanafunzi wengine wamekusanyika. Anawaambia hivi: “Nimemuona Bwana!” kama vile wanamuke hao wengine walikuwa wamewaelezea. (Yohana 20:18) Lakini, maneno hayo ‘yanaonekana kwao kama hayana maana.’—Luka 24:11.