Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 138

Kristo Iko Kwenye Mukono wa Kuume wa Mungu

Kristo Iko Kwenye Mukono wa Kuume wa Mungu

MATENDO 7:56

  • YESU ANAKAA KWENYE MUKONO WA KUUME WA MUNGU

  • SAULI ANAKUWA MWANAFUNZI

  • TUKO NA SABABU YA KUFURAHI

Siku kumi kisha Yesu kupanda mbinguni, roho takatifu ilimwangwa siku ya Pentekoste, hilo lilihakikisha kuwa iko kabisa mbinguni. Na ushuhuda mwengine ulikuwa karibu kutokea. Mbele tu mwanafunzi Stefano apigwe majiwe kwa sababu ya kutoa ushahidi kwa uaminifu, alisema hivi: “Angalia! ninaona mbingu zimefunguka na Mwana wa binadamu amesimama kwenye mukono wa kuume wa Mungu.”—Matendo 7:56.

Wakati iko na Baba yake mbinguni, Yesu angengojea amri moja yenye kuwa wazi yenye ilitabiriwa katika Neno la Mungu. Daudi aliongozwa na roho ya Mungu ili kuandika hivi: “Yehova alimuambia Bwana wangu [Yesu]: ‘Kaa kwenye mukono wangu wa kuume mupaka niweke maadui wako kuwa kiti cha miguu yako.’” Wakati kipindi cha kungojea kingeisha, ‘angeenda akitiisha katikati ya maadui wake.’ (Zaburi 110:1, 2) Lakini Yesu angefanya nini mbinguni wakati iko anangojea wakati wa kutenda juu ya maadui wake?

Kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33 wakati wetu kutaniko la Kikristo lilizaliwa. Yesu alianza kutawala juu ya wanafunzi wake watiwa mafuta akiwa mbinguni. (Wakolosai 1:13) Aliwaongoza katika kazi ya kuhubiri na kuwatayarisha kwa ajili ya daraka lao la wakati wenye kuja. Ni daraka gani? Wale wenye wangebakia waaminifu mupaka mwisho, wangefikia kufufuliwa na kuwa wafalme pamoja na Yesu katika Ufalme wake.

Mufano muzuri zaidi wa mutu mumoja mwenye angekuwa mufalme ni Sauli, mwenye kujulikana sana kwa jina lake la Kiroma, Paulo. Alikuwa Muyahudi mwenye alikuwa na bidii kwa ajili ya Sheria ya Mungu, lakini alidanganywa na viongozi wa dini ya Wayahudi mupaka akakubali Stefano apigwe majiwe. Kisha, kwa ‘kuogopesha wanafunzi wa Bwana na . . . kutaka kuwaua,’ Sauli akaenda Damasko. Kuhani Mukubwa Kayafa alimupatia ruhusa ya kufunga wanafunzi wa Yesu na kuwaleta katika Yerusalemu. (Matendo 7:58; 9:1) Lakini, wakati Sauli alikuwa katika safari, mwangaza ukatokea na kumuzunguka na akaanguka chini.

Sauti ya mutu mwenye haonekane inamuita hivi: “Sauli, Sauli, Sababu gani unanitesa?” Sauli anauliza hivi: “Wewe ni nani Bwana?” Anajibu hivi: “Mimi ni Yesu mwenye unatesa.”—Matendo 9:4, 5.

Yesu anamuambia Sauli aingie katika muji wa Damasko na angojee maagizo mengine, lakini alipaswa kuongozwa kwa sababu mwangaza huo wa muujiza ulikuwa umemufanya kipofu. Katika maono mengine, Yesu anamutokea Anania, mumoja kati ya wanafunzi wake wenye kuishi katika Damasko. Yesu anamuambia aende mahali fulani kutafuta Sauli. Anania anaogopa kufanya hivyo, lakini Yesu anamuhakikishia hivi: “Mutu huyu ni chombo chenye nimechagua ili kupeleka jina langu kwa mataifa na vilevile kwa wafalme na kwa wana wa Israeli.” Sauli anaanza kuona tena, na katika Damasko “akaanza kuhubiri . . . juu ya Yesu, kwamba huyu ndiye Mwana wa Mungu.”—Matendo 9:15, 20.

Kwa musaada wa Yesu, Paulo na waeneza-injili wengine waliendelesha kazi ya kuhubiri yenye Yesu alikuwa ameanzisha. Mungu aliwabariki kwa kuwasaidia kupata matokeo makubwa. Kisha kupita miaka 25 hivi tangu wakati Yesu alimutokea katika barabara ya kuenda Damasko, Paulo aliandika kuwa habari njema ilikuwa ‘imehubiriwa katika uumbaji wote chini ya mbingu.’—Wakolosai 1:23.

Kisha miaka fulani, Yesu alimupatia Yohana, mutume mwenye alikuwa anapenda, maono mbalimbali. Maono hayo yanapatikana katika Biblia katika kitabu cha Ufunuo. Kupitia maono hayo, kwa kweli Yohana, anaona Yesu anarudia katika mamlaka yake ya Kifalme. (Yohana 21:22) ‘Kwa muongozo wa roho [Yohana] alikuja kuwa katika siku ya Bwana.’ (Ufunuo 1:10) Hilo lingekuwa wakati gani?

Kujifunza unabii wa Biblia kwa uangalifu kunaonyesha kuwa “siku ya Bwana” ilianza katika siku zetu. Katika mwaka wa 1914, vita yenye ilifikia kuitwa Vita ya Kwanza ya Ulimwengu ilianza. Na kwa miaka mingi kisha hapo kumekuwa vita nyingi sana, magonjwa, njaa, matetemeko ya inchi na ushuhuda mwingine wenye umetimiza kwa kiasi kikubwa “alama” yenye Yesu alitolea mitume wake juu ya “kuwapo” kwake na “umalizio.” (Matayo 24:3, 7, 8, 14) Kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme inaendelea kufanywa sasa, haiko katika Utawala wa Roma tu, lakini katika dunia yote.

Yohana aliongozwa na roho ya Mungu ili kueleza maana ya mambo hayo. Alisema hivi: “Sasa kumekuwa wokovu na nguvu na Ufalme wa Mungu wetu na mamlaka ya Kristo wake.” (Ufunuo 12:10) Ndiyo, Ufalme wa Mungu wenye kuwa mbinguni, wenye Yesu alitangaza sana, ni jambo la kweli kabisa!

Hiyo ni habari ya muzuri sana kwa wanafunzi wote washikamanifu wa Yesu. Wanaweza kuweka katika moyo wao maneno haya ya Yohana: “Kwa sababu hiyo mufurahi, ninyi mbingu nanyi wenye munakaa ndani yake! Ole wa dunia na wa bahari, kwa sababu Ibilisi ameshuka kwenu, akiwa na kasirani kali, akijua kwamba iko na kipindi kifupi cha wakati.”—Ufunuo 12:12.

Kwa hiyo, Yesu hakae tena kwenye mukono wa kuume wa Baba yake na kungojea. Yeye ni Mufalme mwenye kutawala, na hivi karibuni ataondoa maadui wake wote. (Waebrania 10:12, 13) Hayo ni mambo ya muzuri sana yenye tunangojea.