Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SURA YA 108

Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego Yao

Wanashindwa Kumunasa Yesu Katika Mitego Yao

MATAYO 22:15-40 MARKO 12:13-34 LUKA 20:20-40

  • VITU VYA KAISARI KWA KAISARI

  • WENYE WATAFUFULIWA WATAFUNGA NDOA?

  • AMRI ZENYE KUWA KUBWA ZAIDI

Maadui wa Yesu wanakasirika. Ametoka tu kuzungumuzia mifano yenye kufunua uovu wao. Sasa Wafarisayo wanataka kumutega. Wanapenda aseme jambo fulani lenye litafanya wamutoe kwa gavana Muroma, na wanalipa wanafunzi wao fulani ili wamunase katika mitego.—Luka 6:7.

Wanamuambia hivi: “Mwalimu, tunajua wewe unasema na kufundisha bila kukosea na hauna ubaguzi, lakini unafundisha njia ya Mungu kupatana na kweli: Je, tunaruhusiwa kulipa Kaisari kodi ya kichwa ao hapana?” (Luka 20:21, 22) Yesu hadanganywe na maneno yao yenye kuonekana kuwa ya muzuri, kwa sababu yanaficha ujanja na unafiki wao. Kama anasema, ‘Hapana, hamupaswe kulipa kodi hiyo,’ atashitakiwa kuwa mutu mwenye anataka kupindua utawala wa Roma. Lakini kama anasema, ‘Ndiyo, mulipe kodi,’ watu wenye hawapendi kutawaliwa na Waroma watakasirika na kumugeukia. Basi, anajibu namna gani?

Yesu anajibu hivi: “Sababu gani munanijaribu, ninyi wanafiki? Munionyeshe feza moja ya kichele ya kodi.” Wakamuletea dinari. Akawaambia: “Sura hii na muandiko huu ni ya nani?” Wakasema: “Ni ya Kaisari.” Kisha Yesu akawatolea muongozo wa muzuri sana: “Basi, mulipe Kaisari vitu vya Kaisari, lakini Mungu vitu vya Mungu.”—Matayo 22:18-21.

Watu hao wanashangazwa na maneno ya Yesu. Kisha kunyamazishwa na jibu lake lenye hekima, wanaenda zao. Lakini siku ingali inaendelea, na mitego ya kumunasa haijamalizika. Kisha Wafarisayo kushindwa kumunasa, viongozi wa kikundi kingine cha dini wanamukaribia Yesu.

Wasadukayo, wenye wanasema kama hakuna ufufuo, wakamuuliza ulizo kuhusu ufufuo na ndoa kati ya mutu na bibi ya ndugu yake. Wanauliza: “Mwalimu, Musa alisema: ‘Kama mutu yeyote anakufa bila kupata watoto, ndugu yake anapaswa kumuoa bibi yake na kumuinulia ndugu yake uzao.’ Sasa kulikuwa ndugu saba (7) katikati yetu. Wa kwanza akaoa na akakufa, na kwa sababu hakukuwa na uzao wowote, akamuachia ndugu yake bibi yake. Ikakuwa vilevile kwa ule wa pili na wa tatu (3), mupaka wote saba (7). Mwishowe, ule mwanamuke naye akakufa. Basi, wakati wa ufufuo, ule mwanamuke atakuwa bibi ya nani kati ya hao saba (7)? Kwa maana alikuwa bibi yao wote.”—Matayo 22:24-28.

Yesu anatumia maandishi ya Musa yenye kukubaliwa na Wasadukayo, kwa kusema hivi: “Munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu. Kwa maana wakati wanafufuliwa kutoka kwa wafu, wanaume hawaoe na wanamuke hawaolewe, lakini wao ni kama malaika wa mbinguni. Hata hivyo, kuhusu kufufuliwa kwa wafu, je, hamukusoma katika kitabu cha Musa, katika habari kuhusu ule muti mudogo wa miiba, kwamba Mungu alimuambia: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo’? Yeye haiko Mungu wa wafu, lakini ni Mungu wa wazima. Mumekosea sana.” (Marko 12:24-27; Kutoka 3:1-6) Watu wakashangazwa na jibu lake.

Yesu amewanyamazisha Wafarisayo na Wasadukayo, kwa hiyo, viongozi hawa wapinzani wanajiunga pamoja ili kuja kumujaribu tena. Mwandishi mumoja anamuuliza: “Mwalimu, ni amri gani ndiyo kubwa zaidi katika Sheria?”—Matayo 22:36.

Yesu anajibu: “Ya kwanza ni hii, ‘Sikia, Ee Israeli, Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja, na unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.’ Ya pili ni hii, ‘Unapaswa kumupenda jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Hakuna amri nyingine yenye kuwa kubwa zaidi kuliko hizi.”—Marko 12:29-31.

Wakati ule mwandishi alisikia jibu hilo, akajibu hivi: “Mwalimu, umesema muzuri kupatana na kweli, ‘Yeye ni Mumoja, na hakuna mwingine isipokuwa yeye’; na mutu kumupenda kwa moyo wake wote, na kwa uelewaji wake wote, na kwa nguvu zake zote, na pia kumupenda jirani yake kama yeye mwenyewe ni muzuri sana kuliko matoleo yote mazima ya kuteketezwa na zabihu.” Halafu Yesu, wakati alitambua kwamba amejibu kwa hekima, akamuambia: “Wewe hauko mbali na Ufalme wa Mungu.”—Marko 12:32-34.

Kwa muda wa siku tatu (Nisani 9, 10, na 11) Yesu amekuwa akifundisha katika hekalu. Watu fulani, kama vile ule mwandishi, wamefurahia kumusikiliza. Lakini hapana viongozi wa dini, wenye sasa ‘hawawezi tena kumuuliza ulizo.’